Watoto wa kishua hamuwezi kuielewa hii picha

Unatumwa dukani ila ukikuta wanaume wanasukuma kabumbu unajumuika nao. Mpira ukiisha ndio unazinduka kwamba uliagizwa vitu vya muhimu na wakati huo ni saa moja usiku alafu mchafu haufai.

Utashushiwa kipigo cha mbwa mwizi lakini kesho mambo yako vilevile. Ndio siku hizi nahiuliza au hii tabia ya kuchepuka huku tukijua madhara iliimarishwa kipindi hicho?
 
[emoji23][emoji23][emoji23] kuna ile kukutanisha miguu mpira upo kati inaitwa bambi hatarr Sana, mi ni ke ila nimecheza sana hiyo
 
Hicho kinaitwa kipute.
Lazima mshtuane kua twendeni tukakipute. Hatari sana hiyo kitu.mda haurudi nyuma aisee nimekumbuka mbali Sana.
Na hapo unakuta ni darasa la 3A vs B then A ni wenye akili miili midogo mnacheza na B wasio na akili but miili mikubwa na warefu A mtakoma duh![emoji51] [emoji51] [emoji23]
 
Hapo pensi umeifungia kamba ya kiatu, mfukoni una goroli mbili, hapo mpira unauliga kwa Ndore/Dole gumba hadi kucha linangoka upaka mchanga habar kwisha.

Fainali ni kutoa njunja/Funza vidolenj
[emoji23][emoji23][emoji23] nilipiga mguu ukutani badala ya mpira maumivu yake sasa haha enzi za mwl raha sana
 
Hamnaa....madogo tu sku hz wanafatilia sana miziki na kina diamond kuliko haya mambo mujarabu kabisaa
 


Ila mkuu, goli 20? mlikuwa mnacheza na wasichana au mabonge?
 
[emoji23][emoji23][emoji23] kuna ile kukutanisha miguu mpira upo kati inaitwa bambi hatarr Sana, mi ni ke ila nimecheza sana hiyo
Bambi hyoo......yn ukipigana na mtu hyo afu yeye akapata maumivu wew usipate....bs unajiona jembe na umekomaa vilivo
 
heheheh.

kweli mkuu ilikuwa noma sana,

aliyefuma mpira ana uwezo wakuamua nani akae nje nani aingie,

inabid uwe rafiki yake tu, usimnyime visheti na ubuyu.
Hyo ndo ilikua sheria kuu......ukipata mpira mtu wa kwanza kufiria kumpa pasi ni mwenye mpira.....na penati zote anapiga yeye
 
Na hapo unakuta ni darasa la 3A vs B then A ni wenye akili miili midogo mnacheza na B wasio na akili but miili mikubwa na warefu A mtakoma duh![emoji51] [emoji51] [emoji23]
hahahahaa hii dhana hivi bado ipo huko mashuleni??
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…