1.Taarifa za uhakika kutoka kwa wasiri wetu zinasema Private Damas Clinton mwajiriwa wa Jeshi la Wananchi Tanzania ambaye alitambulika kirahisi katika video za ubakaji na ulawiti akiwa na wenzake.
Wote wamekamatwa na kutiwa nguvuni tangu jana
2.Wamehifadhiwa moja ya kikosi mkoani Morogoro,wanaweza kusogezwa mkoani Dar es saalam wakati wowote.
3.Hakuna taarifa kuhusu kukamatwa na kushikiliwa kwa Afisa Jeshi (Afande) aliyewatuma kubaka na kulawiti kama ambavyo video zinasikika, zaidi ya taarifa ya leo asubuhi ameonekana akiwa kambini katika mazoezi ya asubuhi "Mchaka Mchaka" pale RTS.
Huenda wanasubiriwa maofisa kutoka Makao makuu kwa hatua zaidi.
4.Kuna juhudi kubwa sana zinafanyika kumuokoa na kumsaidia Kiongozi wao "Afande" ambaye ni afisa Jeshi kwa ranki ya "CAPTAIN" aliye watuma kufanya udhalilishaji na ukatili
3.Moja ya njia inataka kutumika ni kumuondoa nchini kwa haraka Afisa Jeshi huyo na kumpeleka nchi za jirani kama sehemu ya kazi "Mission" ili kukwepa hatua za kisheria.
4.Mwana Mama huyu ambaye ni Afisa Jeshi ngazi ya "CAPTAIN" muwe wake pia ni Afisa jeshi ranki yake pia ni "CAPTAIN" Ingawa ranki hii sijaithibitisha kwa vyanzo vingine.
UTARATIBU UPOJE..?
1.kwa kawaida Jeshi la Polisi haliwezi kwenda katika kambi au kikosi chochote kumkamata mualifu ambaye ni askari katika kambi hizo.
2.Jeshi la Polisi Makao Makuu wanatakiwa kuandika Barua kwenda Makao makuu ya Jeshi kumuomba askari wao na kueleza sababu ya kumuomba askari huyo ikiwemo tuhuma zake ili waweze kukabidhiziwa.
3.Jeshi kwa utaratibu wao,wanavyo vyombo vya ukamataji ndani ya Jeshi (DMP) ambavyo vitaelekezwa kumkamata na kumfikisha Makao makuu kabla ya kumpeleka mahala anapohitajika na Jeshi la Polisi baada ya kupokea maombi rasmi.
4.Kama wataendelea kushikiliwa Jeshini kabla ya Polisi kukamilisha utaratibu huu,askari wa ranki za chini wana mahabusu zao tofauti na maafisa wanapokuwa wametenda makosa wakiwa ndani ya utumishi wa Jeshi.
5.Uwezekano wa Kushitakiwa katika Mahakama za Kijeshi bado upo kama pamoja na kuhojiwa na maelezo yao kwenda kwa Mwanasheria Mkuu wa serikali pamoja na ofisi ya Mkurugenzi wa mashitaka
Wanaweza kurudishwa katika Mahakama za Kijeshi kwa dhumuni la kuwasaidia.
ambapo hasara yake kwa umma na Jamii hakuna Chombo cha habari kitakachoruhusiwa kuingia kusikiliza mwenendo wa kesi na kuripoti kesi hiyo.
Mahakama ya kijeshi haihusiki na uhalifu huu uliofanyika nje ya majukumu ya jeshi, hii unatozwa hukumu katika mahakama za kiraia maana sio sehemu ya kijeshi
Ingekuwa imetokea kwenye mazingira ya majukumu kama vile wakiwa Mission ya ndani au nje ya nchi
Basi ingetakiwa kuhukumiwa kijeshi kwa kosa la "SEA" (SEXUAL ABUSE) katika chapter 9 ya sheria za kijeshi ambazo ni code of service discipline (CSD) na sheria za umoja wa kimataifa wa kijeshi GENIVA CONVENTION 3.
MAONI YA WANANCHI
Bado wana Imani na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) na wameapa kulinda hadhi na heshima ya Jeshi letu tukufu.
Kuoza kwa Samaki mmoja hawataki kusababishe kuoza kwa samaki wote,wanataka kuona JWTZ linaendelea kuwa kimbilio la Wananchi,Wanyonge ndiyo maana wanataka wahalifu wasilindwe kwa namna yoyote kuepuka kulichafua Jeshi letu tukufu lenye sifa lukuki Barani Africa na Duniani