Watanzania wengi hawajui thamani ya upendo

Watanzania wengi hawajui thamani ya upendo

Wabongo hata katika level ya familia hawana furaha kazi ni kununiana na kufokeana hata kwa mambo madogo madogo ambayo si ya kumindiana.

Watoto tunakaa nao vibaya sana. Kanuni za asili za kimalezi zinasema unapoongea na mtoto yoyote chini ya umri wa/rika la utu uzima unatakiwa kuclear akili yako isiwe na stress wala hasira kwasababu hawa ni kundi maalumu la wanajamii ambao hawaitazami dunia katika unegative wake yaani hawajui kama dunia ina macomplication ya kunyimana amani na upendo. Unatakiwa kuongea nao kwa upole, kwa sauti elekezi na ya kimamlaka ili wajue wapo chini ya usimamizi. Na usoni usiwaonyeshe sura ya jazba, hasira wala chuki.

Wanawake zetu ndio balaa kabisa hapa. Hawajui maana ya upendo. The moment ukimuonyesha upendo anaujibu na dharau au mizaha au vituko. Ukimpenda binti ukasema ngoja nianze nae kwa kumtoa out yeye hataelewa hiyo lugha atahisi unamtega ili umle na atataka akukomeshe aidha kwa kuagiza vitu vya bei, kukuomba mahitaji ambayo si ya ulazima kwake kwa wakati huo au atakuletea rafiki zake ili wakukamue ukomoke.
Ukija kuuliza why umemfanyia vile yule kijana wa watu, atakujibu ni kwasababu wanaume wanapenda kuturubuni watuchezee, hiki ndicho kimejaza akili yake kichwani. [emoji23][emoji23][emoji23] Ila ukidadisi utagundua binti hajui nini maana ya kupendwa au mapenzi ya kweli ya dhati wao wanachojua ni tuliwe ili tupewe pesa za mahitaji of which hii ukiifikiria kwa kina ni ukahaba.
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Hiki kipengele ndio my current situation
Niko sehemu hapa wamekaa watu watatu wanaongea wanacheka sana tena kwa sauti hadi kuna mtu kawafuata kawaambia waheshimu mahali tulipo
Nchi yetu nzur watanzania wacheshi tofauti na Mataifa mengine Sisi wengi wetu tuna penda kufurahi hatuja zoea kununiana mfano mmekutana na rafiki zako mliosoma shule ya msingi baada ya miaka 15 kupita kwanini msifurah na kucheka
 
Back
Top Bottom