Watu Muhimu katika Historia ya Nchi yetu

Watu Muhimu katika Historia ya Nchi yetu

What is wrong with a short? Kwa ile weather ya Dar Es Salaam I can be comfortable wearing a short or a lob (kanzu)!!
 
Mama Ntilie:

Huu uzoefu wako hauko ukamili. Wakati TAA inabadilika na kuwa TANU 1954, wimbi la kudai uhuru tayari lilikuwepo barani Africa. Na haitawezekana kwa watanzania kuanza kudai uhuru mwaka 1954, hii itakuwa ni kutotendea haki struggle za wananchi zilizokuwepo kabla.

Phenomena unayoiona hapa, imetokea karibu katika nchi zote za kiafrika. Wananchi walianzisha vyama, lakini baadaye waliwapa nafasi vijana waliotoka masomoni Ulaya.

Kwa mfano Kwame Nkrumah alikuwa yupo uingereza hana mpango wowote. Lakini kwa sababu alikuwa amesoma watu walimrudisha Ghana na kumpa madaraka.
Nkrumah hakusoma Uingereza. Alisoma Marekani katika chuo kikuu cha Lincoln jimboni Pennyslvania. Alipokuwa Marekani alikutana na wana harakati wengi tu kutoka Black diaspora, including Guyana, Jamaica, Trinidad and Tobago, na wote hawa wakizungumzia haki ya watu weusi kujitawala. Kwa huyo wakati Nkrumah anarudi kwao alikuwa ameshaamua kuingia katika siasa.
Kamuzu Banda, Jomo Kenyatta na wengine wengi tu walikuta watu wameweka misingi mizuri ya vyama vya kudai uhuru. Na hawa ndio walioandikwa kwenye historia.
Zakumi,
Nkrumah hakusoma Uingereza. Alisoma Marekani katika chuo kikuu cha Lincoln jimboni Pennyslvania. Alipokuwa Marekani alikutana na wana harakati wengi tu kutoka Black diaspora, including Guyana, Jamaica, Trinidad and Tobago, na wote hawa wakizungumzia haki ya watu weusi kujitawala. Kwa hiyo wakati Nkrumah anarudi kwao alikuwa ameshaamua kuingia katika siasa.
 
Nia ya Mhe. Mkandara ni njema kabisa lakini ndugu yetu Junius naona umeenda nje ya mstari. Unamlaumu Baba wa Taifa eti alijali umaarufu wake tu wengine aaa! You are being very unfair to him! Did you expect him kusimama jukwaani na kutoa orodha ya wale alioshirikiana nao katika kupigania Uhuru? Ama ulitaka pamoja na makujumu mazito ya kuliongoza taifa basi aketi chini awaandikie historia. Kazi hiyo ni yenu wasomi na hata wale wasio wasomi kuandika historia ya nchi hii kwa kuwafuata wanasiasa na wananchi ambao bado wako hai wanaojua kilichotokea miaka hiyo. Hata hivyo Mwalimu did justice to his fellow wapiganaji kwa sababu amewahi mara kadhaa kuwataja watu kama akina Mzee Tambaza, Sykes, Rupia na wengine wengi tu katika hotuba zake wakati akisimulia juu ya harakati za kupigania Uhuru. And for your information baada ya kustaafu wapo Watanzania waliokuwa wakionana naye na na kupata simulizi na mengi yaliyotokea katika historia ya nchi hii. I assure you, he wasn't all that mean kama unavyotaka kutuaminisha Junius!

Kwa uzoefu wangu, naona wengi wanaomkandia Mwalimu na kumshutumu kwa namna moja ama nyingine ni wale ambao kama si wao basi 'ancestors' wao waliguswa na 'fimbo' ya Mwalimu katika mambo kadha wa kadha.

kwanza you need to get your facts right...Nyerere alikuja Dar mwaka 1952 akiwa kama mwalimu wa shule ya St. Francis College, Pugu.Alikuwa hajui mtu na alikuwa ni jamaa ambaye yupo yupo tuuuu

Nyerere alikuwa na Mwapachu huko Tabora katika mwaka 1945, na Makerere College na baadaye nchini Uingereza wakichukua masomo ya juu...nadhani walikuwa Edinburgh Inawezekana kwamba Nyerere kufuatia harakati za chama cha TAA, alisikia kuhusu Abdulwahid Sykes kupitia kwa Mwapachu alipokuwa bado yuko Uingereza. Mwapachu na Nyerere walikuwa wanafunzi katika Makerere College wakati ambapo Kasella Bantu na Nyerere walifundisha katika shule moja, St. Mary's School kule Tabora. Na hii haina ubishi ukitaka kujua mengi zaidi soma kitabu kilichoandikwa na Mwandishi maarufu wa historia ya Tanganyika, BW. MOHAMED SAID katika kitabu chake cha The Life and Times of Abdulwahiid Sykes. sasa hili la kutaka kutuambia tunapindisha Historia umelitoa wapi? Hakuna anayemkandia Nyerere ila ukweli unaelezwa kama ulivyo na si kwa kusoma tuu lakini inabidi ukae chini na wazee wa mji ambao walikuwepo enzi hizo ndio utaelewa watu wanazungumiza nini

Of course inawezekana hukuambiwa lakini unaambiwa kati ya ma RADICALS hakuna aliyekuwa kama KASELLA Bantu mwanachama wa TAA mwenye msimamo usiotetereka wa kupinga ukoloni alijiuzulu kufundisha na alikuja Dar es Salaam kujiunga na Tanganyika Broadcasting Corporation (TBC)....


Na unaambiwa kwenye hotuba ya kuaga yenye kuhuzunisha ambayo Nyerere aliitoa tarehe 1985 kwa Wazee wa Dar es Salaam, kikundi cha Waislamu pekee wakazi wa mjini waliomuunga mkono tangu kuundwa kwa TANU, Nyerere aliwaambia wasikilizaji wake kwamba ilikuwa Kasella Bantu aliyemtambulisha yeye Nyerere kwa Abdulwahid.


Hii ilikuwa ni moja ya zile nyakati adimu sana ambazo Nyerere alizungumza hadharani kuhusu siku zake za mwanzo na ilikuwa mara ya kwanza kutaja jina la Abdulwahid hadharani akimhusisha na historia yake mwenyewe na ile ya chama.


sasa mnataka kubisha nini?
 
kwanza you need to get your facts right...Nyerere alikuja Dar mwaka 1952 akiwa kama mwalimu wa shule ya St. Francis College, Pugu.Alikuwa hajui mtu na alikuwa ni jamaa ambaye yupo yupo tuuuu

Nyerere alikuwa na Mwapachu huko Tabora katika mwaka 1945, na Makerere College na baadaye nchini Uingereza wakichukua masomo ya juu...nadhani walikuwa Edinburgh Inawezekana kwamba Nyerere kufuatia harakati za chama cha TAA, alisikia kuhusu Abdulwahid Sykes kupitia kwa Mwapachu alipokuwa bado yuko Uingereza. Mwapachu na Nyerere walikuwa wanafunzi katika Makerere College wakati ambapo Kasella Bantu na Nyerere walifundisha katika shule moja, St. Mary's School kule Tabora. Na hii haina ubishi ukitaka kujua mengi zaidi soma kitabu kilichoandikwa na Mwandishi maarufu wa historia ya Tanganyika, BW. MOHAMED SAID katika kitabu chake cha The Life and Times of Abdulwahiid Sykes. sasa hili la kutaka kutuambia tunapindisha Historia umelitoa wapi? Hakuna anayemkandia Nyerere ila ukweli unaelezwa kama ulivyo na si kwa kusoma tuu lakini inabidi ukae chini na wazee wa mji ambao walikuwepo enzi hizo ndio utaelewa watu wanazungumiza nini

Of course inawezekana hukuambiwa lakini unaambiwa kati ya ma RADICALS hakuna aliyekuwa kama KASELLA Bantu mwanachama wa TAA mwenye msimamo usiotetereka wa kupinga ukoloni alijiuzulu kufundisha na alikuja Dar es Salaam kujiunga na Tanganyika Broadcasting Corporation (TBC)....


Na unaambiwa kwenye hotuba ya kuaga yenye kuhuzunisha ambayo Nyerere aliitoa tarehe 1985 kwa Wazee wa Dar es Salaam, kikundi cha Waislamu pekee wakazi wa mjini waliomuunga mkono tangu kuundwa kwa TANU, Nyerere aliwaambia wasikilizaji wake kwamba ilikuwa Kasella Bantu aliyemtambulisha yeye Nyerere kwa Abdulwahid.


Hii ilikuwa ni moja ya zile nyakati adimu sana ambazo Nyerere alizungumza hadharani kuhusu siku zake za mwanzo na ilikuwa mara ya kwanza kutaja jina la Abdulwahid hadharani akimhusisha na historia yake mwenyewe na ile ya chama.


sasa mnataka kubisha nini?
And the point is?
 
Rugambwa.gif

Kardinali Laurian Rugambwa kardinali wa kwanza afrika.....
 
Waliopigania uhuru ni Waswahili bwana,kwa maana ya wasilamu na wakristo maskini.Mwazna alikuwapo Huseni Majaliwa,Bukoba alkuwapo Ali Migeyo,Kahama Ali Saidi Maswanya,Paulo Bomani,Mwananyolo na Gerevas waliokubali mseto na kuitwa wapumbavu.Lakini wale waliokuwa wamejikita katika Misheni na kuwa karibu sana na wakoloni walikuja kurukia tu kama Lyanyantika Masha na wengineo walikuja kupewa kazi na nyerere.
Kule darisalam ambako ndiko kulikuwako na vuguvugu kubwa ni wale wazee wa kipwani walikuwa wanampelekesha mkoloni.Nyererr yeye alilpelewka na kapputula yake na kasela bantu hadi kwa kina sykes na kutambulishwa huko.[/QUOTE]


Maneno yako ni mazima kabisa

Infact Nyerere alikuwa mgeni kabisa mjini Dar es Salaam na kama ilivyokuwa mazoea, Kasella Bantu alimchukua Nyerere kwa Abdulwahid kukamilisha kufahamiana na kukutana na watu maarufu wa pale mjini. Mbali na Dossa Aziz aliyekutana na Nyerere kwa muda mfupi katika mkutano mkuu wa TAA , ilikuwa ni Mid 40's, Kasella Bantu mwenyewe na Denis Phombeah, hakuna mtu mwingine katika makao makuu ya TAA aliyewahi kusikia habari za Nyerere...infact Nyerer was a NO BODY

Wakati huo, Abdulwahid na mdogo wake Ally, walikuwa na mawasiliano na International Union of Socialist Youth iliyokuwa Austria na mipango ya kupeleka mjumbe Umoja wa Mataifa, NewYork ilikuwa mbioni. Nyerere na baaadaye Mwapachu walirudi toka Uingereza wakiwa wameshawishika na mawazo ya Fabian Society, kikundi cha wasomi cha mrengo wa kushoto cha Labour Party ya Uingereza. (Btw mimi ni member wa Fabian Society)

Ukikaa na wakee kama akina Mzee Katungunya pale nje ya msikiti wa Manyema watakuwambia kuwa Abdulwahid, Nyerere, Ally, Dossa Aziz, Mhando, Rupia, Dunstan Omari na wengine walizoea kukutana kila Jumapili kwa ajili ya baraza ama nyumbani kwa Dossa Aziz mtaa wa Congo au nyumbani kwa Abdulwahid mtaa wa Stanley. Sehemu hizi ndizo ambazo wazalendo hawa walikuwa wakikutana kujadili mustakabali wa Tanganyika....ambayo siku hizi mnaiita Tanzania ya MAFISADI
 
Zakumi,
Nkrumah hakusoma Uingereza. Alisoma Marekani katika chuo kikuu cha Lincoln jimboni Pennyslvania. Alipokuwa Marekani alikutana na wana harakati wengi tu kutoka Black diaspora, including Guyana, Jamaica, Trinidad and Tobago, na wote hawa wakizungumzia haki ya watu weusi kujitawala. Kwa hiyo wakati Nkrumah anarudi kwao alikuwa ameshaamua kuingia katika siasa.


Jasusi:

Ni kweli Nkrumah alisoma Marekani, lakini baadaye alikwenda kuishi Uingereza. Huko alitaka asome London School of Economics lakini baadaye aliingiza kwenye Pan Africanism. Na huko alikuwa mpiga porojo wa siasa kwenye migahawa.

Alirudi Ghana baada ya kupata mwaliko wa Joseph B. Danquah ambaye alikuwa ni kiongozi wa United Gold Coast Convention (UGCC) hili awe katibu mkuu wao.

Hivyo aliporudi Ghana alitokea Uingereza. Kwa reference zaidi soma mikutano ya Pan Africanism iliyofanyika uingereza the rest is commentary.
 
To be fair ilivyoonekana Mwalimu Nyerere alimuona Abdulwahid Sykes kuwa ni mtu mwenye akili sana, asiye na choyo na mtu wa kupendeka. Kwa upande mwaingine Abdulwahid alimwona Nyerere kuwa ni mtu aliyeelimika sana na mwenye ustadi wa kupendeza wa kujadiliana.

kilichokuja kumkumba Nyerer baada ya uhuru anakijua Mwenyezi Mungu tuu
 
To be fair ilivyoonekana Mwalimu Nyerere alimuona Abdulwahid Sykes kuwa ni mtu mwenye akili sana, asiye na choyo na mtu wa kupendeka. Kwa upande mwaingine Abdulwahid alimwona Nyerere kuwa ni mtu aliyeelimika sana na mwenye ustadi wa kupendeza wa kujadiliana.

kilichokuja kumkumba Nyerer baada ya uhuru anakijua Mwenyezi Mungu tuu
kilichokuja kumkumba Nyerer baada ya uhuru anakijua Mwenyezi Mungu tuu

Please go on kipi?
 
kilichokuja kumkumba Nyerer baada ya uhuru anakijua Mwenyezi Mungu tuu

Please go on kipi?

hatuwezi kuenda mbele bila kujua huko nyuma ilikuwaje..unajua historia ukitaka kuenjoy basi inabidi uwe na subra...kwanza ni muhimu kujua yaliyotokea huko nyuma au unasemje ?
 
To be fair ilivyoonekana Mwalimu Nyerere alimuona Abdulwahid Sykes kuwa ni mtu mwenye akili sana, asiye na choyo na mtu wa kupendeka. Kwa upande mwaingine Abdulwahid alimwona Nyerere kuwa ni mtu aliyeelimika sana na mwenye ustadi wa kupendeza wa kujadiliana.

kilichokuja kumkumba Nyerer baada ya uhuru anakijua Mwenyezi Mungu tuu

Unajiita Atheist na baadaye unasema anakijua Mwenyezi Mungu. Hapo umeondoka kwenye u-Atheist.

Anyway. Baada ya uhuru viongozi wengi wa Africa walikuwa kwenye ideaological battles na kusahau walichopigania uhuru. Na matokeo yake vyama vya kupigania uhuru vikawa vimejaa makada wa kisiasa na ambao ndio walioandika historia za nchi.
 
Kwa kuanza tuu ni muhimu kujua kuwa Nyerere hakuwa na uzoefu wa ujuzi wowote wa kisiasa uliostahiki kutajwa wakati huo wa kulinganisha na ule wa Abdulwahid.


Chama cha African Association huko Tabora kiliposhiriki katika ule mgomo wa jumla in the late 40's Nyerere hakujihusisha na chama hiki cha wafanyakazi ingawa alikuwa katibu wa chama

sasa je hii ilikuwa ni calculated risk au nini? sijui labda nitamuuliza Mohammed Said anifafanulie zaidi maana alipata bahati ya kuongea na wazee ambao walimpa insight zaidi

Anyway, kutokana na sababu hiyo kuheshimiana kulitokea baina ya Abdulwahid na Nyerere, Kila Jumapili Nyerere alikuwa akisafiri toka Pugu hadi Dar es Salaam kuhudhuria mikutano hii isiyokuwa ya kawaida na baada ya mikutano ama Dossa Aziz au Dunstan Omar alimrudisha Nyerere kwa gari hadi Pugu....so hivi ndivyo ndivyo Nyerere alivyokuja kuingia ndani ya duru za ndani zaidi za TAA katika makao makuu na hatimaye akajapendekezwa kugombea cheo cha juu kabisa cha uongozi wa cham in 1953.
 
Unajiita Atheist na baadaye unasema anakijua Mwenyezi Mungu. Hapo umeondoka kwenye u-Atheist.

Anyway. Baada ya uhuru viongozi wengi wa Africa walikuwa kwenye ideaological battles na kusahau walichopigania uhuru. Na matokeo yake vyama vya kupigania uhuru vikawa vimejaa makada wa kisiasa na ambao ndio walioandika historia za nchi.

issue ilipo inhand in historia ya nchi yetu unless una lako jambo

au imekuudhi Abdulwahid Sykes na Kasela Bantu kumwonyesha Nyerere njia?
 
Hotuba mnayoizungumzia nimeipata toka kwa jamaa wa Tanzania Daima.

*******************************************************************


Katika kumuenzi Baba wa Taifa, leo tunawachapishia moja ya hotiba zake zilizowakuna wengi. Hii ni sehemu ya hotuba ya Julius Nyerere alipokutana na Baraza la Wazee wa Dar es Salaam, kuagana nao kabla hajastaafu urais. Ilichapishwa kwa mara ya kwanza katika gazeti la Radi, Toleo Na. 2 la mwaka 1986 lililokuwa likimilikiwa na Ndimara Tegambwage. Gazeti hili lilifutwa na serikali kwa madai kuwa lilikuwa halitoki kwa muda mrefu – Mhariri Tanzania Daima.

MIMI nimeanza siasa na wazee wa Dar es Salaam; na wazee wa Tanzania. Nimeanza nao mapema sana; mapema kweli. Nilirudi kutoka masomoni, Uingereza Oktoba 1952 – miaka 33 nyuma. Wakati huo nikiwa kijana mdogo wa miaka thelathini na kidogo hivi.

Niliporudi nikakubaliana na wamisionari hapo Pugu (sekondari), nifundishe shuleni kwao. Lakini nikiwa shuleni – Chuo Kikuu – nilijua. Niliishaamua kwamba maisha yangu yatakuwa ya siasa. Niliamua hivyo: Nitafundisha kwa muda wa miaka mitatu, nione hali inavyokwenda na kuzoeana na wenzangu kabla ya kuanza maisha ya siasa.

Niliporejea nchini hapo Oktoba, nikaenda Butiama. Januari nikarudi Dar es Salaam. Nikaanza kazi. Nikataka kujua habari za African Association. Mzee Mwangosi anakumbuka. Yeye ndiye aliniambia habari za African Association. Aliisha niambia habari hizo tangu nikiwa Makerere – Chuo Kikuu – nikiwa mwanafunzi.

Pale, mimi na wanafunzi wenzangu tulikuwa tumeanzisha chama kinachoitwa Tanganyika African Welfare Association (TAWA) cha wanafunzi wa Tanganyika; mimi nikiwa katibu wao. Hapa tukaona mambo yanakwenda vizuri kidogo.

Tukaona kwanini TAWA iwe ya wanafunzi peke yao na siyo Tanganyika nzima. Kwa hiyo nikawaandikia baadhi ya watu Tanganyika. Nikasema, jamani ee, tumeanzisha chama, kwanini msianzishe huko matawi ya chama hicho?

Ndugu Mwangosi akapata barua hiyo. Alikuwa miongoni mwa waliopata barua hiyo. Akaniandikia – nikiwa Makerere – akasema: Wewe kwanini unataka kuanzisha chama kipya? Kipo chama. Kipo Chama cha TAA (Tanganyika African Association).

Kwa hiyo la maana si kuanzisha matawi, maana chama kipo na matawi yameenea; la maana ni kwamba hicho chama chenu mfute, na muanzishe tawi la Tanganyika African Association.

KUVUNJWA KWA TAA

Hivyo ndivyo tulivyofanya. Kwa hiyo mimi nikawa katibu wa katawi ka TAA hapo Makerere. Niliporudi Tabora na kuanza kufundisha pale St. Mary's (sasa inaitwa Sekondari ya Milambo), nikachaguliwa katibu wa TAA wa jimbo ambalo makao yake makuu yalikuwa Tabora. Ulipofanyika mkutano wa TAA mjini Dar es Salaam, nilihudhuria nikiwa mjumbe kutoka Tabora.

Kwa hiyo nilikuwa naijua Tanganyika African Association. Nilipokuwa ninaondoka kwenda Ulaya kusoma, nilikuwa nimeishaonja shughuli za TAA. Sasa niliporudi, baada ya kukaa Pugu siku chache, nikaja mjini Dar es Salaam. Nikauliza nani wanaongoza TAA? Nikaambiwa kuna jamaa mmoja anaitwa Abdul Sykes. Sasa ni marehemu. Abdul ndiye alikuwa katibu wakati huo.

Nilipelekwa na Kasela Bantu - ambaye naye aliteleza-teleza na hatunaye hapa (kwenye mkutano). Kasela Bantu alikuwa mwalimu mwenzangu. Tulifundisha pamoja Milambo. Nilipokuja Dar es Salaam, nikakuta anafanya kazi Radio (Tanganyika Broadcasting Corporation). Ni Kasela Bantu aliyenipeleka kwa Sykes.

Wakati huo mambo yalikuwa yanasinzia kidogo. Kwa muda mfupi mwaka ule, tukafufua-fufua, hasa kutoka Januari. Kufika Aprili, TAA ikafufuka. Tukafanya mkutano hapo Anautouglou. Kwenye mkutano huu wakanichagua kuwa rais wao – wa TAA.

Ninasema yote haya kwa shukrani kwa wazee. Jamaa hawa walikuwa watu wazima wa Dar es Salaam, na mimi kijana mdogo Mzanaki, na Kiswahili changu si kizuri sana – cha matatizo.

Nimekuja, natoka Ulaya, tena masomoni. Muda mfupi tu jamaa hawa wakaniamini haraka sana – katika muda wa miezi mitatu. Wakanichagua Rais wa TAA. Hapo ndipo nilianza shughuli mpya ya kuandika katiba ya TAA na kuipa madhumuni hasa ya shabaha ya kuleta uhuru.

Baada ya miezi 13, hapo 1954, tukaanzisha TANU. Jina hili lilipendekezwa na kina Abdul Sykes. Walikuwa wamelifikiria tangu zamani, walipokuwa askari vitani huko Burma (Vita vya Pili).

WAZEE NA MSIMAMO

Miezi minne baada ya kuanza kazi Pugu nikawa ninakuja Dar es Salaam, kwa mguu; kila Jumamosi. Baadaye wazee wakanipa baiskeli nikawa ninakuja mjini kukutana na wenzangu; kufanya mikutano.

Hivyo ndivyo tulivyofanya. Wazee wakaniamini upesi sana. Tukawa na uhusiano mkubwa sana. Wadogo wenzangu wengine walikuwa Abdul Sykes, Abass Sykes (mdogo wake), Dosa Aziz – waliokuwa wengi ni wazee.

Katika kuhutubia mikutano yangu, nilikuwa nikisema: Wazee na ndugu zangu! Wazee hasa ndio walikuwa na mikutano ya awali ya TAA na TANU. Walikuwa na msimamo wa hali ya juu kabisa! Hawakuyumba hata kidogo! Vijana walikuwa na mashaka. Wengine walikuwa na vikazi vyao, waliogopa kuvipoteza.

Nalo jambo lenyewe ni la hatari – la kuzungumzia uhuru! Unaweza ukakosa kazi; na wapo waliopoteza kazi; wengine wakaacha kazi. Kina Rashid (Kawawa) waliona watoke kwenye shughuli hizo tuje tuungane katika chama.

Wazee wa Dar es Salaam, na baadaye wa nchi nzima, wakatuunga mkono, na kila nilipokwenda, watu wa kwanza walionielewa, walikuwa wazee.

Nilikwenda Songea mwaka 1955 mara baada ya kujiuzulu. Huko wazee walinipokea na kunielewa. Nilianza safari za kuitembelea Tanganyika nzima. Nilikwenda Mbeya. Mkutano wangu niliufanya na wazee; kikundi kidogo cha wazee, ndani ya nyumba ya mtu.

Kwa mkutano huu wa Mbeya, wazee wakauliza: Unatafuta nini? Nikawaambia natafuta uhuru. Wale wazee, kwa sababu ya vita vya Maji Maji, na wanakumbuka, kabisa, wakaona mimi ninatafuta jambo la hatari. Tulifanya mkutano wa makini kweli. Wakauliza: Wewe unawezaje kuleta uhuru? Wewe una njia gani kudai uhuru na usitiwe kitanzi na Waingereza?

WAINGEREZA WAONGO
Tulielezana. Nikawaambia ninyi wazee, Waingereza wanawadanganya, Waingereza wametumwa na ule Umoja wa Mataifa uliokufa (League of Nations), waje kuishika Tanganyika kwa muda tu; watusaidie, na wakati tutakapokuwa tayari, watuachie tukajitawale.

Waingereza wanafanya ujanja; hawasemi. Vita vimekwisha (vya Pili) na Umoja wa Mataifa mwingine – mpya (United Nations Organisation – UNO) umewakabidhi Tanganyika kwa shabaha ileile. Sisi siyo koloni lao. Wamepewa dhamana tu.

Kwa hiyo nikawaambia wazee, hakuna haja ya kumwaga damu. Tuwaseme tu! Tuwashitaki kwa waliowaleta hapa kwamba hawafanyi kazi yao; wamesahau kabisa!

Wazee wakauliza: Eh, inawezekana? Nikasema inawezekana. Kazi yetu ya kwanza ilikuwa kuwaambia watu kwamba uwezekano wa kujitawala upo. Hilo lilikuwa la kwanza. Wazee walijua maana ya kujitawala. Walitamani kujitawala, lakini hawakujua waanzie wapi.

Vijana hawakuwa na habari kwamba kujitawala kunawezekana. Kwa hiyo kwa wazee sikuwa na matatizo. Wao hawakuwa na kazi; hawakumwogopa Mwingereza. Hawakuogopa kufukuzwa kazi. Baadhi walikuwa wafanyabiashara.


Mzee John Rupia (marehemu) alikuwa mfanyabiashara na kaidi (mkaidi) kidogo. Aliwahi kutishwa na kunyang'anywa leseni yake ya biashara. Akaambiwa akiendelea kushirikiana na kijana mwenda wazimu (Julius Nyerere), atanyang'anywa leseni moja kwa moja. Rupia aliwajibu: Potelea mbali!

Nasema yote haya ikiwa njia ya kutoa shukrani kwa wazee na imani yao kwa vijana wakati huo.

Imani hujenga imani. Na mambo haya makubwa ya nchi, kama hayana baraka za wazee hayaendi. Magumu sana. Wanasema ngoma ya watoto haikeshi! Mimi nilipata baraka za wazee tangu zamani. Tangu awali kabisa.

TWINING AMEKWISHA

Siku moja, Dosa akanifuata Magomeni (Dar es Salaam). Akasema: Leo wazee wanakutaka. Wapi? Kwa Mzee Jumbe Tambaza. Wanakutaka usiku. Nikasema haya, nitakuja. Nikaenda. Nikakuta wazee wameshakaa; wameniita kijana wao kuniombea dua. Mimi Mkristo, wao Waislamu watupu. Wakaniombea dua za ubani. Tukamaliza.

Tulipomaliza wakasema kuna dua pia za wazee wao. Basi wakanitoa nje. Tukatoka. Zilipomalizika zilikuwa za Kurani; sasa zikaja dua za wazee – za jadi.

Walikuwa na beberu la mbuzi. Wamechimba shimo. Wakaniambia simama. Nikasimama. Beberu akachinjwa, huku anaambiwa, "Twining (Twainingi) umekwisha!" (Edward Twining alikuwa gavana wakati huo). Ndipo nikaambiwa: Tambuka! Nikavuka lile shimo. Hapo nikaambiwa na wazee: Basi nenda zako; tangu leo Twining amekwisha!

Sasa mimi Mkristo; hao Waislamu. Na mimi mkorofi-korofi katika mambo haya (ya kutambika). Lakini tulikuwa tunaelewana na wazee wangu hao. Kwa hiyo nilitambuka pale na kuambiwa: Nenda nyumbani salama. Twining hawezi tena!

Wazee wangu wengine wanakumbuka tulikuwa tunakwenda Bagamoyo. Kwenye makaburi kule! Tunapiga dua huko kwenye makaburi na wazee wangu.

Baadhi yetu mtakumbuka safari moja jamaa wa Kenya, hawa kina Tom Mboya (marehemu) walishitakiwa. Tukasema tuwasaidie. Tuwasaidie vipi? Tukasema tufunge. Tukaomba nchi nzima kufunga siku hiyo. Tufunge! Tukafunga. Hakuna kula. Na siku ya kufunga tulikuwa na mkutano Bagamoyo. Tukaenda huko. Tukafanya mkutano hadi saa 12 jioni.

Baada ya mkutano tukaenda nyumbani kwa mzee Mohammed Ramia (marehemu). Hapa ndipo tulikuwa tumefikia. Mimi nikamuuliza mzee: Sheikh, una Aspro? Akajibu: Kwa nini unataka Aspro? Nikajibu kuwa kichwa kinaniuma kwelikweli. Akasema subiri.

Tulisubiri hadi saa ya kufuturu. Tukafuturu vizuri. Mzee Ramia akaniuliza: Bado unataka Aspro? Nikajibu kichwa sasa hakiumi. Kumbe ilikuwa njaa.

Nawaelezeni haya kwa sababu huko tulikotoka, tulishikamana sana. Tulishirikiana sana na wazee.
 
hatuwezi kuenda mbele bila kujua huko nyuma ilikuwaje..unajua historia ukitaka kuenjoy basi inabidi uwe na subra...kwanza ni muhimu kujua yaliyotokea huko nyuma au unasemje ?
Hizo point zote ulizoongea, are you trying to discredit that Nyerere ni katika "Watu Muhimu ktk Historia ya Nchi yetu?".

Umeongelea kuwa Nyerere admired Sykes and this other guy admired Nyerere, sasa sielewi, unataka kusema Nyerere ali-exploit wema wa hawa watu wa - Pwani; au siyo kuwa hawa watu - Wa-Pwani (Dalisalamu) walikuwa na expectation kubwa mno baada ya Uhuru. Ulivyoongea hapo juu inaonekana kuwa Nyerere alifanya dhuluma kubwa sana kwa baadhi ya watu wa Dalialamu na itikadi zao hasa wale WaIslamu, huoni kuwa, inawezekna kuwa Nyie pamoja na wewe mlikuwa minority on those people who were in struggle for the liberation of the motherland.

How can Mr. Nyerere alone triumph to such higher stage and have such powers without the majority at the core?
 
Balozi Paul Bomani alikuwa architect muhimu wa vyama vya ushirika kanda ya ziwa, vyama vilivyoleta matumaini na mwanga wa ukombozi kwa wakulima wa kiafrika kutoka unyonywaji wa wakoloni kwa kupitia vibaraka wao wa kihindi waliokuwa na monopoly ya vinu vya kuchambua pamba (ginneries) kuanzia sehemu za Nasa, Kwimba, Musoma na pande zote za mashariki na kusini mwa ziwa Victoria Tanzania.
 
issue ilipo inhand in historia ya nchi yetu unless una lako jambo

au imekuudhi Abdulwahid Sykes na Kasela Bantu kumwonyesha Nyerere njia?

Mimi historia ya Tanzania sijuhi vizuri lakini naichambua kwa vigezo vyangu.

Historia ya nchi nyingi za kiafrika zimepikwa na kuwakuza watu pale isivyo. Nyerere amechukua uongozi wa TAA akiwa na miaka 31 au 32. Ndio kwanza amerudi na hajajijenga. Na zaidi ya hapo alikuwa na familia changa.

Ukichukua umri aliyokuwa nayo na mazingira ya wakati utaona kuwa historia ya Tanzania nayo imepikwa.

Ukienda upande wa Kaskazini ya Tanzania, watu wa mwanzo kuanzisha chama cha ushirika barani Africa, utaona kuwa Tanzania haikusubiri mpaka TANU ianze ili wadai uhuru wao.

Vilevile mapambano ya kudai uhuru Tanganyika yanakuwa Exaggerated. Mwingereza hakuwa na faida yoyote ya kukaa Tanganyika.
 
Bangusule,
Naona umemaliza somo. Ngoja sasa waje akina Junius watuambie jinsi Nyerere alivyoua babu zake.
 
Back
Top Bottom