Watanzania Wawili wakamatwa South Africa na Madawa




HUKU skendo ya kunaswa akiwa na madawa ya kulevya ikiendelea kumtesa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, Video Queen maarufu Bongo, Agnes Gerald ‘Masogange' anatarajiwa kupandishwa kortini nchini Afrika Kusini leo kujibu shitaka ambalo mwenyewe hajaliweka wazi, Ijumaa linakupasha.


Agnes Gerald ‘Masogange'.
AWALI YA YOTE
Mwishoni mwa wiki iliyopita, habari ya mjini ilikuwa Masogange kanaswa na madawa ya kulevya nchini Afrika Kusini.
Habari zilisambaa kwamba sanjari na Masogange, mwingine aliyenaswa naye ni mdogo wake (mtoto wa mama yake mdogo Agnes) aitwaye Melisa Edward.
Kwa mujibu wa habari hiyo ya mjini, wawili hao walinaswa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oriver Tambo uliopo Kempton Park siku ya Ijumaa wiki iliyopita wakitokea Tanzania wakiwa na ‘mzigo' wa kilo nyingi aina ya ‘crystal methamphetamine' wenye thamani ya shilingi za Kitanzania bilioni 6.8!

IJUMAA LAANZA KUSAKA UKWELI
Baada ya kunasa habari hiyo, Ijumaa liliingia mzigoni kuusaka ukweli ambapo hata hivyo, madai hayo yalikuwa yakijifungafunga sana.
Mtu mmoja wa karibu na Masogange alipoulizwa kuhusu ukweli au uongo wa habari hiyo alikuwa na haya ya kusema:
"Ni kweli Agnes amekamatwa akiwa na madawa ya kulevya kule Sauzi. Lakini si yenye thamani hiyo ya bilioni sita bali ni milioni arobaini tu. Hata hivyo, ameachiwa kwa dhamana ila paspoti yake imezuiliwa.
"Nadhani kuna mambo yanawekwa sawa ikiwezekana atarudi nyumbani."
JIJINI DAR, KAMANDA WA KUPAMBANA NA MADAWA YA KULEVYA ANENA
Jumatatu iliyopita, Kamanda wa Polisi wa Kikosi cha Kudhibiti Madawa ya Kulevya Tanzania, Godfrey Nzowa aliviambia vyombo vya habari kuwa, Watanzania wawili walikamatwa nchini Afrika Kusini na mamlaka ya mapato wakiwa na madawa ya kulevya kutoka Tanzania yenye thamani ya shilingi bilioni 6.8.
Kamanda Nzowa aliwataja Watanzania hao kuwa ni Agnes Gerald ambaye ana miaka 25 na Melisa Edward mwenye miaka 24. Alisema wawili hao baada ya kukamatwa na chombo hicho walikabidhiwa kwa polisi ambapo mahojiano yanaendelea.


IJUMAA LAMWIBUKIA KAMANDA NZOWA
Baada ya Kamanda Nzowa kuwataja kwa majina wawili hao Jumatatu iliyopita, siku iliyofuata, Ijumaa lilipiga hodi kwenye ofisi za kamanda huyo kwa lengo la kutaka kujua kama Agnes Gerald aliyemtaja jana yake ni Masogage au majina yanafanana tu.
Kamanda huyo hakuwepo ofisini kwake asubuhi hiyo na kwa mujibu wa wasaidizi wake, alikuwa kwenye kikao cha dharura kwenye Ofisi za Polisi wa Kimataifa ‘Interpol'.
APIGIWA SIMU
Ilibidi Ijumaa limsake kwa njia ya simu ya kiganjani kwa mara kadhaa. Alipopokea akaulizwa kuhusu Agnes Gerald aliyemtaja kama ni Masogange yule staa.
Kamanda Nzowa: "Eee, mimi siwezi kusema ni huyo, ninachojua ni Agnes Gerald tu basi. Sasa kama ni Masogange mimi sifahamu lolote."


JUMANNE USIKU SIMU KUTOKA SAUZI
Mpaka hapo, timu nzima iliyokuwa ikifuatilia habari hiyo haikuona ukweli wa Agnes Gerald kuwa ni Masogange na kwa vile siku zote Global Publishers inasimamia utafiti kabla ya kuandika habari iliamua kuiweka pembeni kwanza ili kuendelea kuichimba.
Saa 2:14 usiku wa siku hiyo, Ijumaa lilipokea simu yenye kuashiria wito (code number) ni ya nje na kabla haijapokelewa, ilibainika ni ya Afrika Kusini.
Ijumaa: Haloo.
Sauti: Haloo, mimi Masogange.
Ijumaa: Mambo Agnes, pole sana na mkasa uliokupata bwana, pole sana.
Agnes: Kwanza naumizwa sana na maneno ambayo watu wanazidi kuyaeneza sehemu mbalimbali bila kuwa na uhakika wowote, mimi sikukamatwa kwa sababu ya madawa ya kulevya.
"Mkasa nilioupata siyo ambao watu wanaueneza kwenye mitandao mbalimbali na katika vyombo ya habari."
Ijumaa: Kwa hiyo madai ya kukutwa na madawa ya kulevya si ya kweli?
Agnes: Kweli nilikamatwa huku kwa matatizo f'lan ila siyo ishu ya madawa kama watu wanavyosambaza.
Ijumaa: Ni tatizo gani sasa?
Agnes: Unajua sipendi tena kuwapa watu faida ila lilikuwa ni tatizo la kawaida, nilikamatwa na baada ya hapo nilitoka na niko huru. Nasubiri tu kwenda mahakamani Ijumaa (leo) mara moja kisha n'tarudi Bongo.
Ijumaa: Mh! Sasa Egg, mbona huku mpaka viongozi wa polisi wamesema ni madawa?
Agnes: Hapana, siyo, ipo ishu ndogo tu.
Ijumaa: Haya pole sana kwa misukosuko.
Agnes: Asante sana, nitakuja huko siku si nyingi.
Habari hii imeandikwa na Imelda Mtema, Haruni Sanchawa na Musa Mateja.

 
nilivyosikia polisi wanaenda uko south nilijua tu wanaenda kuweka mipango sawa waachiwe.

habari ya juzi imenisikitisha kusikia madawa yanalindwa na wanajesh na polis bandarini.

huu mpambano umetushinda .
 
kwa kuwa ni gazeti la udaku habari hii naiweka kapuni kwanza,ila vyovyote vile inaweza kuwa,kama jinsi tulivyo sikia kwa cowbama kuwa kuwa alitumia kiasi kikubwa cha madawa mpaka kupelekea kifo ,kumbe haikuwa hivyo ila nikupotosha ukweli,hata hili inaweza kuwa kweli
 
du nachoka kabsa hapa kuna kitu cyo bure ..... Mkulu nina wac wac naye
 
yaani watu hawakuona kitu chochote cha kuwasingizia waibuke na Sembe

Lisemwalo lipo kama halipo sijui huwa wanamaziliaje ati .............
 
Natamani Kunywa sumu maana hatujui uongo ni upi na ukweli ni upi
 
Ishu ni madawa wasitake kupotosha ukweli wale askari walikwenda kuweka mambo sawa ni biashara za wakubwa na pia ni viburudisho vyao lazima watawato WAKUBWA BILA MADAWA YA KULEVYA HAIWEZEKANI
 
Hivi wale jamaa wa wikileaks siku hizi wapo wapi? Maana ndio sehemu yake hii
 
Tukiuza maji baridi typhod,bangi haramu,mihogo na lupilipili ma na luchumvi ma inakolea kosingo kipindupindu.
 
nilivyosikia polisi wanaenda uko south nilijua tu wanaenda kuweka mipango sawa waachiwe.

habari ya juzi imenisikitisha kusikia madawa yanalindwa na wanajesh na polis bandarini.

huu mpambano umetushinda .

Umeona eehh.....!!!!! Huu mpambano kushinda si rahisi.
 
Sasa kwa style hii ya mkulu kuwatetea..ndo anazidi kuwapa vichwa hawa ma drug dealer..coz wanajua yupo wa kuwatetea...ujinga huu..I wsh 2015 ifike
 
nilivyosikia polisi wanaenda uko south nilijua tu wanaenda kuweka mipango sawa waachiwe.

habari ya juzi imenisikitisha kusikia madawa yanalindwa na wanajesh na polis bandarini.

huu mpambano umetushinda .

Hapa kuna viini macho vingi sana mkuu. Ila mwisho wa hila aibu.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Na habar ya leoleo ni kuwa wamefutiwa dhamana baada ya polisi kustukia kuwa wanataka kutoroshwa
 
Sasa kwa style hii ya mkulu kuwatetea..ndo anazidi kuwapa vichwa hawa ma drug dealer..coz wanajua yupo wa kuwatetea...ujinga huu..I wsh 2015 ifike
Yaani,una maanisha Prezidaa anawalinda hawa watu dhidi ya makosa yao binafsi!
 
Ujinga ujinga tu. Eti "nilikamatwa issue ndogo tu sasa niko huru", mara tena "Ijumaa naenda mahakamani", sijui nini . Upambaaaaaaaaaaaaaaaaav mkubwa. issue ndogo na uko huru inakupeleka mahakamani kufanya nini ijumaa? Ndiyo maana China wananyonga. Vimutu kama hivi vinashindwa kusoma halafu vinadhani eti ni vi ana muziki, muziki wenyewe haviwezi vinabaki kuwa makapu ya kusafirishia madawa. Pambavu kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…