Watanzania tuwe na huruma, tuwasamehe Bongo Movie.

Kosa lao ni kutaka wote walipe kodi sawa au makonda kuwasaidia wasanii wa mkoa wake kwa kuimplement maagizo ya nape na mwakyembe?
 
Wamefanya makosa gani? Wengi wao kuwa upande wa ccm ni kosa? Kulalamika kuibiwa kwa kazi zao through piracy ni kosa? Kuilalamikia serikali iweke uwanja sawa wa soko baina yao na wauza cd za nje kwa kulipa kodi sawia hilo nalo ni kosa?
Katika hali ya kawaida na kwa uelewa wako ndogo wa mambo unadhani kuna usawa kati ya muvi za nje na za ndani kwamba wakiweka mazingira sawa ya ushindani basi bongo mavi watatoboa?

Nikusaidie tu, hata wakiweka kodi mara tatu kwenye movie za nje na movie za bongo mavie wakaondoa kodi au wakagawa bure bado watu watanunua za nje na kuacha bongo mavi zikidoda.
 
Waambie waache kuwaandama wauzaji wa CD za nje pale kariakoo...kuzuia movie za nje haimaanishi kuwa za ndani ndio zitauza zaidi..

BTW tuko kwenye soko huria, mtu anachagua apendacho..Wajiulize kwa nini movie zao hazipendwi lakini za nje zinapendwa?? Wakishajirekebisha ndio tutawasamehe la sivyo kama mbwai mbwai tu!
 
Kuna kosa gani kujiusisha kwenye siasa wakati ni haki yao kikatiba?
 
Imewachukia kwa nini?
 
Tatizo ni kwamba Jambazi anavua viatu mlangoni na jini anaangalia bara bara kama inamagari.
 
Kwanza uwanja uwe sawa huku wanarekebisha kasoro zingine. hakuna mfanyabiashara duniani atakayekubali kuona mshindani wake halipi kodi kama yeye.
 
Kwanza uwanja uwe sawa huku wanarekebisha kasoro zingine. hakuna mfanyabiashara duniani atakayekubali kuona mshindani wake halipi kodi kama yeye.
 
Unaamini kuwa wasanii wanaweza kuzuia wengine wasiuze cd? Wana mandate gani ya kufanya hivyo? Hata makonda hana mandate hiyo.
 
Kuna kosa gani kujiusisha kwenye siasa wakati ni haki yao kikatiba?
Sio kila kitu ambacho ni haki yako kikatiba n kisheria basi unaweza kukidai tu, wakati mwingine unatumia akili na busara.

Viongozi wa dini wana haki kisheria na kikatiba kujihusisha na siasa, ila wanashauriwa kutumia akili na busara ili wasiwagawe waumini wao.

Tatizo sio sheria au haki kikatiba, tatizo ni kutotumia akili na busara kulingana na mazingira na wakati.
 
Kawaambie waombe radhi. Wamuite na DAB wao na press waombe radhi.
 
Hiyo sio sab ya msingi kwa sab sio wasanii wote wamejiingiza kwenye siasa. Tumeshuhudia wasanii wengi wamejihusisha kwenye siasa mbona masoko ya kazi hayajashuka? Ney wa mitego ameifanyia kampeni chadema wazi wazi mbona anaendelea kujaza watu kwenye show zake? Diamond amefanya kampeni za ccm na ni shabiki wa makonda kada wa ccm lkn anazidi kufanya vizuri sokoni? Hiyo ni mifano michache. Soko la bongo movie limeanza kushuka miaka zaidi ya mitano iliyopita na kilio chao kimeanza siku nyingi kabla ya magufuli wamekuwa wanalalamika mfululizo na wakaanza kusikilizwa kwa kuteuliwa mwakilishi kwenye bunge maalum la katiba na hatimaye kutambuliwa kwenye katiba inayopendekezwa. Yanayoendelea sasa ni mwendelezo wa malalamiko yao ya muda mrefu. Utahusishaje siasa ya 2015 wakati matatizo yao yapo miaka mingi nyuma?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…