Watuhumiwa waliolawiti mtoto Arusha wakosa sifa ya Kushtakiwa kwa kosa la Jinai kwa kutokuwa na umri sahihi

Watuhumiwa waliolawiti mtoto Arusha wakosa sifa ya Kushtakiwa kwa kosa la Jinai kwa kutokuwa na umri sahihi

Bushmamy

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2019
Posts
9,140
Reaction score
15,963
Sakata la mtoto wa kiume (3) kudaiwa amelawitiwa na watoto wenzie Jijini Arusha, limekuwa na sura mpya baada ya kesi kushindwa kufikishwa Mahakamani kwa madai kuwa waliotenda tukio hilo hawawezi kukabiliwa na kesi ya jinai kutokana na miaka yao kuwa chini ya umri wa kushtakiwa kwa kosa hilo.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Arusha Justine Masejo amethibitisha kuwa kesi hiyo haijafikishwa mahakamani kutokana na umri wa watuhumiwa hao kuwa mdogo kushtakiwa kwa kosa la jinai, mmoja akidaiwa kuwa umri wa miaka 5, na mwingine miaka 9.

"Kulingana na sheria za nchi watuhumiwa wale walikuwa chini ya umri wa kushtakiwa, mmoja alikuwa na miaka mitano na mwingine miaka tisa, mtoto wa miaka mitano huwezi kumshtaki kwa jinai, hilo shauri linashughulikiwa kinamna nyingine wakishirikiana na Ustawi wa Jamii" Kamanda Justine.

Aidha, Mama mzazi wa mtoto huyo amesema kuwa mtoto wake anaendelea kujisaidia damu na amekuwa na maumivu makali huku madaktari wakimwambia hamna dawa za kuweza kumponya mtoto wake.

"Madaktari wananiambia dawa hamna zinazoweza kumponya mtoto, wananiambia labda waje madaktari bingwa, nimeshachoka" Mama wa mtoto.

Pia soma: Arusha: Mtoto wa miaka 3 adaiwa kulawitiwa
 
Aidha, Mama mzazi wa mtoto huyo amesema kuwa mtoto wake anaendelea kujisaidia damu na amekuwa na maumivu makali huku madaktari wakimwambia hamna dawa za kuweza kumponya mtoto wake.
Aisee 😞😟
Hao watoto waliomfanyia mwenzao ukatili huu wamejifunzia wapi kwa umri huo? Malezi, malezi, malezi.

Wazazi na walezi kuwapa watoto uhuru wa kila kitu sio kuwapenda, ni kuwaangamiza ila tunaona ndio kwenda na wakati na ujanja kumbe ushamba. Matumizi ya simu na kompyuta kwa watoto yamezidi sana, huko kwenye simu wanaona na kujifunza mengi sana.

Kuwaruhusu watoto kwenda kwenye mabanda ya video nayo sio salama, hiyo tabia imekithiri sana dar na arusha ila wazazi wanaona ni sawa tu.

Kuwaruhusu watoto kuangalia maudhui yasiyofaa kwa watoto, mtoto anajijia na flash ina movies hujui hata maudhui yake na wewe upo umejipumzisha chumbani unachat jf au upo nje na kazi zako, ndani mtoto sauti kaweka ya chini kabisa anaangalia ujinga ambao unamuingia vilivyo akilini.

Hali ni mbaya ila tukizubaa itazidi kuwa mbaya zaidi, malezi sio kitu chepesi, umeshakubali kuwa mzazi/mlezi kubali kuwajibika na kugharamika kwa sababu matunda ya unachokipalilia ni miaka michache mbeleni utaanza kuona mazuri au mabaya yake.

NB: SAMAKI MKUNJE ANGALI MBICHI.
 
Sakata la mtoto wa kiume (3) kudaiwa amelawitiwa na watoto wenzie Jijini Arusha, limekuwa na sura mpya baada ya kesi kushindwa kufikishwa Mahakamani kwa madai kuwa waliotenda tukio hilo hawawezi kukabiliwa na kesi ya jinai kutokana na miaka yao kuwa chini ya umri wa kushtakiwa kwa kosa hilo.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Arusha Justine Masejo amethibitisha kuwa kesi hiyo haijafikishwa mahakamani kutokana na umri wa watuhumiwa hao kuwa mdogo kushtakiwa kwa kosa la jinai, mmoja akidaiwa kuwa umri wa miaka 5, na mwingine miaka 9.

"Kulingana na sheria za nchi watuhumiwa wale walikuwa chini ya umri wa kushtakiwa, mmoja alikuwa na miaka mitano na mwingine miaka tisa, mtoto wa miaka mitano huwezi kumshtaki kwa jinai, hilo shauri linashughulikiwa kinamna nyingine wakishirikiana na Ustawi wa Jamii" Kamanda Justine.

Aidha, Mama mzazi wa mtoto huyo amesema kuwa mtoto wake anaendelea kujisaidia damu na amekuwa na maumivu makali huku madaktari wakimwambia hamna dawa za kuweza kumponya mtoto wake.

"Madaktari wananiambia dawa hamna zinazoweza kumponya mtoto, wananiambia labda waje madaktari bingwa, nimeshachoka" Mama wa mtoto.

Pia soma: Arusha: Mtoto wa miaka 3 adaiwa kulawitiwa
Baba Mungu tusaidie sisi wanao
 
Back
Top Bottom