Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Watuhumiwa sita wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki leo December 06,2024, wakituhumiwa kutaka kumteka Mfanyabiashara Deogratius Tarimo katika eneo la Kiluvya Wilayani Ubungo Jijini Dar es salaam.
Waliofikishwa Mahakamani ni Bato Bahati Tweve, Nelson Elmusa, Anitha Alfred Temba, Isaack Mwaifuani, Fredrick Juma Msatu na Benki Daniel Mwakalebela.
Itakumbukwa December 04,2024 Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaaam liliwakamata Watu wanane wanaotuhumiwa kutaka kumteka Mfanyabiashara Deogratius Tarimo katika eneo la Kiluvya, Ubungo Dar es salaam.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Jumanne Muliro akiongea na Waandishi wa Habari alisema Watuhumiwa hao walikamatwa kwa nyakati tofauti katika Mikoa ya Dar es salaam, Ruvuma na eneo la Mbingu, Mlimba Mkoani Morogoro.
“Pia lilipatikana gari aina ya Toyota Raum ambayo ilitumiwa wakati wa tukio hilo huku ikitumia namba isiyo halisi T 237 EGE na baada ya ufuatiliaji kufanyika imefahamika namba yake halisi ya gari hiyo ni T237 ECF”
Pia, Soma: Polisi: Tumewakamata watuhumiwa waliokula njama ya kutaka kumteka Tarimo - Kiluvya
Waliofikishwa Mahakamani ni Bato Bahati Tweve, Nelson Elmusa, Anitha Alfred Temba, Isaack Mwaifuani, Fredrick Juma Msatu na Benki Daniel Mwakalebela.
Itakumbukwa December 04,2024 Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaaam liliwakamata Watu wanane wanaotuhumiwa kutaka kumteka Mfanyabiashara Deogratius Tarimo katika eneo la Kiluvya, Ubungo Dar es salaam.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Jumanne Muliro akiongea na Waandishi wa Habari alisema Watuhumiwa hao walikamatwa kwa nyakati tofauti katika Mikoa ya Dar es salaam, Ruvuma na eneo la Mbingu, Mlimba Mkoani Morogoro.
“Pia lilipatikana gari aina ya Toyota Raum ambayo ilitumiwa wakati wa tukio hilo huku ikitumia namba isiyo halisi T 237 EGE na baada ya ufuatiliaji kufanyika imefahamika namba yake halisi ya gari hiyo ni T237 ECF”