Watu waliomkufuru Mungu wakafariki dunia

Umemsahau baba wa elimubya anga.. Stephen hawkings.. Japo yeye hajafa ila kapooza mwili mzima
 
Ni sahihi ulivyo andika. Ni kweli Mungu hawezi kufanya visasi na binadamu hata siku moja, wala siyo mafundisho ya kikristo na Biblia.
 
Mungu bwana, Anampambanisha Shetani na mwanadamu a.k.a Kiumbe dhaifu ilihali anaujua uwezo wa shetani kiutendaji ni sawa na yeye tu.......
Shetani ni kiumbe dhaifu kupita mwanadamu.
Mwanadamu umeumbwa kwa mfano wa Mungu mwenyewe.
Ukapewa utawale vitu vyoote vilivyo angani, ardhini na chini ya ardhi.
Huyo Shetani anakuonea wivu jinsi Mungu alivyokupendelea mamlaka na uwezo.
Ukimkataa Shetani anakukimbia, ukimkaribisha anakuja kukuchanganya akili yako.
Usijidharau ndugu
Wewe ni Bora kuliko Shetani na unalindwa na Malaika kila sekunde
Jitambue ukuu wako.
 
mungu wa yakobo na isaka is a fool and a murderous crazy pagan god.
Kumbe unaamini kuwa kuna Mungu.
Tutajie wewe basi huyo Mungu wa kweli.
Usinitajie Lusifer kwani yeye anakiri kuwa kaumbwa na Mungu na bado anasikitika kwa kuondolewa katika cheo chake alichopewa na Mungu.
Nimemsikia mwenyewe Lusifer akimwita Mungu "The Creater of Universe"
Najua hata wewe unanafasi ya kuonana naye, mwulize atakujibu hivyohivyo.
Uliko lala sisi tumeamkia huko.
Tutajie Mungu ambaye si wa kipagani, tusikie.
 
Hili somo ni kubwa sana linapita uwezo wako unaotumia sasa.
Kwa mleta mada nadhani you are wrong....Mungu ana upendo kweli hawezi kuwafanya watu wake hivyo......think
Umemgeuka mwenzio unamwambia yuko wrong
 
Ni sahihi ulivyo andika. Ni kweli Mungu hawezi kufanya visasi na binadamu hata siku moja, wala siyo mafundisho ya kikristo na Biblia.
Mungu alifanya kisasi na mwanadamu

1 aliwaua wana wa israel jangwani

2 alishindwa kumsamehe adamu na mkewe bustanini

3. Alishindwa kuwasamehe watu enzi za nuhu na kuwaangamiza kwa gharika

4. Alishindwa kuwasamehe watu wa sodoma na gomolah na mke wa Ruthu kumgeuza nguzo ya chumvi

Japokuwa anadai yeye ni mwingi wa rehemu anasamehe dhambi zote na kufuru zote za wanadamu

Lakini ni mungu mwenye kisasi asiye na huruma kwa watu wake
Anasema mimi ni mungu mwenye wivu nawapatiliza mbali wana maovu wa. baba zao kizazi cha kwanza cha pili cha tatu na cha nne cha wanichukiao

maana yake baba alifanya dhambi mtoto ataadhibiwa na mjukuu ataadhibiwa na kitukuu kitaadhiwa ni hadi kizazi cha nne je hicho si kisasi?



 
Hamna kisasi hapo.

Adamu alishaambiwa,
"ukila tunda la katikati hakika utakufa"
Kipindi cha ghalika Mungu alishawaonya watu kuwa anachukizwa na atawaua wakosaji.
Sasa nani mwenye makosa hapo ?

Sodoma na Gomola wala usiwatetee
Huko Saudi Arabia mashoga wanachinjwa hadi leo, hii tabia haivumiliki, Mungu alishawaonya wakaasi.

Kuhusu kuangamia kwa Waisraeli jangwani, kumbuka Mungu alishawapa Amri kumi.
Mojawapo inasema "usichonge sanamu na kuiabudu"
Wao wakachonga sanamu na kuziabudu Musa alipokaa mlimani siku arobaini.
Watu elfu tatu wakaangamia.

Wengi sijui kwanini mnashindwa kuelewa ngoja niwape mfano.

Anayetengeneza gari anakupa maelezo kuwa,
Usiweke maji kwenye tenki la petroli.
La sivyo utaliua gari nk.
Mbona wenye magari mnazingatia hii tabia ?
Je ukikosea kuweka maji na ukaliuwa gari lako utamlaumu mtengeneza magari ?

Mungu amekuumba na amekupa masharti ili wewe uyafuate ili uishi vizuri.
Na amekuambia ukivunja masharti haya (amri zake) hakika utakufa.
Mungu anapo amua kumwua mwanadamu hatendi dhambi hata akikuwa kwa maji, moto, ugonjwa, ajali nk.
Kwani alipokuumba mlikubaliana uishi mda gani ? na ufe kwa kitu gani ?

Ukiona unaishi ujue unaishi sio kwa matakwa yako bali Mungu ndo anaye amua uishi hadi lini na akiamua anakuchukua mda wowote bila hiari yako na huwezi kumlaumu.

Mungu ni mwenye rehema kwasababu mtu ukimkosea amekupa muda wa kutubu.

Ukikaidi kutubu anakuangamiza kwa jinsi anavyoona yeye inafaa, sasa unamlaumuje hapo, si amesha kuambia mapema.

Wewe kama unaona unapenda kutenda dhambi na hutaki kutubu kama alivyokuagiza, basi mwombe Mungu akuuwe ili uiepuke adhabu ambayo yeye ataiamua juu yako baadae
Na kwasababu umeshazaliwa inakupasa utubu kwanza halafu umwombe akuchukue usijeanguka kwenye dhambi tena.
Ni kama chumba cha mtihani, ukishaingia basi ni lazima upate matokeo ya Zero au Pass.
Mwanadamu usinge wekewa sheria na adhabu na Mungu hii dunia isinge kalika.
(Angalia madai ya Mashoga)

Sio Mungu pekee hata wewe unasheria na adhabu ulizoziweka hapo nyumbani kwako.
Serikari nayo ina sheria na adhabu.
Mungu ndiye mwanzilishi wa sheria na adhabu.

Hebu ishi kwa kufuata sheria za Mungu. ndipo utakapoziona rehema na upendo wake, tena utafurahia maisha bila ghalama yoyote, ni raha kwa kwenda mbele milele daima.

Umesikia ?
Mungu amesema
hivi
"Asema BWANA ; lakini mtu huyu ndiye nitakaye mwangalia, mtu aliye myonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu"
Isaya 66 : 2

Hata hapo mtaani kwako kama hufuati sheria ndogondogo za mtaa, na ukaamua kuwaibia majirani zako, hakika watakuchoma moto na kukuuwa kabisa.
Sijui utamlaumu nani.

Fata sheria, hata huyo Lusifer anayekudanganya kuwa Mungu ni mwonevu, ana sheria zake, na ukimkosea anakuua vilevile. tatizo la Lusifer ni kuwa hana jambo la manufaa kwa wafuasi wake, ni kiumbe dhaifu kilicholaaniwa na Mungu.
Kama unataka haki ndugu yangu.
Inabidi ujitegemee.
Yaani ujiumbe mwenyewe,
Ujipe uhai na chakula,
Ujitengenezee dunia yako,
Ukae peke yako bila kiumbe kingine chochote,
Uwe mwenye nguvu za kujilinda na nguvu nyingine yoyote itakayotaka kukufisha.

Kama huwezi hayo fata Amri za aliye kuumba maana ndiye mwenye nguvu na wajibu wa kukulinda na kuamua uishi hadi lini

Pole kwa mfadhaiko.
 
Umekalili kwelikweli
 
Na abdalla kigoda,celine kombani,samwel sitta, aliongea nini?!?!!!!
 
Kwa comment hii sidhani Kama upo hai, na Kama upo hai I think Uko vibaya Sana kiafya
 
Umekalili kwelikweli
Sijakariri huu ndio ukweli.
Binadamu anayejiona ni dhaifu kupita Shetani, hajitambui.
Angalia dunia inavyopendeza kwa kila unachokiona, kazi nzuri ya mwanadamu.
Huyo shetani sijamwona akitengeneza hata sindano ya kuchomea papasi.
Siku moja mtu alipandisha mapepo, akawa anaomba aletewe bia ya Safari ili anywe, akaomba na ubani, kuku nk.
Nikacheka sana
Nikamwuliza "ivi wewe huo ujini wako woote unashindwa kutengeneza bia, au kwenda kununua bia bar"
Sioni cha mana chenye akili kilichofanywa na Shetani au huyo Lucifer, zaidi ya kujifichaficha na kuwahadaa binadamu wasio jitambua.
Mi sisogelewi na Shetani yeyote.
Mimi ni bora sana kilinganisha na hivyo viumbe vichafu,
Kama unajiona kuwa ni dhaifu kuliko Shetani ni tatizo lako la kuto kujitambua.

Jitambue mkuu uko juu sana,
Shetani mwenyewe anawashanga watu wanaomtetemekea.
Ndo maana ukienda kwa mgangamchawi kuomba msaada anakuambia,
Nenda kamwue mwanao au mzazi wako au ndugu wa karibu au Arbino ili ukamatwe na ufungwe au kunyongwa
Kwani anakuona ni mpumbavu.
Mungu amekupa kilakitu halafu wewe unaenda kuomba msaada kwa kitu dhaifu.
Anakupa masherti hayo ili mteseke wote
Ha...ha...wacha hayo mawazo
Wewe ni bora kupita Lucifer.



Sent from my TECNO-N8 using JamiiForums mobile app
 
Mimi nimemkufuru Mungu tangu Jamiiforums inaitwa Jamboforums.

Na sijafa mpaka leo.

Na kama kufa wote tutakufa.

Hakuna Mungu. Hakuna Shetani.

Mungu na Shetani ni wewe mwenyewe.

Mimi nimesomesha daktari Tanzania. Anatibu watu. Nimesaidia kuumba udaktari wa huyu mtu anayetibu watu. Ndio uungu wangu huo.

Ninapofanya mabaya, huo ndio ushetani wangu.

Acheni kutishiana ujinga hapa.
 
Samani Bosi wangu.
Kwani wewe ulitaka ufe ?

Ukiona hivyo ujue Mungu anakupa muda ili utubu.
Na nadhani huo muda wa kutubu utakujia tu siku moja.

Mungu halazimishwa kufanya jambo lolote na mtu yeyote.

Yeye ana muda wake wa kufanya mambo yake ambao sisi binadamu hatuujui.

Kama siku ya kuzaliwa kwetu,
tulijiona tu tumezaliwa wala hatukujua tunazaliwa lini na kwanini.

Kama kweli uliwahi kumkufuru Mungu basi nakushauri utubu kama hutaki basi ni maamuzi yako tunayaheshimu.







Sent from my TECNO-N8 using JamiiForums mobile app
 
Ukiondoa woga wa kumuogopa Mungu asiyeonekana wala kuthibitika wengi tuliopewa tangu tunazaliwa, ukiangalia mambo kwa kufikiri kwa kina, kutumia mantiki na uchunguzi usioshinikizwa na jamii, bali unaotafuta ukweli, utapata jibu moja.

Huyu Mungu hayupo.

Ni jitihada za watu kutafuta ukweli wakijikwaa jikwaa katika usiku wa giza nene la ujinga, jitihada za kutawalana kwa kutishana na ujinga wa kuogopa kusema hatujui tusivyovijuana kutaka kuvipa jibu rahisi la Mungu.
 
Peleka ujinga wako huko.
Mjinga sana ww, tena mvivu wa kufikiri.
Sijakutukana, bali ni sifa yako
 
aiseee inaogofya Mwenyezi Mungu atusamehe na utupe hekima katika maneno na mawazo yetu ,atupe kuchagua yapi ya kunena yapi ya kuwaza.
Acha kuwa na akili fupi!!
Je anaekufa na miaka 2 huyu nae tusemeje?
Embu jaribu kuipa kazi akili yako kufikiri kuliko kukariri
 
ww ni mjinga, bado akili za kupandikizwa zinakupeleka. Hakuna Mungu.
Mungu ni Uongo takatifu uliotengenezwa na wahuni wa kale
Wewe amini hakuna Mungu kwa sababu zako binafsi. Pia, waache wanao amini kuna Mungu kwa sababu zao binafsi! Mjinga anasema hakuna Mungu ingawa creation Inaonesha wazi kwamba kuna Muumba aliye sababisha. Pia mjinga anasema kuna Muumba sababu ya uwepo wa ushahidi wakutosha. Kwahiyo, wewe ni mjinga pasipo amini uwepo wa Mungu na wengine wajinga kwa kuamini uwepo wa Mungu. Wacha Mungu ataamue siku ikifika, labda by then utakuwa umeshaoza kubakia mifupa kaburi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…