Watoto watelekezwa na wazazi wao Morogoro. Mahusiano ya wazazi yanavyoweza kuathiri watoto

Watoto watelekezwa na wazazi wao Morogoro. Mahusiano ya wazazi yanavyoweza kuathiri watoto

NostradamusEstrademe

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2017
Posts
3,402
Reaction score
4,532
Watoto watelekezwa na wazazi wao Morogoro, DC atoa maagizo

Mkuu wa Wilaya ya Ulanga mkoani Morogoro, Ngollo Malenya, ameagiza kukamatwa kwa wazazi wawili, Thomas Ulanda na Adelyda Nakashawa kwa kuwatelekeza watoto watatu huku mmoja anayesoma kidato cha nne akiwa ndiye anayewahudumia wenzake.

Watoto hao wakazi wa Kijiji cha Gombe, mkoani Morogoro, walitelekezwa na wazazi wao wanaodaiwa kuachana na mwanamke akaolewa na mwanaume mwingine.

Mkuu huyo wa wilaya leo Alhamisi, Julai 21, 2022 ametembelea nyumbani kwa watoto hao na kuvielekeza vyombo vya dola kuwasaka wazazi hao.

Chanzo: Mwananchi

“Wazazi hao waliachana, mwanamke akaolewa na mwanaume mwingine na baba akaoa mwanamke mwingine na kuwatelekeza watoto wao kwenye kijumba ambacho muda wowote kitaanguka na kimewekewa miti kusimamisha ukuta,” amesema Malenya.

Kwa kuwa ukuta wa nyumba waliyokuwa wakiishi unakaribia kuanguka, Mwenyekiti Mtendaji wa kampuni ya Faru Graphite, John De Vries ameahidi kuwajengea nyingine na kuwasomesha.

Hata hivyo, Malenya amewapongeza majirani wa eneo hilo kwa kuwahifadhi watoto hao hasa nyakati za masika na njaa, akitaka wengine waige mfano huo.

=====

1658479817722.png

Morogoro. Mkuu wa Wilaya ya Ulanga mkoani Morogoro, Ngollo Malenya, ameagiza kukamatwa kwa wazazi wawili, Thomas Ulanda na Adelyda Nakashawa kwa kuwatelekeza watoto watatu huku mmoja anayesoma kidato cha nne akiwa ndiye anayewahudumia wenzake.

Watoto hao wakazi wa Kijiji cha Gombe, mkoani Morogoro, walitelekezwa na wazazi wao wanaodaiwa kuachana na mwanamke akaolewa na mwanaume mwingine.

Mkuu huyo wa wilaya leo Alhamisi, Julai 21, 2022 ametembelea nyumbani kwa watoto hao na kuvielekeza vyombo vya dola kuwasaka wazazi hao.

“Wazazi hao waliachana, mwanamke akaolewa na mwanaume mwingine na baba akaoa mwanamke mwingine na kuwatelekeza watoto wao kwenye kijumba ambacho muda wowote kitaanguka na kimewekewa miti kusimamisha ukuta,” amesema Malenya.

Kwa kuwa ukuta wa nyumba waliyokuwa wakiishi inakaribua kuanguka, Mwenyekiti Mtendaji wa kampuni ya Faru Graphite, John De Vries ameahidi kuwajengea nyingine na kuwasomesha.

Hata hivyo, Malenya amewapongeza majirani wa eneo hilo kwa kuwahifadhi watoto hao hasa nyakati za masika na njaa, akitaka wengine waige mfano huo.
 
Sema ww ni hatar
Inasikitisha sana, Mungu awasimamie hao watoto. Sasa naelewa kuna mtu alianzisha thread inasema “ anatamani mama yake angemuabort” . Imagine hao watoto wanajisikiaje? Wakiona watoto wenzao wakiwa na wazazi wao? Wakiugua inakuwaje? Inafikirisha sana
 
Hawa wazazi wote hawana akili na utu pamoja na hao walioana nao!Watoto wamekosa nini?Je wao walikua kwa kunyanyaswa,kwa kweli inaumiza sana.Kuna watu wanakesha kuomba Mungu awape watoto,hawa wanachezea zawadi toka kwa Mungu.Bora mkuu wa wilaya kayaona wapate adhabu.wajinga kabisa.
 
Huu uzi nimeutoa kwa makusudi maalum.Siku moja watoto wangu wakiwa wadogo walinitoa machozi japo sikuonyesha kulia wazi wazi.Walikuwa wanacheza na wqtoto wa mama mmoja alikuwa anakujaga kwangu kuomba kazi za ukibarua endapo atabahatisha.Wale watoto baba yao alimtelekeza mama yao kisa eti amemzaliwa mtoto mwenye kifafa hata hivyo yule baba pamoja na kumkimbia mkewe hatimaye baadae alikuja kufariki.

Yule mama alikuwa anaishi maisha ya tabu mno kiasi kwamba wakati mwingine nilikuwa naamua anisaidie kazi ndogo ndogo tu ajisikie naye anapata hela kwa jasho lake.

Sasa watoto wa yule mama wakawa wanacheza na wananga mtoto wangu wa kiume ambaye wakati huo alikuwa mdogo wa miaka 3 alimuuliza mtoto wa yule mama hivi kwanini nyie hamna baba kama sisi.Hilo swali lilinikata maini yangu niliingiwa na uchungu mkubwa mno maaana watoto hawajui wasemalo.

Hadi leo hii yule mama nikiwa ni kitu kidogo namsaidia ndio chanzo cha mimi kutoa story hiyo nilivoiona kwenye gazeti.Tukio hili lilitokea mwaka 1998
 
Huu uzi nimeutoa kwa makusudi maalum.Siku moja watoto wangu wakiwa wadogo walinitoa machozi japo sikuonyesha kulia wazi wazi.Walikuwa wanacheza na wqtoto wa mama mmoja alikuwa anakujaga kwangu kuomba kazi za ukibarua endapo atabahatisha.Wale watoto baba yao alimtelekeza mama yao kisa eti amemzaliwa mtoto mwenye kifafa hata hivyo yule baba pamoja na kumkimbia mkewe hatimaye baadae alikuja kufariki.
Yule mama alikuwa anaishi maisha ya tabu mno kiasi kwamba wakati mwingine nilikuwa naamua anisaidie kazi ndogo ndogo tu ajisikie naye anapata hela kwa jasho lake.
Sasa watoto wa yule mama wakawa wanacheza na wananga mtoto wangu wa kiume ambaye wakati huo alikuwa mdogo wa miaka 3 alimuuliza mtoto wa yule mama hivi kwanini nyie hamna baba kama sisi.Hilo swali lilinikata maini yangu niliingiwa na uchungu mkubwa mno maaana watoto hawajui wasemalo.
Hadi leo hii yule mama nikiwa ni kitu kidogo namsaidia ndio chanzo cha mimi kutoa story hiyo nilivoiona kwenye gazeti.Tukio hili lilitokea mwaka 1998
Sawa mkuu,Ubarikiwe sana na Mungu kwq msaada huo.
 
Back
Top Bottom