Watanzania wenzangu, ni ukweli usiopingika kwamba sekta ya mafuta na gesi imefungua fursa kwa wawekezaji wakubwa na wadogo katika taifa letu, na kutoa mwanya kwa wale wanaotaka kuwa wajasiriamali katika sekta hii.
Sekta hii imendelea kutengeneza utajiri kwa wawekezaji mbalimbali waliojizatiti kuwekeza hasa wawekezaji wakigeni.
Lakini inavunja moyo sana asilimia kubwa ya Watanzania bado wako kwenye benchi wanasubiri kwa sababu ya ukosefu wa taarifa ambazo ndio leo nakuja kuzitoa kwenye jukwaa hili waziwazi.
Watanzania wajasiriamali tunaakili sana lakini tunacheza kidogo sana katika tasnia ya mafuta na gesi.
Ukweli mchungu ni kwamba uchumi wetu wa ndani utaweza kubadilishwa na kuwa bora zaidi kwa ushiriki wetu mkubwa kwenye uwekezaji katika hii Sekta wala sio wageni.
Kwa nini tunasubiri hadi sasa wakati wengine wamechukua maeneo yote mazuri kwenye tasnia ya mafuta na gesi? Ila bado hatujachelewa.
Ingawa fursa katika tasnia ya mafuta na gesi zinaweza kuonekana kama zinahitaji mtaji mkubwa, lakini kuna fursa nzuri tu za uwekezaji mdogo katika tasnia hii.
Haijalishi ukubwa wa mfuko wako, ukitazama kwa umakini, bado utagundua fursa za biashara ndogo ndogo unazoweza kuwekeza na kuleta ushiriki wako katika sekta hii.
Fursa za Biashara Zenye Faida Katika Sekta ya Mafuta na Gesi Katika Taifa letu
8. Kuanzisha kampuni ya Ushauri
Ingawa makampuni mengi ya ushauri katika taifa letu yamejielekeza kwenye uhandisi na ushauri wa miradi, lakini kuna pengo katika soko ambalo linahitaji mwongozo, msaada, na rasilimali kwa wawekezaji wanaomiliki au wanaotaka kuanzisha biashara katika sekta ya mafuta na gesi.
Hivyo, unaweza kujaza pengo hili kwa kuanzisha kampuni yako ya ushauri na kutoa msaada wa kibiashara kwa watu wanaotaka kuanzisha biashara endelevu katika sekta ya mafuta na gesi.
Biashara hii ya ushauri inafaa zaidi kwa watu ambao hawana mtaji mkubwa wa kujitosa katika biashara ghali ya mafuta na gesi lakini wanao ujuzi wa kina uliojikita katika sekta ya mafuta na gesi.