Enzi hizo watoto wa hohehahe hakuna cha chai wala bibi yake uji, saa nne mapumziko tunapiga sembo hadi kengele ya kurudi class. Nguo zimeloa mijasho ya kutosha, saa sita break fupi tunarudi dimbani, saa nane na 30 dimbani, tukisharudi nyumbani tunapumzika, jioni tena tunarudi uwajani shuleni. Ilikuwa kama dozi ya malaria kutwa ×4!!
Na hakuna kuoga hadi siku tutakapokula wali ndo tunabananishwa, soka kama kawaida iwe kabla au baada ya kuoga.
Huu mchezo huwa ni wa kipekee sana aisee, vipaji vingi vinafia vijijini huko kutokana na mazingira ya bara letu, wazazi hawajui faida za michezo, ukiwa unacheza sana ni viboko tu hadi unaacha! Pia watoto tulikuwa tunacheza tu tukiwa hatujui kwamba hiyo ni ajira yenye mshahara mrefu sana huko majuu!
Akina Diego Costa, Roberto Carlos, Carlos Tevez, Salomon Kalou, Ronaldinho Gaucho, Didier Drogba..etc..etc walianzia kwenye mazingira magumu na wengi wao walikuwa vijijini ndani sana, lakini kwakuwa ni mambele, waliweza kujua faida na kutumia vyema vipaji vyao. Sisi tunabanana na jiwe letu huku maisha yanatupiga, umri umeshasonga na hata kutuliza kabumbu tu ni seleka!