Watanzania wengi ni wezi, hatuna uhalali wa kuihoji Serikali

Watanzania wengi ni wezi, hatuna uhalali wa kuihoji Serikali

Pia mishahara inatofautiana Sana. Kulikuwa FM mtanzania alkuwa akilipwa 1.5 m akaajirwa mhindi akawa analipwa $3000 na tsh 400000 Kama allowance. Ukimlipa hiyo hela mtz ataiibia kweli hiyo kampuni?
Nadhani Wana wasiwasi na uwezo wetu vichwani
mafisadi ya sisiemu yalikua yanalipwa hela nyingi tu ila yalikua bado yanaiba
 
kuna shirika flani linaitwa la msalaba mwekundu lilinaendeshwa na watanzania 100% lilipewa kazi ya kusimamia mambo ya afya kwenye kambi za wakimbizi likawa liko funded na mashirika ya nje UNHCR, UN, NK wao ikawa kila mwaka hesabu zao ni loss wakat mashirika mengine hayana loss, mpaka masponsor wakajitoa, shirika likaanza kua linawalipa mishahara wafanyakazi wake kwa kusua sua hadi inapita miez miwili kapa,
hapo ndo nilijua mtanzania haaminiki
Watanzania waaminifu ni wachache sana wengi ni waizi Ila hawajapata nafasi
 
Hii ni mindset iliyojengeka kwenye kizazi,kwahiyo ukitaka kuondokana na hii hali inabidi ipite miaka kama 30 ya kubanana ili watu warudi tena kwenye mstari,imefikia mahali usipokuwa mwizi unaonekana mshamba,na hii sio kwa jamii tu ya mtaani,ni mpaka kwenye familia unayotoka...
 
Tanzania sio wezi ni vibaka, maana hatujafikia international level.
 
+Ubabaishaji mwingi na maneno zaidi ya yale ya kwenye kanga.
 
True kama watawala ni wezi Kwann watawaliwa wasiwe wezi.
 
Mtawala anaiba kodi ya watawaliwa anaficha ulaya,baba anaiba kazini analeta nyumbani mama nae anamuibia baba anawalisha viporo watoto hali baba kaacha pesa kisha anatuma kwao, dada wa Kazi nae anaiba Vyakula au chochote anauza kwa jirani Ili apate ziada atume kwao.Wizi upo toka juu hadi chini.
 
Unakuta mtu akipewa kazi labda ya udereva wa Lori,anaambiwa na wenzake "Ushindwe kujenga tu! Hapo wana maanisha amuibie tajiri,

Fisadi anayeendesha Gari la kifahari anasifiwa ila muungwana anayepanda Daladala na mwenye maadili mema na kutokua na tabia ya wizi anadharaulika!

Wizi ni tabia,na solution ya hii tabia inatakiwa ianzie kwenye malezi kuanzia utotoni,kumbadili mtu mzima kuacha wizi sio kazi rahisi.
 
kwakweli huu ndio ukweli mchungu, asilimia kubwa sisi ni wezi na kila mmoja huiba kwa nafasi yake,

mimi nimefanya hata kazi kwenye mashirika ya kimataifa wenye vyeo vya juu kule ni watu wa kenya, uganda, zimbabwe na nchi zingine vyeo vya chini wamewapa watanzania wanaogopa kuwapa vyeo vya juu wataiba,

nimefanya kazi mashirika ya wakimbizi kambi za kigoma kwenye yale mashirika wanaogopa kuwapa vyeo watanzania wakiwatilia mashaka asiyeamini akaangalie mashirika yote yaliyopo kwenye kambi za wakimbizi watanzania wana nafasi gani,

Nimepata kuishi kwenye wilaya flani walikua wanajenga barabara kwa kiwango cha Rami, ndugu zangu watanzania walineemeka kwa wizi wa cement, nondo, mafuta na kokoto, wizi ulikua mkubwa sana watu walijenga mijengo kwaajili ya wizi mpaka mchina alinyoosha mikono, ulikua hata ukiitaji cement ya elfu tano unapata

maofisini kwetu ndio kabisaaa haina haja ya kuuliza, ilifika hadi hatua madereva wa halimashauri wanaenda kupiga nyoka mafuta ya serikali yananyonywa vichochoroni tubadilike tuache wizi,
hebu angalia hii video hapo chini hao Raia nao wana uhalali gani wa kuhoji serikali ilihali nao ni wezi?

Tubadilike jamani
View attachment 1918587

Kwahiyo hata wazazi wako pia ni wezi?
 
Mara ya mwisho tutakuja tuiibe na Tanzania yetu kabisa! Sijui tutaishi wapi tukishaiiba 😁
 
Sasa serikali ni nani kama sio haohao watanzania.
 
Ni kweli kabisa na hiyo inadhihirka pale wanapopandishiwa bei za vitu kama mafuta, mbolea, sukari, tozo mbalimbali kama za miamala, majengo, watanzania hutawaona wakilalamika kwa uwazi (maandamano) ili kuonesha mshikamano ya kuwa wanaumia. Kila mtu anatazama maisha yake, kama ana njia kama hizo za wizi, haoni maana ya kulalamika.
 
Ni kweli kabisa na hiyo inadhihirka pale wanapopandishiwa bei za vitu kama mafuta, mbolea, sukari, tozo mbalimbali kama za miamala, majengo, watanzania hutawaona wakilalamika kwa uwazi (maandamano) ili kuonesha mshikamano ya kuwa wanaumia. Kila mtu anatazama maisha yake, kama ana njia kama hizo za wizi, haoni maana ya kulalamika.
😀😀
 
Back
Top Bottom