Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Albert Msando, amethibitisha kutokea kwa ajali leo asubuhi, saa 12, katika eneo la Michungwani, Kata ya Segera, Wilaya ya Handeni. Ajali hiyo, iliyohusisha lori na Coaster, imesababisha vifo vya watu 7 na kujeruhi wengine 10.
Akizungumza kuhusu tukio hilo, Mkuu wa Wilaya amesema: "Naendelea kuwasisitiza sana madereva kuwa makini na kuchukua tahadhari. Ajali hii sababu ni UZEMBE WA DEREVA."
Kutokana na uzembe unaojirudia, Msando amesema: "Nimemuelekeza OCD atakayekiuka sheria ya barabarani eneo la Handeni tutampandisha Mahakamani na kuomba adhabu ya kifungo."
Ameongeza kuwa wale wanaopiga simu kuomba msaada kwa madereva wao wakikiuka sheria wasitegemee msaada wowote. "Hakuna msaada zaidi ya kukaa lock up kwa mujibu wa sheria na kupandishwa kizimbani," alisema.
Msando pia ametoa onyo kali kwa madereva: "Ukifika kijiji cha Manga, Wilaya ya Handeni, ewe dereva usipofuata sheria za usalama barabarani usitulaumu. Ajali nyingi zinaepukika."
Kwa upande wa abiria, Mkuu wa Wilaya amewahimiza kuchukua hatua wanapogundua dereva anaendesha kiholela. "Acheni kukaa kimya wakati dereva anaendesha hovyo aidha shuka, utarejeshewa nauli yako na toa taarifa kwa Jeshi la Polisi tudhibiti huu uzembe,"
Akizungumza kuhusu tukio hilo, Mkuu wa Wilaya amesema: "Naendelea kuwasisitiza sana madereva kuwa makini na kuchukua tahadhari. Ajali hii sababu ni UZEMBE WA DEREVA."
Kutokana na uzembe unaojirudia, Msando amesema: "Nimemuelekeza OCD atakayekiuka sheria ya barabarani eneo la Handeni tutampandisha Mahakamani na kuomba adhabu ya kifungo."
Ameongeza kuwa wale wanaopiga simu kuomba msaada kwa madereva wao wakikiuka sheria wasitegemee msaada wowote. "Hakuna msaada zaidi ya kukaa lock up kwa mujibu wa sheria na kupandishwa kizimbani," alisema.
Msando pia ametoa onyo kali kwa madereva: "Ukifika kijiji cha Manga, Wilaya ya Handeni, ewe dereva usipofuata sheria za usalama barabarani usitulaumu. Ajali nyingi zinaepukika."
Kwa upande wa abiria, Mkuu wa Wilaya amewahimiza kuchukua hatua wanapogundua dereva anaendesha kiholela. "Acheni kukaa kimya wakati dereva anaendesha hovyo aidha shuka, utarejeshewa nauli yako na toa taarifa kwa Jeshi la Polisi tudhibiti huu uzembe,"