Watu wawili wa karibu Ikulu aliyekuwa rais Haiti kuhojiwa kuhusiana na njama za kumuua

The Mongolian Savage

JF-Expert Member
Joined
Jul 5, 2018
Posts
8,082
Reaction score
17,838
Wanajamvi habari za weekend

Maafisa wa karibu ya ikulu Haiti
Wako kizuizini wakihojiwa.



Ni Jean Liguel Civil. Huyu alikuwa mkuu wa Rais Jovenel Moise security Coordinator. Anabinywa sasa hivi sehemu salama.



Mwengine ni Dimitri Hérard, head of the General Security Unit of the National Palace naye anaminywa na kuhojiwa sehemu salama.



Pia mwanamama Magalie Habitant ambaye ni mwanasiasa maarufu na mwanachama wa chama pinzani cha PHTK political party ambaye Chama chake na Chama rais Moise aliyeuwawa waliungana na kuwa marafiki naye anaminywa na kuhojiwa sehemu salama kwasababu mamluki wauaji waliishi kwake kabla ya tukio.

Aidha wale raia wawili wa Marekani wenye asili ya Haiti.



James Solages 35 na Joseph Vincent waliokamatwa wanajitetea wenyewe walikuwa watafsiri tu na walijulishwa na mamluki wa Colombia ya kuwa walikuwa wanaenda kumkamata rais Moise akiwa hai siyo kumuua.

Pia mke wa mmoja wa mamluki wa Colombia anadai mume wake alipata kazi na kampuni ya ulinzi Colombia na kusafiri mwezi mmoja uliopita kwenda Dominican republic nchi iliyopakana na Haiti na inashare kisiwa kimoja kilichogawanyika hizo nchi mbili. Cha kushangaza amekuja kugundua mume wake alihusika kwenye mauaji ya ya Rais wa Haiti wakati muda wote alijua yuko Dominica Republic akifanya kazi ya ulinzi akilipwa dollars 2700 kwa mwezi .

Mamluki hawa walivamia na kufanikiwa kuingia makazi ya Rais na kummiminia rais J Moise risasi 12 na kumng'oa jicho lake la kulia.



Marehemu Rais Jovenel Moise alikuwa mfanya biashara mashuhuri wa magari na spare.



Kamuacha mjane Martine naye alijeruhiwa kwenye tukio na anapigania maisha yake hospitalini Florida Marekani.



Martine first Lady ana miaka 47



Wamebarikiwa na watoto watatu binti mmoja na vijana wawili



Mungu ailaze mahali pema peponi roho ya Rais Jovenel Moise na namtakia kheri mkewe apone haraka sana.

Senior JF local and international political analyst and correspondent.

Source: The sun na Dailymail online
 
Kuna uvumi ulienea jana port au prince mji mkuu wa Haiti eti Marekani wanatoa visa za humanitarian. Maskini wa Haiti kwa makundi wakamiminika ubalozi wa Marekani.

 
Huyu Solange 35 raia wa Marekani mwenye asili ya Haiti aliyehusika kumuua Rais Moise na kujitete alikuwa mkalimani. Mwaka jana aliwashtaki wazungu wawili majirani zake Florida eti walimuita nyani na kuwa anahofia maisha yake. Ugimvi ulitokea baina yao baada ya jamaa kujimilikia parkinf space ambayo haikuwa yake ikapelekea Ugomvi mkali na kuitwa nyani na eti akamaindi. Liuaji.
 
Mkuu ni kweli unayosema. Kwasababu sijaona breaking news huyu mwanamama mrembo kaondoka. Nadhani yuko mahututi hospital
Aise, niliona kwenye chanzo kimoja hivi. Lakini nimeingia fact check naona wamekanusha hiyo taarifa.
 
... kumbe Haiti, the Americas, ni wamakonde pure kuliko Afrika!
 
Mission imefanikiwa kwa zaidi ya 50%
Sema escaping root yao haikupangwa vzr. but the "Target" eliminated
 
Unaweza kukuta masterplan wa mchezo mzima ndiye kiongozi sasa, hawa wahusika hawamjui walikuwa tu wanawasiliana na kiongozi, na kazi imeisha wnatolewa kafara.
Siku zote ukipiga mission kama hizi wale wa chini lazima wauawe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…