Watanzania tuige mfano wa Ujerumani, tunapaswa kumsahau Magufuli na kuweka bidii kusonga mbele

Watanzania tuige mfano wa Ujerumani, tunapaswa kumsahau Magufuli na kuweka bidii kusonga mbele

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Sidhani kama kuna Mtanzania ambae hajui mazuri ya Magufuli akiwa raisi wa Tanzania, atapinga kwamba Magufuli hakuwa na roho ya uzalendo kwa Tanzania, alichukia ufisadi, alichukia watu ambao anawaona walikwamisha bidii zake za kuindeleza Tanzania. Hakuna Mtazania atakaepinga kwamba Magufuli alikuwa mchapa kazi kweli kweli, mwenye kupenda nchi yake na raia wa Tanzania, mzalendo namba moja.

Lakini hilo linakukumbusha nini?

Linatukumbusha kiongozi aliewahi kuwa na hulka ya Magufuli pale Germany, Adolf Hitler. Hitler alikuwa mzalendo kweli kweli. Alisimamia Germany na kuifanya Germany kuwa taifa lenye uchumi wenye nguvu kuliko mataifa yote. Alipenda uzalendo, alichukia ufisadi na usaliti dhidi ya nchi yake. Hitler alikuwa muasisi wa gari za VW, Volks Wagen (People's Car) ili kila raia wa Germany aweze kumudu kuwa na gari. Hakuna kiongozi katika Germany anaeweza kusemwa alileta maendeleo kwa nchi yake kama alivyofanya Hitler, mzalendo namba moja wa nchi yake.

Lakini sasa, nani leo unamsikia akimsifia Hitler kwa makubwa aliyoifanyia Germany? Hakuna, kwa sababu hakuna mtu aliyesahau machungu yaliyosababishwa na Hitler.

Hakuna mtu hapa Tanzania asiyejua machungu yaliyoletwa na Magufuli katika azma yake ya kuiendeleza Tanzania, machungu ambayo hayana utetezi hata uyaangalie kwa mtazamo upi. Hayana justification.

Hata hivyo, kwa tulio hai, kuwachukia Hitler au Magufuli, ambao tayari wamekufa, ni dalili kwamba tuna matatizo ya afya ya akili, tunahitaji psychiatric help. Kuwasifia pia ni tatizo, kwa sababu tunaumiza wale walioumizwa nao, ambao bado wapo hai pamoja nasi. Tutapanda gari za VW za Hitler, tutapita kwenye flyover za Magufuli, lakini hatutaimba sifa zao.

Kama Germany ilivyoamua kumsahau Hitler pamoja na mazuri aliyoifanyia nchi yake, Tanzania tunapaswa kumsahau Magufuli pamoja na mazuri aliyoifanyia nchi yetu.

Tuangalie mbele sasa. Tusahau yaliyopita, tuachane na kulinganisha uongozi wa sasa na uliopita. Tuvunje magenge. Tuanze upya.

The world and your country need YOU now, not Hitler, not Magufuli.
 
Uzalendo ni dhana inayobidi kurejewa na kuangaliwa kwa kina.

Hitler alikuwa mzalendo?

Ukianzisha vita ya kijinga itakayoifanya nchi yako iangamizwe na watu wako wengi kuuawa, ukawabagua raia wa nchi yako wengi na kuwaua, je, wewe ni mzalendo?
 
Uzalwndo ni dhana inayobidi kurejewa na kuangaliwa kwa kina.

Hitler alikuwa mzalendo?

Ukianzisha vita ya kijinga itakayoifanya nchi yako iangamizwe na watu wako wengi kuuawa, ukawabagua raia wa nchi yako wengi na kuwaua, je, wewe ni mzalendo?
Swali zuri sana

Nasubiria mleta mada akujibu
 
Uzalwndo ni dhana inayobidi kurejewa na kuangaliwa kwa kina.

Hitler alikuwa mzalendo?

Ukianzisha vita ya kijinga itakayoifanya nchi yako iangamizwe na watu wako wengi kuuawa, ukawabagua raia wa nchi yako wengi na kuwaua, je, wewe ni mzalendo?
Ujinga wa mtu sio kipimo cha uzalendo. Hitler alikuwa mzalendo kweli kweli, labda kama una maana nyingine ya uzalendo. Lolote alilofanya alifanya kwa nguvu zote kwa ajili ya mapenzi kwa nchi yake. Na katika Wa-Germany aliowaua Hitler, aliwaona kuwa sio wazalendo, wasaliti.
 
Mtanikumbuka
Hapana. Tutakusahau kwa faida ya Tanzania! Lolote linakalotokea baada ya wewe kuondoka tuta deal nalo katika mazingira yaliyopo. Hatutalia kwamba tuna mafisadi kwa sababu Magufuli hayupo - kwa kuwa hilo halituondolei mafisadi. Tunapaswa ku-deal nao sasa, bila kumtaja Magufuli.
 
Magu alikuwa katili na mbinafsi Sana haya uwanja WA ndege kijijini kwake Chato alijijengea alikuwa mshamba Fulani hivi
 
Umefananisha Simba na Nyani.

Mifano yako Haina uhusiano sawa.

JPM awe kama Hitler kweli? Au unahadithi za vijiweni?
 
Ujinga wa mtu sio kipimo cha uzalendo. Hitler alikuwa mzalendo kweli kweli, labda kama una maana nyingine ya uzalendo. Na katika Wagermany aliowaua Hitler, aliwaona kuwa sio wazalendo, wasaliti.
Uzalendo ni nini?

Baba yako akimuua mama yako na kuichoma moto nyumba yenu akisema kwa sababu anaamini kufanya hivyo ni kuipenda familia yake, je, kufanya hivyo kutakuwa ni kuipenda familia yake kweli?
 
Sidhani kama kuna Mtanzania ambae hajui mazuri ya Magufuli akiwa raisi wa Tanzania, atapinga kwamba Magufuli hakuwa na roho ya uzalendo kwa Tanzania, alichukia ufisadi, alichukia watu ambao anawaona walikwamisha bidii zake za kuindeleza Tanzania. Hakuna Mtazania atakaepinga kwamba Magufuli alikuwa mchapa kazi kweli kweli, mwenye kupenda nchi yake na raia wa Tanzania, mzalendo namba moja.

Lakini hilo linakukumbusha nini?

Linatukumbusha kiongozi aliewahi kuwa na hulka ya Magufuli pale Germany, Adolf Hitler. Hitler alikuwa mzalendo kweli kweli. Alisimamia Germany na kuifanya Germany kuwa taifa lenye uchumi wenye nguvu kuliko mataifa yote. Alipenda uzalendo, alichukia ufisadi na usaliti dhidi ya nchi yake. Hitler alikuwa muasisi wa gari za VW, Volks Wagen (People's Car) ili kila raia wa Germany aweze kumudu kuwa na gari. Hakuna kiongozi katika Germany anaeweza kusemwa alileta maendeleo kwa nchi yake kama alivyofanya Hitler, mzalendo namba moja wa nchi yake.

Lakini sasa, nani leo unamsikia akimsifia Hitler kwa makubwa aliyoifanyia Germany? Hakuna, kwa sababu hakuna mtu aliyesahau machungu yaliyosababishwa na Hitler.

Hakuna mtu hapa Tanzania asiyejua machungu yaliyoletwa na Magufuli katika azma yake ya kuiendeleza Tanzania, machungu ambayo hayana utetezi hata uyaangalie kwa mtazamo upi. Hayana justification.

Hata hivyo, kwa tulio hai, kuwachukia Hitler au Magufuli, ambao tayari wamekufa, ni dalili kwamba tuna matatizo ya afya ya akili, tunahitaji psychiatric help. Kuwasifia pia ni tatizo, kwa sababu tunaumiza wale walioumizwa nao, ambao bado wapo hai pamoja nasi. Tutapanda gari za VW za Hitler, tutapita kwenye flyover za Magufuli, lakini hatutaimba sifa zao.

Kama Germany ilivyoamua kumsahau Hitler pamoja na mazuri aliyoifanyia nchi yake, Tanzania tunapaswa kumsahau Magufuli pamoja na mazuri aliyoifanyia nchi yetu.

Tuangalie mbele sasa. Tusahau yaliyopita, tuachane na kulinganisha uongozi wa sasa na uliopita. Tuvunje magenge. Tuanze upya.

The world and your country need YOU now, not Hitler, not Magufuli.
Tungemsahau kama Serikali ya Samia isingeyakumbatia majizi Sugu!! Yaani Mwigulu ni Waziri wa fedha kabsaa halafu tumsahau Mzalendo Magufuli? Makamba na Nape kabsaa!!! Haoana hapana lazima tutabaki na Magufuli katika mioyo yetu
 
Uzalendo ni nini?

Baba yako akimuua mama yako na kuichoma moto nyumba yenu akisema kwa sababu anaamini kufanya hivyo ni kuipenda familia yake, je, kufanya hivyo kutakuwa ni kuipenda familia yake kweli?
Inawezekana ndio. Katika vita za wenyewe kwa wenyewe, kumbuka sababu ni uzalendo. Raia wanauwawa, wanawake nk, kwa jina la uzalendo. Kwa hiyo uzalendo hauangalii logic, na kuna wakati unatoka nje ya kuwa reasonable. Uzalendo (patriotisn, nationalism) mara nyingine unahalalisha kuua wale ambao wanaonekana sio wazalendo, tena mara nyingine kwa mateso sana.

Katika kupigania haki na usawa Afrika Kusini, wale waliojiona wazalendo waliona ni halali kuwachoma moto watu wengine kwa kutumia tairi shingoni kwa sababu kushirikiana kwao na makaburu kulionwa kuwa sio uzalendo. Na japo waliofanya hivyo walijulikana baada ya uchaguzi wa 1994, hadi leo wanaonwa kuwa wazalendo waliopigania haki na usawa
 
Maendeleo ya kuwafanya wananchi kwa angalau wawe na usawa yaani kupunguza tabaka la wenye nacho na wasio nacho, kati yake lazima kuna mmoja aumie

Kile ambacho alikuwa akikifanya Magufi ni kujaribu kupunguza tabaka hilo, kitu ambacho kiliwaumiza wenye nacho na wale ambao walikuwa wapo kwenye milija ya ulaji

Na ndiyo maana JPM ataendelea kukumbukwa na mamilioni ya Watanzania walala hoi ambao ndio alikuwa akiwatetea na shabaha yake ni kuwasogeza kwenye hali ya unafuu wa maisha, na ndiyo maana alijaribu hata kuruhusu kila mtu ajitafutie riziki lake popote pale mpaka hapo serikali inapowatengenezea mazingira rasimi ya kufanyia biashara zao

Vongozi wa aina hii huwa wachache mno, wengi wao wa viongozi, hujikuta wakiendelea kuwatengenezea mazingira mazuri kwa walionacho tu na kuwaongezea zaidi na zaidi na kuwasahau kabisa hao wanaojaribu bahati zao katika kujitafuta

Na kamwe, Magufuli ataendelea kuchukiwa na hao hao ambao JPM alijaribu kuziba mirija ya ukwapuaji

Na kwa sababu hiyo, Wale ambao wako upande wa Magufuli kumtetea kwa nguvu zote bila kujali na wasiamini wasemayo hao wanaosema waliumizwa, ni hao mamilioni ya Watanzania walala hoi na mimi nikiwemo na wala siwezi kujificha kwa sababu tu ya hao ambao wameifanya nchi hii kama mali ya babu zao!


Synthesizer Umeongelea jambo mhimu sana mkuu, binafsi nakuunga mkono, ila viongozi wajitahidi mno kuwatendea haki wananchi wote ilikwa pamoja tugawane sote hiyo keki ya Nchi yetu
 
Hapana. Tutakusahau kwa faida ya Tanzania! Lolote linakalotokea baada ya wewe kuondoka tuta deal nalo katika mazingira yaliyopo. Hatutalia kwamba tuna mafisadi kwa sababu Magufuli hayupo - kwa kuwa hilo halituondolei mafisadi. Tunapaswa ku-deal nao sasa, bila kumtaja Magufuli.
Magufuli ni sehemu ya historia ya Tanzania. Huwezi kukwepa kumtaja.

Umpende, usimpende, ni historia.

Historia haikwepeki.

Na kama humpendi Magufuli, ukikwepa kumtaja Magufuli, unaongeza nafasi ya mabaya aliyoyafanya Magufuli unayoyachukia yajirudie.

Na kama unampenda Magufuli, ukikwepa kumtaja Magufuli, unaonheza nafasi ya mazuri aliyoyafanya Magufuli unayoyapenda yasijirudie.

Kwa hivyo, watu wote, wanaonpenda na wasiomoenda Magufuli, wana sababu kubwa na nzuri kujifunza historia na kuepuka mabaya na kudumisha mazuri aliyoyafanya Magufuli.

Ndiyo maana Magufuki ataendelea kutajwa kwa miaka na miaka.

Hata Nero aliyemuua mama yake mwenyewe na kutuhumiwa kuunguza Roma na Caligula aliyemchagua farasi wake kuwa Senator wa Roma, bado wanatajwa mpaka leo, licha ya vituko vyao vyote.
 
Back
Top Bottom