Watoto wa Wasira waliojiunga CHADEMA watoa ufafanuzi juu ya uhusiano wao na Waziri Wasira


Kwani Stephen Wasira ndiye muasisi wa hilo jina (WASIRA)? Yeye kalikuta na ataliacha kama walivyoliacha mababu zake. Kuonesha hasira kuwa habari imepotoshwa ni ujinga kwani mtoto wa kaka yake kwake ni nani? Cha ajabu kabisa ni kwamba ukimuuliza Wasira habari za maendeleo atakasirika na kuanza kukutajia takwimu za Uarabuni pipa la mafuta limepanda bei, mara Iran na Iraq kuna vita hivyo uzalishaji wa mafuta umepungua hivyo watanzania tusitarajie maendeleo yoyote kwani hata nchi zilizoendelea zimeathirika. Siku zote yeye huwa ni mwenye hasira tu kama jina lake linavyoonesha (Wahasira). Hafai hata kuwa mjumbe wa nyumba kumi.
 


Mercyless labda kama unabisha kwa ajili tu ya ubishi na sio kuelewa... Katika Siasa ni nani at present anakulikana kwa jina la Wassir? Unaposema kuwa watoto wa Wassira kama kweli one in madau na mwanaharakati wa Siasa unadhani ni nani atadhaniwa anamaanishwa?

Nakubali kuwa Waziri Wassira hakupaswa kuchukizwa na hio habari sababu mwisho wa siku sio kwamba hao watoto ni wa mbali, ni watoto wa karibu na hata wanapaswa kumuita yeye baba yao. Wassira ana mapungufu yake, lakini haina maana kuwa he is the one to take all the blame katika huu mkanganyiko. Watoto wana haki ya kulaumiwa asmuchas wanahabari.
 
Sidhani kama kuna media yeyote inasema ni watoto wa Steven Wasira, wala wao hawakusema hivyo. Tukiweka siasa pembeni hoja zao ni kali sana
 
I bet you, if one of those Wassira women contests the Bunda constituency come 2015 , she will beat Stephen wassira hands down!! Wanachohitaji ni ujasiri tu wa kuthubutu!!

Huoni watamletea maswahibu baba yao mdogo ambaye ameamua kuacha mbachao kwa msala upitao?
 
hii habari nawapongeza sana Ester na Lilian kweli nawaombea kwa Mungu dumuni na baba yenu aliye wakana kwa kinywa msameheni maana hajui alitendalo hata walio watupia maneno ya kejeli muachieni Mungu na mwuwasamehe
 

Unajua siasa za leo za Tanzania ni za maji taka sana. Kinachongombaniwa wala sikioni. Halafu Mzee Wassira naye angekaa kimya na kupotezea angekuwa na busara zaidi kuliko alivyoongea. Tukumbuke watu wengi sababu ya siasa za sasa wanawekewa mitego ambayo kwa kukosa kutulia na kuwa makini, wanashindwa kuigundua na kuingia matatizoni. Damu nzito kuliko maji bwana...haikimbiwi sababu ya kubadili misimamo yangu au fikra zangu leo wala kesho.
 
Naam mabinti mmenena vema sana,karibuni tuikomboe nchi yetu kutoka kwa wakoloni weusi
 
hapa nasubiri watoto wa Nape,kabla 2015 hakuna rangi mtaacha kuona na magereza yanawangoja enyi wakoloni weusi mmeuza nchi ,shame on you!!
kumbe nape mtalaka wake alisoma na kaka zangu mlimani primary, namjua fikaaaaa mtalaka wake, ndio maana nape kadata na hatakaa awe na akili timamu, maana mtalaka wake ni full pasua kichwa! lol muwe mnamsamehe, nimejua jana si makosa yake kuwa hivi alivyo!
 

Kukaa kimya ingekuwa busara, ila kwa hali ilivo sasa kwa hizi siasa za kushindana kati ya CDM na CCM sio rahisi kuwa mzee angekaa kimya. Hasa tokana na the way wana CDM waliipa uzito hio habari kwa Dr. Slaa himself kwenda kuwakabidhi kadi...

Hapo wanatowa tu faida ya mahusiano yao... Inaelekea kuwa hawako karibu ki hivo asmuchas ni wa karibu. For kama wangekuwa karibu (kwa tamaduni zetu wa TZ) hao mabinti wangejiunga CDM kimya kimya bila hata ya kutangaza (kwani wao kutangaza ama kutotangaza unachama wao kungewapunguzia kitu kama hawana any secret agenda?- Sidhani).
 

AshaDii:
Nakubaliana na wewe hasa hapo nilipoweka red. Kama kweli mtu yoyote anapojiunga na chama fulani ni furaha kubwa kwa nini wenye majina makubwa wakijiunga inakuwa kitu cha ajabu sana? Kwani kura zao ni thamani zaidi ya moja kwa kila mtu? Siasa za kishabiki zitasababisha Tanzania isipige hatua za kimaendeleo kwa kuwa muda mwingi unapotea katika kushughulikia mambo yasiyo na tija. Waandishi wa habari jitahidini kuwa objective in educating the public please.
 
kumbe sio watoto wa wasira bana.
yes yes yes ritz, mi baba yangu hata jina lake halimo kwenye list ya majina ambayo walao yamewahi kusikika. But, i love him (rip my dear daddy), i respected and still respect him, don't have a replacement.
He was wise and very fair man, sihitaji kuitwa sijui mtoto wa nani.
Na hiyo watu wengi wako hivyo, ni fedheha kubwa kuitwa mtoto wa fisadi, mla rushwa n.k kwa hiyo usifikiri ni sifa mno kuitwa mtoto wa wasira, inategemea wasira ana value gani kwenye jamii
 
AshaDii

Nakubaliana nawe kuhusu swala la Wasira na watoto hawa kuweka mambo sawa, lakini sikubaliani nawe kuwa waandishi waliandika kishabiki swala hili bali that's what NEWS is, according to sociology of news production.

Kwetu sisi waafrika, mtoto wa baba mkubwa au baba mdogo bado ni mwanao tu hata kama tutapinga na kusema ni mtoto wa ndugu yangu, bado ni mwanao kwa tamaduniza kiafrika. Waandishi hawakukosea kusema wale ni watoto wa wasira according to African tradition and culture!

Naomba kuwakumbusha: Mkapa katika kampeni Arumeru alisema Vincent Nyerere sio mtoto wa Nyerere. Hope mnakumbuka kilichotokea baada ya hapo maana hadi ndugu za Nyerere walikuja juu na kusema kuwa Mkapa amepotoka.

Anyway huo ni mtazam wangu tu
 
Last edited by a moderator:

Ile tu kusema si watoto wangu Mzee alikuwa anatuma ujumbe ufike kokote kule alikotaka ufike. Ndio maana nasema mara nyingine ni mbinu za kuwaingiza wanasiasa kwenye king bila kujitambua.Mtoto wa mdogo au kaka yako ambaye ametangulia mbele ya haki inakuwaje sio mtoto wako? Labda hii Afrika ya leo imebadilika kabisa imeachana na mambp ya jana.
Actions speak louder than words....
Hence the saying: If you know the enemy and know yourself, you need
not fear the result of a hundred battles. If you know yourself but not the
enemy, for every victory gained you will also suffer a defeat. If you know
neither the enemy nor yourself, you will succumb in every battle.
Sun Tzu
 
Katika hii vita ya Wasira na Dr Slaa nyasi ndizo zitaumia. Sijui hadi sasa nani move hii imemjenga ni yupi amebomoka. Ila kwa taarifa hii naona Chadema imepata credit sana na Wasira amekuwa discredit sana. Kauli zake zitamuumiza sana huko baadae kama bado anataka kuendelea na siasa
 

Objectivity? Do you believe in Objecivity? Can you give me an example of being objective without having ANY element of subjectivity? Am telling you it is impossible. This term 'Objectivity' is just a strategic ritual to defend professionalism and not otherwise.

There is no way mwandishi wa habari akawa objective, anachokifanya ni ku-take position. Swala hapo ni position ipi ataichukua na kwa faida ya nani. The process of taking position bado inabaki kuwa ni something subjective
 
Kudadeki watu mna hasira, itakuweje siku so and so Kikwete akijiunga CDM?

Wanajamii hapa mtaani kwetu wanasema kuwa hawa watoto wa George Wasira wameolewa na Wachaga; nielezeni kama ni kweli; maana huenda ikawa wanalinda ndoa zao.
 
"Pia CHADEMA ni Chama maarufu sana Tanzania kwa sasa hata pengine ni maarufu kuliko CCM hivyo hakihitaji kujipatia umaarufu kwa mgongo wetu".

Very bold statement na ni vijana wachache sana wanaweza kuitoa kauli kama hii bila woga. Kama utu anapalilia apate ugali, haweza kusema haya. Big Up!
 
Wanajamii hapa mtaani kwetu wanasema kuwa hawa watoto wa George Wasira wameolewa na Wachaga; nielezeni kama ni kweli; maana huenda ikawa wanalinda ndoa zao.
Acha mawazo mgondo ya kikabila. Mbona mimi nawafahamu na najua hawajaolewa? Hata wangekuwa wameolewa na Wachagga au la ingekuwa immaterial, kwani uchagga una uhusiano gani na siasa za vyama?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…