#COVID19 Watengeneza chanjo bandia ya Covid-19 walivyonaswa Afrika Kusini, China

#COVID19 Watengeneza chanjo bandia ya Covid-19 walivyonaswa Afrika Kusini, China

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
1614858057098.png

Polisi nchini China na Afrika Kusini wamekamata maelfu ya dozi bandia za chanjo ya Covid-19 na kuwakamata wahusika, Polisi wa kimataifa, Interpol wameeleza.

Polisi wamewakamata watu 80 kwenye kiwanda nchini China kwa madai ya kutengeneza chanjo bandia , ambapo dozi 3,000 zilibainika tayari zikiwa zimetengenezwa katika kiwanda hicho.

Raia watatu wa China na mmoja wa Zambia walikamatwa katika ghala huko Gauteng, Afrika Kusini, ambapo chupa zilizokuwa na dozi 2,400 ziligundulika. BBC

Nadhani tusikimbilie kuchanjwa, wacha tuone kwanza sinema itavyokuwa
 
View attachment 1717151
Polisi nchini China na Afrika Kusini wamekamata maelfu ya dozi bandia za chanjo ya Covid-19 na kuwakamata wahusika, Polisi wa kimataifa, Interpol wameeleza.

Polisi wamewakamata watu 80 kwenye kiwanda nchini China kwa madai ya kutengeneza chanjo bandia , ambapo dozi 3,000 zilibainika tayari zikiwa zimetengenezwa katika kiwanda hicho.

Raia watatu wa China na mmoja wa Zambia walikamatwa katika ghala huko Gauteng, Afrika Kusini, ambapo chupa zilizokuwa na dozi 2,400 ziligundulika. BBC

Nadhani tusikimbilie kuchanjwa, wacha tuone kwanza sinema itavyokuwa
Watanzania bwana!! Yaani na wewe una amini habari hizi za kuchonga kutoka BBC - hujui lengo lao ni nini hasa kuhusu Uchina - hivi inaingia akilini kwa Taifa lolote Duniani linaweza kutumia chanjo fake bila ya kuziagizia kutoka kwenye source zinazo tambulika kimataifa, zikachunguzwa kwa umakini zinatoka viwanda gani vinavyo tambulika na kuwasiliana nao moja kwa moja?

Tuachane na kueneza uzushi husio na mantiki ukiwa na lengo la kuipiga vita China ili iwe vigumu kuingiza sokoni chanjo zao ambazo hazina changa moto na madhara makubwa unlike western mRNA based covid-19 vaccines, as I said propaganda zote hizi kuhusu China zina lengo moja kuu nalo ni: kutaka kuwaribia biashara Wachina ili chanjo zao zisihuzike Duniani.

Tukumbuke kwamba malengo ya BBC na USA main stream media ni kutaka Dunia isikie chanjo zinazo zalishwa kutoka kwenye viwanda vya madawa/chanjo vya huku Merikani na Ulaya specifically viwanda kama: Oxford/Zeneca BioteN na Johnson & Johnson basi, that is the crux of the matter here hakuna kingine zaidi ya hujuma.

Hata hayo magodown wanayo onyesha ya huko South Afrika kwamba ndiko wachina wana hifadhi chanjo, sijui za kuuzia Serikali gani huo ni usanii mtupu - jiulize swali dogo why of all places kwa nini chanjo hizo zipelekwe South Africa na Mzambia ahususike?

Mbona hawataji jina la kiwanda kinacho husika na kashfa hii inayo tia shaka mwanzo mwisho - tukumbuke kwamba katika ushindani huu wa biashara za chanjo Duniani tutakuja kusikia mengi yenye lengo la kuchafuana tu kwa kuwa biashara yenyewe ina fahida ya matrillioni ya US dollars ndio maana tutaendelea kusikia stori za kutunga tu.

Wachina wanaweza kuwa na mambo yao ya ndio sivyo lakini sio hili la chanjo - hapo tu wanawasingizia typical BBC modus operandi.
 
View attachment 1717151
Polisi nchini China na Afrika Kusini wamekamata maelfu ya dozi bandia za chanjo ya Covid-19 na kuwakamata wahusika, Polisi wa kimataifa, Interpol wameeleza.

Polisi wamewakamata watu 80 kwenye kiwanda nchini China kwa madai ya kutengeneza chanjo bandia , ambapo dozi 3,000 zilibainika tayari zikiwa zimetengenezwa katika kiwanda hicho.

Raia watatu wa China na mmoja wa Zambia walikamatwa katika ghala huko Gauteng, Afrika Kusini, ambapo chupa zilizokuwa na dozi 2,400 ziligundulika. BBC

Nadhani tusikimbilie kuchanjwa, wacha tuone kwanza sinema itavyokuwa
Kwani serikali hununua wapi bidhaa zake? Je Ni kwenye black markets?
 
Uhuni mwingine wa BBC kwa nini 'South Afrika na sio Tanzania au Congo!
Majungu kama majungu mengine kwa hisani ya watu wa Marekani!
 
Taarifa hiyo ni ya uongo huyo mzambia alikamatwa na wachina wakitengeneza viatu feki kwenye godauni lao huko mines land na watu wa viwango...SA dawa wanatengeneza wenyewe kutoka kampuni ya Johnson and Johnson kiwanda kipo Port Elizabeth na Aspen na wengine wanaojihusisha na tafiti watatoa majibu baada miezi kadhaa SA sio bongo wanaisiasa waliagiza dawa India wataalamu kutoka great skill hospital walipoipitia wakakataa kuwa haina sifa za kuua vidudu vipya vya covid...bongo wapo mawaziri walikunywa novida ya madagaska hadharani bila hata kufanyiwa tafiti...
 
Niliona video moja iliosambaa mitandaoni ikionyesha pakti la dawa ndani mna vidonge aina kama ya rangimbili, baada ya jamaa kukifungua kidonge kimoja alikuta ndani mmewekwa misumari, sisi binaadamu ni zaidi ya shetani sometimes, nilishangaa sana
 
Back
Top Bottom