Watanzania Wawili wakamatwa South Africa na Madawa

Watanzania Wawili wakamatwa South Africa na Madawa

afadhali kufanya kazi kwa kanjibai mwishoni mwa mwez anakupa elfu 70 pilipili sado moja na kacholi 3. hawa wanasubir kuchomwa sindano za sumu kabla hawajaachiwa waje wafie tz.
 
duh kama ni uyo balaa wamekamatwa na kilo 150 za madawa zenye thamani ya bilioni 6 za kitanzania kweli walijiamini kupita na mzigo mkubwa kama huo haijawaitokea kukamatwa mzigo mkubwa kama huo huko

wasanii wetu haooo, wakija hapo oooh tuna million mia mojaa kweny accounts haya waongee na kamanda nzowaaaa
 
nami nashangaa title yake
huku kilichomo kikikanusa uhalisia wa uraia wao
cha kujiuliza hayo madawa yalipenyaje JKN airport?
jana tumeambiwa wamewakamata tena wawili wakielekea bangkong
nadhani wahusika wataanikwa,, Bil 6 sio mchezo

Nani atakae waanika? hivi huwezi jiuliza kilo 150 zimepitaje Tanzania? nijuavyo mimi hawawezi kujianika na hata wakianikwa hakuna wa kuwakamata, Mbona Rais aliwahi pelekewa list ya ma big Dealer akaaishia kusema viongozi wa dini wanafanya biashara ya madawa ya kulevya nani alikamatwa?
 
Kwa Tanzania sijui hata kama kuna sheria.

Although rarely prescribed, methamphetamine hydrochloride is approved by the U.S. Food and Drug Administration(FDA) for the treatment of attention deficit hyeractivity disorder and obesity under the trade name Desoxyn.

watanzania tuache ushabiki na unafiki..hao wadada wamefanya kipi cha ajabu.mbona amuongelei makontena ya pembe za ndovu yanayokamatwa kila siku na ni mali asili zetu wote..wanachukua hela ili waasi wa nchi za jirani watumie ardhi yetu.meli zinakuja kumwaga uchafu wa nyuklia ktk bahari yetu...EPA,rada na ndege ya raisi wote kimyaa....baba akiwa mlevi,mwizi na mzinzi usitegemee watoto watakuwa waungwana.ni hayo tuuu
 
Ila aiingiii akilini kwa kweli! Sasa alibeba na lift au torori huyo mtoto wa kike? Mifuko 3 ya cement jamani sio mchezo
 
Waliokamatwa na 'unga' wa mabilioni ni mabinti

- Wote ni Watanzania, walianzia safari Dar, washikiliwa Afrika Kusini

NA THOBIAS MWANAKATWE | 9th July 2013


Wanawake wawili raia wa Tanzania wametambuliwa kuwa ndiyo wanaodaiwa kuingiza shehena ya dawa za kulevya zenye thamani ya zaidi ya Sh. bilioni 6.8 nchini Afrika Kusini wakitokea Tanzania.

Akizungumza na NIPASHE jana, Kamanda wa Polisi Kitengo cha Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Geofrey Nzoa, alisema haijafahamika wanawake hao wanatoka mikoa gani.

Kamanda Nzoa aliwataja wanawake hao kuwa ni
Agnes Jerald ambaye alisema hajapiga hesabu ya umri wao, ila alizaliwa mwaka 1988 kwa maana hiyo ana umri wa miaka 25 na Melisa Edward ambaye alisema amezaliwa mwaka 1989 kwa maana hiyo atakuwa na umri wa miaka 24. Wawili hao bado wanaendelea kuhojiwa na polisi wa Afrika Kusini.

Alisema Jeshi la Polisi Nchini kwa upande wake linaendelea kufanya uchunguzi kubaini kama dawa hizo walitoka nazo wapi na pia linawasaka watu ambao watakuwa ndiyo wamiliki wa dawa hizo.

Jumapili iliyopita NIPASHE ilipata taarifa za kukamatwa kwa dawa za kulevya aina ya Crystal Methamphetamine zenye thamani hiyo nchini Afrika Kusini wakati zikisafirishwa kutoka Tanzania.

Taarifa hizo zilionyesha kuwa wanawake wawili walikamatwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Oriver Tambo uliopo eneo la Kempton Park siku ya Ijumaa wiki iliyopita wakitokea Tanzania.

Wanawake hao walikamatwa na maofisa wa Mamlaka ya Mapato ya Afrika Kusini wakiwa na masanduku sita ambayo yalipokaguliwa yalikutwa na takribani kilo 150 za dawa hizo ambazo pia zinajulikana kama ‘Tik’ zikiwa na thamani ya bei ya mtaani ya Randi milioni 42 sawa na Sh. bilioni 6.8.

Baada ya kukamatwa na dawa hizo wanawake hao walikabidhiwa polisi.

Tukio hilo linatoka takribani wiki moja baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Juni 28, mwaka huu kutangaza kuwa tatizo la dawa za kulenya hivi sasa ni janga la kitaifa nchini.

Alisema kumekuwa na wimbi kubwa la Watanzania wanaojiingiza katika biashara haramu ya dawa za kulevya ndani na nje ya nchi na kwamba, katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, watuhumiwa 10,799 walikamatwa kwa kujihusisha na dawa hizo.

Pia alisema katika kipindi hicho, Watanzania 240 walikamatwa katika nchi za Brazil, Pakistan na Afrika Kusini, na hivyo kuharibu taswira ya nchi na kusababisha Watanzania wasio na hatia kupata usumbufu na masharti magumu wanapotaka kusafiri kwenda nchi mbalimbali duniani.

Pinda alisema mwaka huu pekee kumekuwa na ukamataji mkubwa wa dawa za kulevya katika eneo la kimataifa la Bahari ya Hindi karibu na Tanzania.

Alisema hivi sasa mikate, maandazi na askrimu zinazouzwa kwenye shule za msingi, zinawekwa dawa za kulevya.

Alisema vitendo hivyo vinafanya vijana wengi wa shule za msingi na hata sekondari kuwa na tabia za ajabu, ikiwamo kuingia darasani wakiwa na kiatu kimoja mguuni, mkufu wenye nyembe na kidani chenye nyembe kifuani.


CHANZO: NIPASHE Home

###########
Kwa wasomaji

Agnes Gerald, maarufu kama Agnes Masogange Alizaliwa Aprili 23, 1988 kwenye hospitali ya Mkoa wa Mbeya na akasoma Shule ya Msingi na Sekondari ya Sangu.​
Kumbe gazeti la NIPASHE lina waandishi wa habari vihiyo na ambao kazi yao ni ku copy na ku paste,hata bongo zao zimeganda,pia wahariri habari wao pia ni vihiyo,hivi kweli inakuwaje mwandishi hujidadisi mwenyewe kwanza,eti walibeba kilo 150 ,kweli kwenye ndege ya abiria mtu anaweza kubeba kilo 150 za madawa ya kulevya,hata kujihoji wenyewe wanashindwa,kwa hiyo hiyo mifuko mitatu ya sementi ilifichwa kwenye masanduku,hayo ndio matunda ya waandishi na wahariri wa vibahasha vya kaki,kazi kila kukicha kukimbilia kwenye harambee za kuchangia makanisa na kuandika habari za kusifia chama cha Mabugando.
Ningekuwa mi ndi Mzee Machache huyu mwandishi na mhariri leo hii wangekuwa wako mtaani,kwa kushusha hadhi za gazeti makini na kuwa gazeti la udaku
 
watanzania tuache ushabiki na unafiki..hao wadada wamefanya kipi cha ajabu.mbona amuongelei makontena ya pembe za ndovu yanayokamatwa kila siku na ni mali asili zetu wote..wanachukua hela ili waasi wa nchi za jirani watumie ardhi yetu.meli zinakuja kumwaga uchafu wa nyuklia ktk bahari yetu...EPA,rada na ndege ya raisi wote kimyaa....baba akiwa mlevi,mwizi na mzinzi usitegemee watoto watakuwa waungwana.ni hayo tuuu
Na wewe ni wa ajabu ndio maana huoni cha ajabu kilichofanywa, hayo uliyoyazungumza kama ufisadi nk tutapambana nayo vipi wakati rasilimali watu ya kupambana na hayo ambayo kwa asilimia kubwa ni vijana ikiwa imeshaharibiwa na madawa? kumbuka mapambano yanahitaji watu wenye akili timamu sio kila mtu anaweza pambana. kwanza wengi wao wakishapiga hayo madawa wala hawakumbuki kuwa wanaibiwa tembo zao, ndio kwanza wanajiona wanaishi mainchi yaliyoendelea.
 
Majanga, majanga, majanga serikali yetu haiwezi kufuatilia hawa watoto wanapata wapi pesa kwani wao pia ni weziiiiiiiiiii, na wao wakifuatiliwa watasema hizo pesa wanazojenga majumba kila siku wanazitoa wapi???? tukianza kuchunguzana leo hii mbona majanga, majanga, majanga twende tuu mwendo mdundooo, imagine hao wadada walipitaje hapo air port DSM very stupidddd..
 
Kumbe gazeti la NIPASHE lina waandishi wa habari vihiyo na ambao kazi yao ni ku copy na ku paste,hata bongo zao zimeganda,pia wahariri habari wao pia ni vihiyo,hivi kweli inakuwaje mwandishi hujidadisi mwenyewe kwanza,eti walibeba kilo 150 ,kweli kwenye ndege ya abiria mtu anaweza kubeba kilo 150 za madawa ya kulevya,hata kujihoji wenyewe wanashindwa,kwa hiyo hiyo mifuko mitatu ya sementi ilifichwa kwenye masanduku,hayo ndio matunda ya waandishi na wahariri wa vibahasha vya kaki,kazi kila kukicha kukimbilia kwenye harambee za kuchangia makanisa na kuandika habari za kusifia chama cha Mabugando.
Ningekuwa mi ndi Mzee Machache huyu mwandishi na mhariri leo hii wangekuwa wako mtaani,kwa kushusha hadhi za gazeti makini na kuwa gazeti la udaku

mdau ushawahi kupanda ndege[sio pw au fast jet]???
hao madada walikuwa wawili,kila mtu kabeba mabegi matatu[kuna trolley airport] do the math.....kwenye ndege kuna free 30-60 kg allowance depending on flight,sasa kwa hawa wawili inamaana wana free luggage allowance btn 60-120 depending on the flight,sasa lets assume free allowance kwa flight hii ni 45kgx2=90kg....wana 150kg-90kg=60kg....hizo 60kg WANALIPIA AS EXCESS LUGGAGE......very common kwenye ndege watu wanabeba kilo nyingi sana so hamna cha ajabu mtu kubebea 150kg kwenye ndege ya abiria......

how JKNA security couldnt detect 150kg of drugs,thats another question......
 
mdau ushawahi kupanda ndege[sio pw au fast jet]???
hao madada walikuwa wawili,kila mtu kabeba mabegi matatu[kuna trolley airport] do the math.....kwenye ndege kuna free 30-60 kg allowance depending on flight,sasa kwa hawa wawili inamaana wana free luggage allowance btn 60-120 depending on the flight,sasa lets assume free allowance kwa flight hii ni 45kgx2=90kg....wana 150kg-90kg=60kg....hizo 60kg WANALIPIA AS EXCESS LUGGAGE......very common kwenye ndege watu wanabeba kilo nyingi sana so hamna cha ajabu mtu kubebea 150kg kwenye ndege ya abiria......

how JKNA security couldnt detect 150kg of drugs,thats another question......
Kaka kuhusu kupanda sidhani PW au Fast jet zinaenda masafa marefu kwa hiyo najua ninachokisema huwezi beba hizo kilo kwenye ndege ,hapa tatizo sio kulipia au vipi bali ni jinsi ya usafirishwaji wa hizo kilo 150 .Najua hata mizigo inavyosafirishwa kwenye ndege,haiwezekani,na ndio maana hata wale wauza unga waliokubuhu hawawezi beba hizo kilo kwenye ndege za abiria bali hutumia ndege ndogo binafsi au meli /mashua zao kubeba huo mzigo
 
Kaka kuhusu kupanda sidhani PW au Fast jet zinaenda masafa marefu kwa hiyo najua ninachokisema huwezi beba hizo kilo kwenye ndege ,hapa tatizo sio kulipia au vipi bali ni jinsi ya usafirishwaji wa hizo kilo 150 .Najua hata mizigo inavyosafirishwa kwenye ndege,haiwezekani,na ndio maana hata wale wauza unga waliokubuhu hawawezi beba hizo kilo kwenye ndege za abiria bali hutumia ndege ndogo binafsi au meli /mashua zao kubeba huo mzigo

wewe unazungumzia ndege gani???kuna ndege wanatoa free luggage allowance 60kg....transatlantic flights,then ukiwa na extra unalipia kama excess luggage.......hao mademu walikuwa wawili hapo wanakuwa na 120kg luggage allowance,30kg wanalipia excess luggage.....bado kuna carry on unayopanda nayo ndani mwenyewe mkononi 10kg free...
hivi unajua watu wanaenda china wanarudi na nguo mzigo wa dukani kwa ndege badala ya meli???ni hivi mkienda china leets say mko wa4 kila mmoja ana free 60kg,wenzio watatu mzigo wao ni wa container unawapa hela wanakuuzia free luggage allowance yao so unakuwa na 60x3=180kg plus ya kwako 60kg total 240kg....sasa unashangaa kg 150 watu wawili???
cha muhimu begi moja mara nyingi wanaweka limit 30kg,so utabeba mabegi mengi.
 
Nimekubali mkuu. Unajua alinichanganya pale nilipoona anaendelea kupost pics instagram. Kumbe ilikuwa danganya toto.

Town hii usije ukaona jina la mtu FB au Twitter au Instagram ukajua ndio mwenyewe watu wapo kikazi zaidi
 
Majanga, majanga, majanga serikali yetu haiwezi kufuatilia hawa watoto wanapata wapi pesa kwani wao pia ni weziiiiiiiiiii, na wao wakifuatiliwa watasema hizo pesa wanazojenga majumba kila siku wanazitoa wapi???? tukianza kuchunguzana leo hii mbona majanga, majanga, majanga twende tuu mwendo mdundooo, imagine hao wadada walipitaje hapo air port DSM very stupidddd..

Bwana Irizar umeuliza swali zuri kwamba ule mzigo ulipitaje pale DAR!!!!mimi nina imani kabisa kuwa pale Dar waliuona ila wangelipua bomu wangepoteza kazi (ile sio biz ya watoto)walichofanya ni kutoa Info kwenye destination airport,ni kuwaambia namba ya ile tag inayofungwa kwenye begi maana ina maelezo yote.Juzi nilikuwa Doha nasubiri ndege ya kuja Dar,kuna vijana watatu wa TZ pia walikuwa na Sembe walikotoka walitoka salama lakini walipofika tu Doha walikuta waarabu wameshapata Info wanawasubiri.
 
Back
Top Bottom