Watu wenye vimradi vya kufuga kuku na kelele za kujiajiri

Watu wenye vimradi vya kufuga kuku na kelele za kujiajiri

Rog chimera

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2018
Posts
398
Reaction score
706
Assalam Aleykum wakuu

Katika uchunguz wangu nimegundua watu wenye vimradi vidogo vidogo ndio wamekuwa wakipiga kelele nyingi kuhusu swala la kujiajiri na wamekuwa wakiwadharau na kuwadhihaki wenzao walioko kwenye ajira.

Wengi wao pato wanalopata kutoka kwenye ujasiriamali wao huo ni dogo sana na wanapata tabu sana ukilinganisha na wale walioajiriwa ambao wanawadharau.😀😀😀😀.

NB: Neno wafuga kuku halija wa target wafuga kuku kama unavyofikiria , soma utafakari kwa makini.
 
Mimi nimeajiriwa ila najua mawazo mgando kama haya ndio yanayotufanya waajiriwa tunakufa masikini. Ni mawazo ya hovyo sana.

Hata kama umemzidi kipato huyo unayemuita mwenye kimradi cha kufuga kuku, tambua amekuzidi mambo mengi sana. Uhuru, ubunifu, experience na uwezo wa kukuza au kubadili biashara yake hiyo.

Ngoja siku kitumbua kiingie mchanga ndio utapata akili hapa mjini au unadhani wanaopoteza kazi ni maboya?

Naona mkuu kama una dalili za wivu na kukata tamaa!!
 
Mimi nimeajiriwa ila najua mawazo mgando kama haya ndio yanayotufanya waajiriwa tunakufa masikini. Ni mawazo ya hovyo sana.

Hata kama nimemzidi kipato huyo unayemuita mwenye kimradi cha kufuga kuku, tambua amekuzidi mambo mengi sana. Uhuru, ubunifu, experience na uwezo wa kukuza au kubadili biashara yake hiyo.

Ngoja siku kitumbua kiingie mchanga ndio utapata akili hapa mjini au unadhani wanaopoteza kazi ni maboya?

Naona mkuu kama una dalili za wivu na kukata tamaa!!
Ahsante mkuu kwa mchango wako .😀😀😀😀
 
Ahsante mkuu kwa mchango wako .😀😀😀😀
Mkuu nikushauri kitu ikiwa utaniruhusu! Badili kabisa approach yako kwa hawa wajasiriamali wadogo!

Jishushe, fanya urafiki na hao watu, jifunze maarifa yao, mapito yao na changamoto walizo nazo; waombe wakueleze fursa zao na malengo yao! Hakika utakuwa na hekima kama ile ya Mfalme Suleiman. Jaribu utanielewa. Na hekima hiyo itakusaidia sana maishani.
 
Mkuu nikushauri kitu ikiwa utaniruhusu! Badili kabisa approach yako kwa hawa wajasiriamali wadogo!

Jishushe, fanya urafiki na hao watu, jifunze maarifa yao, mapito yao na changamoto walizo nazo; waombe wakueleze fursa zao na malengo yao! Hakika utakuwa na hekima kama ile ya Mfalme Suleiman. Jaribu utanielewa. Na hekima hiyo itakusaidia sana maishani.
Ahsante mkuu , bado umeajiriwa???😛😛
 
Nini rai yako mkuu waache kufuga kuku wakaajiriwe?
Sio kila mtu anafuga anafanikiwa.

Kama huamini jaribu uone.
Nadhani wewe ni mmojawapo....so una stress za kushindwa mradi
Ujinga ni pale kila aliyeajiliwa anachukia kazi yake, anathamini kufuga kuku kuliko ajila
 
Ndio mkuu ila kasalary kote nainject kwenye miradi and will soon quit. Nina majuto tu sikuanza mapema!
We ni miomgoni mwa wale wasiotumia akili, mnadhani maisha yanaanza na hela, ni ulimbukeni wa vijana siku hizi kudhani kujiajiri ni kuingiza hela kwa miradi inayoweza kuwa duplicated kiurahisi na watu wengine. Badala ya kupenda kazi zetu, kuwa wabunifu, tumekuwa na mawazo makapi ya kusikia eti ufugaji wa kuku unalipa kila mtu anakimbilia huko huko, yaani nakuhakikishia ukiacha kazi kwa huo mradi wako ambao kila mtu anaweza copy na kufanya utajuta
 
Back
Top Bottom