Watu wanaoongea sana (micharuko) huwa hawana siri, chukua tahadhari

Watu wanaoongea sana (micharuko) huwa hawana siri, chukua tahadhari

OMOYOGWANE

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2016
Posts
4,701
Reaction score
11,920
Kwa utafiti wangu usio rasmi, kuna wale watu wanaongea sana, ukiwakuta kwenye kikundi cha watu au popote pale wao mara nyingi hupenda kudominate mijadala, mara nyingi waongeapo huongea kwa sauti ya juu sana, hujifanya wanajua kila kitu, pia hawa watu hupenda kuzoeana haraka na kila mtu ndani ya muda mfupi, mara nyingi huwa hawana aibu pia ni wachangamfu sana.

Hawa watu huwa hawana siri, pia huwa wanapenda kuhamisha maneno kutoka point A kwenda B kisha kuyarudisha point A.

Hawa watu wapo kila mahali kuanzia mashuleni, vyuoni, kwenye nyumba za kupanga, nyumba za ibada, .mtaani, nyumbani kwako n.k

Wanaweza kuwa ndugu zako, wadogo zako, kaka zako, mke wako n.k

Kama unajambo hutaki lijulikane kwa watu wengi basi epuka kuwashirikisha hawa watu.

Kuwa makini, chukua tahadhari.
Nawasilisha.​
 
Kwa utafiti wangu usio rasmi, kuna wale watu wanaongea sana, ukiwakuta kwenye kikundi cha watu au popote pale wao mara nyingi hupenda kudominate mijadala...​
Ni kweli, ingawa wengine waongeaji sana lakini wanajitahidi kuchagua maneno.
Nadhani mada yako inazungumzia makundi ya Extroverts.

Lakini kumbuka siri ina muda wake wa kuishi, baada ya hapo huwa siyo siri tena. Wakati mwingine mtunza siri huitoa mwenyewe[emoji23]
 
Naweza kusema nami ni miongoni mwa hao watu.

Sio watu wote wa design hiyo ni wambeambea Mkuu.

Sema namna wengi wao walivyo wachangamfu na wenye wepesi wa kuzoeana na watu wapya na kutengeneza marafiki hutafsirika kuwa huwa wanatoa siri za watu.

Kimsingi watu wa hivyo ni wazuri huchangamsha hadhara,wepesi kutengeneza connection na wengi wao wana marafiki wengi.

Kuongea kuna faida ila tuu kusizidi sana Mkuu, Kumzoea mtu mkimya ni tabu sana. Sometimes unashindwa ata kumtabiria mtu mkimya kujua anawaza nini ni ngumu sana.

Nafikiri mtu muongeaji huwa na afya ya akili maana huuchangamsha ubongo mara kwa mara sababu anapoongea ubongo hutumika kufikiria cha kusema na kukipima kama ni sawa au laah.

Kuongeaongea sio vibaya, ubaya unakuja Je, kinachozungumzwa kina maana? Kina mantiki?

Mimi huwa naongea sana kwa watu ninaowafahamu tu, Huwa siongei kabisa mbele ya watu nisiowajua huwa nawasoma kwanza kwa mijadala midogo ya uchokozi. Kupitia kuongea huwa naelewa uelewa wa mtu ukoje.

Kamwe usionge ongee hovyo kama hujui upeo wa unaezungumza nae.
 
Ni kweli, ingawa wengine waongeaji sana lakini wanacmjitahidi kuchagua maneno.
Nadhani mada yako inazungumzia makundi ya Extroverts.

Lakini kumbuka siri ina muda wake wa kuishi, baada ya hapo huwa siyo siri tena. Wakati mwingine mtunza siri huitoa mwenyewe[emoji23]
Kazi kwako usije kusema hatukukuambia
 
lakini saikologia inasema hawa watu ndio marafiki wa kweli,ni rahisi sana kuhisi uwepo wa pengo lake na ni waaminifu kweli kweli hata ktk ndoa.

sasa chagua moja hapo kipi ni muhimu kwako kati ya hivyo.
 
lakini saikologia inasema hawa watu ndio marafiki wa kweli,ni rahisi sana kuhisi uwepo wa pengo lake na ni waaminifu kweli kweli hata ktk ndoa.

sasa chagua moja hapo kipi ni muhimu kwako kati ya hivyo.
Watu wakimya ndio watunza siri, wanauwezo wa kuona jambo au kusikia wakahifadhi siri ķwa miongo kadhaa
 
Wengi wao vichwa vyao havina filter yaani kinachopita kichwani ndio anakiongea ,hawafikiri kabla ya kuongea wao wanaongea kwanza ndio wanafikiri.. kwenye kumwaga Siri wapo vizuri yaani unaweza kumwbia Jambo lako lkn akalimwaga mbele ya watu hata kwa Njia ya kukutania

Afu mara nyingi watu wa hivi wanakuwaga ma big
 
kwanini uwe na siri sasa, siri ni dalili ya uchawi.. hao watu wako sahihi sana...
 
Wengi wao vichwa vyao havina filter yaani kinachopita kichwani ndio anakiongea ,hawafikiri kabla ya kuongea wao wanaongea kwanza ndio wanafikiri.. kwenye kumwaga Siri wapo vizuri yaani unaweza kumwbia Jambo lako lkn akalimwaga mbele ya watu hata kwa Njia ya kukutania

Afu mara nyingi watu wa hivi wanakuwaga ma big
Mkuu 😃😃😃😃

Yaani umepita mule mule, alafu wanapenda kufuatilia sana life la watu
 
kwanini uwe na siri sasa, siri ni dalili ya uchawi.. hao watu wako sahihi sana...
Kama ni hivyo secret service au TISS wote ni wachawi,

Unadhani kwanini idara za ujasusi huwa wanapenda kurecruit watu wakimya?
 
Kama boda-boda wale watu %kubwa ni waongeaji na hawana siri iko radhi akuonyeshe mke wa mtu alie mlala, tena ni waongo, ni wajuaji wa kila jambo.......sijui ndo sehemu ya kazi yao au kua idle pale wakati wanasubilia abiria.
 
Ila wanaconnection hao balaa ukiwa nao karibu ufi njaaa..
 
Kama ni hivyo secret service au TISS wote ni wachawi,

Unadhani kwanini idara za ujasusi huwa wanapenda kurecruit watu wakimya?

wachawi tu pia.... siri ni uchawi...

sasa natunza siri ya nini na iweje...
 
Back
Top Bottom