Watu wanajua kutunza aisee

Watu wanajua kutunza aisee

Kwa wale wa Malori nadhani watakua wanaijua, nishawahi kuiona 113 (Scania) namba D kwa kweli nilichochoka
Namba D zipo nyingi tu . Haya magari kuna watu wanayabahatisha huko ireland na Uk kwenye backyards na mashamba wananunua na kuyaaleta nchini .likija hapa linapata usajili mpya , naamimi utayaona hadi namba E
Hesabu zake kununua ni ngumu sana though maana. Ni very expensive hadi kofi unakuta linafika hadi 90+ mill
 
Kuiyona scania namba d sio tatizo huwenda ndio limenunuliwa muda huu ,changamoto ni hiyo gari hapo juu kwa maaana wakati usajili namba A unamalizika hiyo gari ilikuwa haijatengenezwa au tuseme bongo hazikuwepo swali ameipata wapi , namm nilishakutana nalo hilo gari sinzaa jamaa akaniambia umeona hiyo hapo kuna namna
Hiyo gari iliwekwa sokoni kwa mara ya kwanza 2003! Namba A tanzania zilianza mwaka gani?

Nakumbuka mpaka 2005 bado usajili ulikuwa namba A!

Kama mtu aliinunua around hiyo miaka, inashindikana nini hiyo gari kuwa no. A?
 
IST ni ya mwaka gani na namba A zimemalizika mwaka gani?

Kuna mtu anayo mpya sana ni namba A!
Huyo mwizi. IST zimeanzia namba B. Hata kuna boya mmoja alikamatwaga kirahisi sana kwa kuweka namba A kwenye IST..na kweli kumbe gari ilikua ya wizi
 
Hiyo gari iliwekwa sokoni kwa mara ya kwanza 2003! Namba A tanzania zilianza mwaka gani?

Nakumbuka mpaka 2005 bado usajili ulikuwa namba A!

Kama mtu aliinunua around hiyo miaka, inashindikana nini hiyo gari kuwa no. A?
Hakuna anaebisha kuwa namba A zipo,ila condition ya gari namba A hata itunzwe vipi haiwezi kuwa kama imetoka Japan. Zipo nyingi namba A model hiyo ila sio mpya hivi
 
Huyo mwizi. IST zimeanzia namba B. Hata kuna boya mmoja alikamatwaga kirahisi sana kwa kuweka namba A kwenye IST..na kweli kumbe gari ilikua ya wizi
Ist gari ya 2002 inashindikana nini kuwa namba A mkuu?

Mtu anamiliki viwanda akaibe Ist hahaha, na hiyo Ist yake ni safi na nzima kuliko hizi namba D nyingi tu..
 
kuna watu wana magari kumi ndani, kwa mwezi anaweza hata asitumie hiyo gari, alafu unakuta ni mstaafu hana pilika pilika tena za kila siku kutoka.
Hujaelewa lengo la uzi.
Ni kuwa hakuna harrier ilikuwepo wakati namba A zinamalizika
 
Kuiyona scania namba d sio tatizo huwenda ndio limenunuliwa muda huu ,changamoto ni hiyo gari hapo juu kwa maaana wakati usajili namba A unamalizika hiyo gari ilikuwa haijatengenezwa au tuseme bongo hazikuwepo swali ameipata wapi , namm nilishakutana nalo hilo gari sinzaa jamaa akaniambia umeona hiyo hapo kuna namna
Sidhani kama ni shida sana.
ASL inaweza kuwa namba iliyotoka mwaka 2007 na hizi gari zimeanza kutengenezwa kabla ya 2007. Hivyo inawezekana ilinunuliwa ikiwa 'brand new' wakati huo.
 
Hakuna Harrier tako la nyani namba A ingekuwa old model sawa hii tako la nyani ni ya juzi tu hapa
 
Halafu Mgeni Mjini humo weye!!... shaabash!! ...kuna watu mjini hawajulikani wewe!! .. weye fanya yako uone Moto!...ndo utajua kuwa hujui!....tena sometimes, wanaendesha style ya

Hiace mbovu, Beatles la zamani/jipya kaa nayo mbali hayo! ukijipendekeza Dakika sifuri tu kibao kinakugeukia! Ukiingia kwenye kumi na nane zao! wanakuingiza mule, una kalizwa kwenye vibench! vya Mantilie humo humo ndani! ndo utachoka!!.....

Halafu Mamtu Yenyewe,hayanaga haraka yale! Mibaunsa ime vaa- vika wash!! na Mikofia ya Rastfari, Mara Miwani myeusi tii!! na Miradio call....yaani utachoka! kosa la kawaida utazunguka nao weeee!! ......Mpaka uyambe kifukuto!...lkn kosa kubwa unaenda fichwa!

Ndo utajua wasio julikana ni nani.....!! Maborn town wanayajuaga kwa, mfano unaweza kumuona Dereva wako wa daladala/Tax Ghafla anakuwa km ana mapepe hivi!! haendi mbele kwa speed, au

anaondoa gari ghafla, wkt macho yako kwenye site Morror nakuangalia!! angalia km mwizi hivi hapo jua amekutana na hawa.....wanajuana sana .... kwa....
1.P/Number!

2.Mwendo!

3.Uchakavu!

4.Upya wake na number haviendani!

5.Waliomo! ni majitu! au yako hapo mbele yanachukuliwa soon! ukisogea zaidi pembeni sambamba nao, utaona kakimurimuri kekunduu au kijaniii kanawaka na kuzima usawa wa domo! utasikia yakiongea maneno km ''chui mwitu, mara kobe, nyau, nyoka nk!

6.kaa!! kaa! yao ilivo mle ndani na nje!! ni km wamemuinamia dereva ivi..sasa km wakitoka, ile toka yao sasa Mweee!

7.Tyre za Gari yao husika utazijiua kwa kuwaachia nafasi waende mbele kidogo, utazimulika km ni usiku...... na style ya tembea yao barabarani!

8.Hawanaga haraka!! na wkt mwingine wana haraka mnoo!

9. Magumashi!! magumashi!! wanaweza kuanzisha mbio ghafla! ukashangaa!

10.Usiku sasa heee!! Wana guji-tochi Maalumu haguonekanagi gukikumulika hugo tokea kwa nyuma lazima mbele huoni! sasa kuna mawili wana haraka zao wanataka kukupita au wana mashaka na wewe!.....hasa km unakimbia sana usiku Mnene!

ukiona ivo cha kufanya punguza mwendo, km ukizidisha wanajua aaahaa!! ndo wale wale!! wanaotujua! ..... unalo! mpaka uvunguni!...cha msingi wewe hapo, ni makosa sana kulisogelea hilo gari km ivo ulivo hapo nyuma yake!!

au labda wewe na dereva wako ni wa kuja! hajui maisha ya barabarani town! ndo maana unashangaa ivo!....wakuja kila kitu ni kushangaa tutuuuuuuu! wkt sie tumeyazoea hayooo!
 
Hakuna anaebisha kuwa namba A zipo,ila condition ya gari namba A hata itunzwe vipi haiwezi kuwa kama imetoka Japan. Zipo nyingi namba A model hiyo ila sio mpya hivi
Usikariri maisha kijana.

Kuna watu wana gari 4 ndani na bado wanaendeshwa na gari za ofisi.

Kuna gari kwa mwaka mzima haitembei hata km 5000. Na inaweza toka nje ya geti hata mara 10 hazifiki.

Nina gari namba C, imesimama kuliko hata namba D zilizotoka mwaka huu. Na hata km 90,000 hainafikisha. Kwa mwezi inaweza ikatoka mara 1 au 2 tu.

Gari ikitunzwa inatunzika vizuri tu.
 
6.kaa!! kaa! yao ilivo mle ndani na nje!! ni km wamemuinamia dereva ivi..sasa km wakitoka, ile toka yao sasa Mweee!

Mkuu umeandika mashairi mengi sana...

Naomba born town aliyeelewa comment ya huyu Binti anieleweshe mimi wakuja...
 
hapo ndio umekosea, wakati namba mpya zinatoka harrier tako la nyani zilikuwepo.
Tatizo la watu wengi wanadhani wao wanapoanza kuiona gari barabarani, au aina fulani ya gari zinapoanza kufurika, basi ndio zimetoka mwaka huo! Ki uhalisia asilimia 90 au zaidi ya magari yote yaliyopo Tanzania ni ya kati ya mwaka 2000 mpaka 2005!

Chukulia mfano gari kama Dualis au Rumion zilivyojaa sasa hivi mtu atadhani ni gari za juzi, kumbe ni gari za 2007 huko! Sasa ikitokea mtu aliinunua mwaka 2008 unaweza kukuta sasaivi anayo na ni namba A au B ukaanza kusema ni ya TISS kumbe wala. Harrier new model zenyewe ni gari za 2003.
 
Hiyo katumia kadi ya zamani old model, kazi za wahuni inatumia usajili wa zamani.

Gari sio number kwanza
 
Back
Top Bottom