Watu wa town mnatuumiza sana sie wa mikoani na kauli zenu " aise huu mkoa bado sanaaa yaan hamna totoz kabisa"

Umesahau na hii kauli...Binti mzuri afu unaishi Mkoani Aisee unatutesa sana wanaume wa Dar.
 
hahaha......aiseeee
 
Sasa sisi dada zao tumekukosea nn mdogo wangu
Kuna wadada wapo huko kipindi bado mdogo wakaja na mazawad masimu makubwa surual wamesuka manywele marefu wakasema wanafanya kazi Posta Red onion hotel

Sasa mwaka jana nikatimba huko nikaenda bar moja inaitwa Fair way kama unaenda Bunju katikati ya Tegeta na Boko eeeh nikakuta ni wahudumu wa Bar

Cha ajabu watoto wao wamewaacha mkoani ikabid waniambie nitunze siri nikawaambia nataka nije mnapokaa lahaulaaaaaa

Chumba kimoja wanakaa watu 9 Ila siku wakirudi mkoani huwa tunakoma watoto weupeee Demiss miye mpaka nataman nipake Mkorogo wa Maimartha wa Jesse nifanane nao.


Na yale manywele wanayarusha kama wakorea nywele mpaka gutako zinafika hapo Demiss nimesuka twende kilioni.

Wadada wa dar mna dhambi kama kaka zenu

Hawa ndo wanatuharibu sisi wa mkoani
 
Wamekusikia mdogo wangu haiwezi jirudia tena
Thubutu kuna huyo nilienda Dar akawa hapatikani siku nipo kwenye kimbinyiko nimeshafika kibaigwa ananipigia simu eti alikabwa na mateja cha kushangaa namba yangu katoa wapi

Mfyuuuuu
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Thubutu kuna huyo nilienda Dar akawa hapatikani siku nipo kwenye kimbinyiko nimeshafika kibaigwa ananipigia simu eti alikabwa na mateja cha kushangaa namba yangu katoa wapi

Mfyuuuuu
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Demiss hurumia mbavu zangu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…