Watanzania tuwe na huruma, tuwasamehe Bongo Movie.

Watanzania tuwe na huruma, tuwasamehe Bongo Movie.

Hakuna msamaha kwa watu wanaoendekeza njaa mpaka kurubuniwa na Bashite kuandamana. Bashite atanunua movie zao, nina kama miaka 3 sijaangalia kabisa uchafu huo, hata watoto hawataki kabisa, wataka series labda sana comedy kama kina Majuto lkn Jb tumbo kubwa akili kiduchu
Kosa lao ni kutaka wote walipe kodi sawa au makonda kuwasaidia wasanii wa mkoa wake kwa kuimplement maagizo ya nape na mwakyembe?
 
Wamefanya makosa gani? Wengi wao kuwa upande wa ccm ni kosa? Kulalamika kuibiwa kwa kazi zao through piracy ni kosa? Kuilalamikia serikali iweke uwanja sawa wa soko baina yao na wauza cd za nje kwa kulipa kodi sawia hilo nalo ni kosa?
Katika hali ya kawaida na kwa uelewa wako ndogo wa mambo unadhani kuna usawa kati ya muvi za nje na za ndani kwamba wakiweka mazingira sawa ya ushindani basi bongo mavi watatoboa?

Nikusaidie tu, hata wakiweka kodi mara tatu kwenye movie za nje na movie za bongo mavie wakaondoa kodi au wakagawa bure bado watu watanunua za nje na kuacha bongo mavi zikidoda.
 
Waambie waache kuwaandama wauzaji wa CD za nje pale kariakoo...kuzuia movie za nje haimaanishi kuwa za ndani ndio zitauza zaidi..

BTW tuko kwenye soko huria, mtu anachagua apendacho..Wajiulize kwa nini movie zao hazipendwi lakini za nje zinapendwa?? Wakishajirekebisha ndio tutawasamehe la sivyo kama mbwai mbwai tu!
 
Uko sahihi!

Kosa lao kubwa ni kujiingiza kwny Siasa sio ubora wa kazi zao kwa kuwa kila kitu bongo ni cha kufoji kasoro forgery yenyewe ndio forgery halisi!

Tukianza pia kujadili Siasa za Vyama vyetu na Timu zetu za Mpira tutagundua ni vichekesho kuliko hata hao Wachekeshaji wa Bongo Movie.

Naskia Kamisaa na Refa wa Mechi ya Africa. Lyon vs Kagera Sugar wanatoafautiana katika Matokeo ya Mechi hiyo kila mmoja Ana record tofauti na Mwenzake!
Kuna kosa gani kujiusisha kwenye siasa wakati ni haki yao kikatiba?
 
Watakunya, washenzi Sana na huyo Steve Nyerere wao, eti kanasema Siku ile katakuwa ka mwisho kutoka ccm,
Sikapendi kale Kajamaa na jinsi kalivyo utadhani kanaishi Kwa kula dozi ya mfuko wa cement, kamekomaa na kufubaa utadhani kachawi.
Shwaini sana na bado, nchi nzima imewachukia
Imewachukia kwa nini?
 
Habari ya wakati huu wakuu.

Sisi watanzania tunafahamika kwa ukarimu na roho nzuri, upendo na kusaidiana, tabia ambayo mwalimu alitufundisha.

Lakini pia sisi ni watu wabaya sana kama mtu atatuudhi, kwa jinsi watanzania mlivyowawakia bongo muvie ni dhahiri kua hao watu wametukwaza sana.

Bongo movie watuudhi na kutughadhabisha sana, katika mitandao yote inayofahamika hapa nchini na blogs naona ni kuwashambulia wasanii wa bongo movie.

Mimi niwaombe ndugu zangu, hawa ni ndugu na jamaa zetu, ni wanetu na wazazi wetu, kama ni watu wenye akili saaa watajirekebisha kwa jinsi walivyosakamwa iwa kazi yao mbovu na kujiingiza katika vita isiyowahusu ya kurubuniwa na DAB mtu ambae amekosa ile wataalam wanaita "moral authority" ya kukemea au kuelekeza lolote liwe baya au zuri kutokan na kukosa kuaminika.

Niombe, hawa watu kama wana akili watajirudi, najua wametambua makosa yao, naomba tuwasamehe tuwape nafasi nyingine vinginevyo tutawaua kwa msongo wa mawazo na msukumo mkubwa wa damu.

Imetosha, tumewasema vya kutosha, kila mahali ukifungua watu wanaponda tu hawa bongo movie, tuwahurumie ndugu zangu, wao pia ni watu wanafanya makosa kama sisi sote tunavyofanya makosa.

Ni hayo tu ndugu zangu.
Tatizo ni kwamba Jambazi anavua viatu mlangoni na jini anaangalia bara bara kama inamagari.
 
Katika hali ya kawaida na kwa uelewa wako ndogo wa mambo unadhani kuna usawa kati ya muvi za nje na za ndani kwamba wakiweka mazingira sawa ya ushindani basi bongo mavi watatoboa?

Nikusaidie tu, hata wakiweka kodi mara tatu kwenye movie za nje na movie za bongo mavie wakaondoa kodi au wakagawa bure bado watu watanunua za nje na kuacha bongo mavi zikidoda.
Kwanza uwanja uwe sawa huku wanarekebisha kasoro zingine. hakuna mfanyabiashara duniani atakayekubali kuona mshindani wake halipi kodi kama yeye.
 
Katika hali ya kawaida na kwa uelewa wako ndogo wa mambo unadhani kuna usawa kati ya muvi za nje na za ndani kwamba wakiweka mazingira sawa ya ushindani basi bongo mavi watatoboa?

Nikusaidie tu, hata wakiweka kodi mara tatu kwenye movie za nje na movie za bongo mavie wakaondoa kodi au wakagawa bure bado watu watanunua za nje na kuacha bongo mavi zikidoda.
Kwanza uwanja uwe sawa huku wanarekebisha kasoro zingine. hakuna mfanyabiashara duniani atakayekubali kuona mshindani wake halipi kodi kama yeye.
 
Waambie waache kuwaandama wauzaji wa CD za nje pale kariakoo...kuzuia movie za nje haimaanishi kuwa za ndani ndio zitauza zaidi..

BTW tuko kwenye soko huria, mtu anachagua apendacho..Wajiulize kwa nini movie zao hazipendwi lakini za nje zinapendwa?? Wakishajirekebisha ndio tutawasamehe la sivyo kama mbwai mbwai tu!
Unaamini kuwa wasanii wanaweza kuzuia wengine wasiuze cd? Wana mandate gani ya kufanya hivyo? Hata makonda hana mandate hiyo.
 
Kuna kosa gani kujiusisha kwenye siasa wakati ni haki yao kikatiba?
Sio kila kitu ambacho ni haki yako kikatiba n kisheria basi unaweza kukidai tu, wakati mwingine unatumia akili na busara.

Viongozi wa dini wana haki kisheria na kikatiba kujihusisha na siasa, ila wanashauriwa kutumia akili na busara ili wasiwagawe waumini wao.

Tatizo sio sheria au haki kikatiba, tatizo ni kutotumia akili na busara kulingana na mazingira na wakati.
 
Kawaambie waombe radhi. Wamuite na DAB wao na press waombe radhi.
 
Sio kila kitu ambacho ni haki yako kikatiba n kisheria basi unaweza kukidai tu, wakati mwingine unatumia akili na busara.

Viongozi wa dini wana haki kisheria na kikatiba kujihusisha na siasa, ila wanashauriwa kutumia akili na busara ili wasiwagawe waumini wao.

Tatizo sio sheria au haki kikatiba, tatizo ni kutotumia akili na busara kulingana na mazingira na wakati.
Hiyo sio sab ya msingi kwa sab sio wasanii wote wamejiingiza kwenye siasa. Tumeshuhudia wasanii wengi wamejihusisha kwenye siasa mbona masoko ya kazi hayajashuka? Ney wa mitego ameifanyia kampeni chadema wazi wazi mbona anaendelea kujaza watu kwenye show zake? Diamond amefanya kampeni za ccm na ni shabiki wa makonda kada wa ccm lkn anazidi kufanya vizuri sokoni? Hiyo ni mifano michache. Soko la bongo movie limeanza kushuka miaka zaidi ya mitano iliyopita na kilio chao kimeanza siku nyingi kabla ya magufuli wamekuwa wanalalamika mfululizo na wakaanza kusikilizwa kwa kuteuliwa mwakilishi kwenye bunge maalum la katiba na hatimaye kutambuliwa kwenye katiba inayopendekezwa. Yanayoendelea sasa ni mwendelezo wa malalamiko yao ya muda mrefu. Utahusishaje siasa ya 2015 wakati matatizo yao yapo miaka mingi nyuma?
 
Back
Top Bottom