Watu ambao asili yenu ni mjini, hamkujui kijjini kwenu, mnalichukuliaje hili swala?

Watu ambao asili yenu ni mjini, hamkujui kijjini kwenu, mnalichukuliaje hili swala?

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
1640173828280.png


Tanzania tuna makabila zaidi ya 120 na yote yana asili yake yalipotoka na mkataa kwao ni mtumwa.

Kumekuwa na ongezeko la watu siku hizi ambao wanazaliwa mjini na vijijini kwao hawakujui kabisa, mtu unaweza kumuuliza wewe ni mhaya, mnyakyusa, n.k wa wapi, anakwambia yeye ni mngoni, msukuma, n.k wa karakoo.

Je kwa watu wa mjini wanalichukuliaje swala la mjini kuwa asili yao bila kujua mizizi yao viijini?

Mfano mimi ni mtu naeishi mkoa flani wa nyanda za juu kusini na nimezaliwa huku lakini asili yangu ni mkoa wa Mara (mkoa huu unaongozea kwa makabila mengi hawapo wakuria pekee), siijui kikamilifu lugha lakini tangu zamani nikiwa mtoto tulikuwa tunaenda na mzee kila mwaka, hali hii menifanya nijuane kwa karibu na ndugu zangu, kujua mila na tamaduni kadhaa, ngoma, matambiko (kila kabila lina matambiko) n.k.

Kila mtu ana asili yake na mkoa wake.....na hao ndio wanaosumbua kutaja kabila zao. Hakuna mngoni, mkurya,mchaga,muhaya wa Arusha,Mbeya,Dar au Mwanza.

Mjenge utamadunu wa kurudi vijijni kwenu na mjuane na ndugu wa ukoo wako. Usijivunie mahali pasipo asili yako.

Muhimu: Hii inawahusu wale ambao makabila yao hayana sana changamoto ya kutupiana makombora ( guided missles ), hawa tunaweza kuwaelewa kwa kiasi
 
Kumekuwa na ongezeko la watu siku hizi ambao wanazaliwa mjini, asili zao wanazozijua ni mjini bila kuwa na watu wanaowajua au kwenda kuwasalimia sehemu zao za asili

Je kwa watu wa mjini wanalichukuliaje swala la mjini kuwa asili yao

Mfano mimi ni mtu naeishi mkoa flani wa nyanda za juu kusini na nimezaliwa huku lakini asili yangu ni mkoa wa Mara, sijui sana lugha yetu lakini huwa ninaenda mara kwa mara maana tayari nina ndugu zangu tuliojuana tangu utotoni kipindi napelekwa huko na mzee wangu (Mara ndio mkoa unaoongoza kwa makabila mengi, Wakurya sio kabila pekee).
Kwani lazima wote tuwe na vijiji.. !! Kama mimi vizazi vyangunwote ni borntown.

Msikariri mambo ya vijiji kwamba kila mtu katoka huko misenyi sijui chato mara muleba. Wengine born here here, hata babu yangu hajui huko mnapopaita kijijini.

So, mrelax kama wewe unakijijini kwenu nenda kapajue. And life goes on
 
Endeleeni kukaa huko tutakuwa tunawaona kwenye taarifa ya habari
 
Nkipata hela ntaenda muheza kuwasalimia..sijui kama wananijua. Na hivi nlivofanana na marehemu mamangu pale kijijini wasije wakatimua mbio bure.
 
Nkipata hela ntaenda muheza kuwasalimia..sijui kama wananijua.
Na hivi nlivofanana na marehemu mamangu pale kijijini wasije wakatimua mbio bure.
Mkuu usirudi kichwa kichwa huko kijijini, huenda ulikuwa hupelekwi kwa sababu za msingi, ukienda wakakujua inaweza kuleta shida kidogo hasa ukizingatia huko muhezi wanasifika sana kwa teknolojia ya gizani
 
Asili hubadilika, huko unakoita kijijini kwenu miaka mingi iliyopita mababu zako hawakuwa wakiishi hapo
 
Kila mtu ana asili yake na mkoa wake.....na hao ndio wanaosumbua kutaja kabila zao. Hakuna mngoni, mkurya,mchaga,muhaya wa Arusha,Mbeya,Dar au Mwanza.

Waambieni wazazi wenu wawapeleke vijijni kwenu mpajue na mjuane na ndugu wa ukoo wako. Usijivunie mahali pasipo asili yako.
 
Kwani lazima wote tuwe na vijiji.. !! Kama mimi vizazi vyangunwote ni borntown.

Msikariri mambo ya vijiji kwamba kila mtu katoka huko misenyi sijui chato mara muleba. Wengine born here here, hata babu yangu hajui huko mnapopaita kijijini.

So, mrelax kama wewe unakijijini kwenu nenda kapajue. And life goes on
Ingetakiwa umuulize babu yako vizuri asili yenu ni wapi? Inawezekana kabisa nyie ni mabaki ya watumwa au wapagazi wa Waarabu mliotelekezwa huko mjini. Tanzania tuna makabila zaidi ya 120 na yoooteee yana asili yake yalipotoka. Kumbuka mkataa kwao ni mtumwa.
 
Ingetakiwa umuulize babu yako vizuri asili yenu ni wapi? Inawezekana kabisa nyie ni mabaki ya watumwa au wapagazi wa Waarabu mliotelekezwa huko mjini. Tanzania tuna makabila zaidi ya 120 na yoooteee yana asili yake yalipotoka. Kumbuka mkataa kwao ni mtumwa.
Watu wakishajenga mijumba hapa mjini tayari wanasahau kwao kabisa, watoto hadi wanakuwa wakubwa hawaijui asili yao hata chembe.
 
Dunia ni kubwa sana aisee. Tembea uone watu wanavoishi utajifunza mengi kuliko kurudi kijijini sehem ambayo hawakujui wala huwajui eti kisa babu yako ndo alipotokea. Mzungu katembea dunia yote katawala karibu kila nchi na hata kabila lake halijui. Saiv wanatengeneza marocket wanataka kwenda sayari nyingine maana dunia washaiona yote ila sisi bado tunataka watoto warudi kijijini wakajifunze makabila yao
 
Kwakweli binafsi nachukulia kawaida tu,
As long as napata mahitaji muhimu mengine mbwembwe za ela tu,
 
Hayo mambo ya makabila yamepitwa na wakati kiasi fulani, Ukiangalia kwa undani zaidi utagundua hata ukoo wako siyo huwo unaotumika kwa sababu wazazi hawatoki kwenye ukoo mmoja.
 
Dunia ni kubwa sana aisee. Tembea uone watu wanavoishi utajifunza mengi kuliko kurudi kijijini sehem ambayo hawakujui wala huwajui eti kisa babu yako ndo alipotokea. Mzungu katembea dunia yote katawala karibu kila nchi na hata kabila lake halijui. Saiv wanatengeneza marocket wanataka kwenda sayari nyingine maana dunia washaiona yote ila sisi bado tunataka watoto warudi kijijini wakajifunze makabila yao
Acha uongo....wazungu wanajua asili yao vzr tu .

New York hasa blooklyn watu wanaishi kulingana na wanapotoka
 
Wazaramu utawapeleka wapi wakati Chanika ni sehemu ya mji na kadri unavyopanuka Kisarawe nayo itakuwa ni sehemu ya mji
 
Back
Top Bottom