LGE2024 Watumishi ambao hawajapiga kura kukiona Songwe, watakaguliwa kama wana wino

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu,

Oneni huyu mpuuzi!

Your browser is not able to display this video.


Kupata taarifa na matukio ya kimkoa kuhusu Uchaguzi Serikali za Mitaa ingia hapa: LGE2024 - Special Thread: Orodha ya Mijadala ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Katibu Tawala Mkoa wa Songwe Bi. Happiness Seneda, amewataka watumishi wote mkoani humo kuhakikisha wanashiriki zoezi la kupiga kura ili kuchagua viongozi wa Serikali za Mitaa kwenye maeneo yao, kwani Serikali imetenga siku hii kuwa mapunziko kwa ajili ya zoezi hilo na sio vinginevyo na baada ya zoezi hilo utafanyika ukaguzi wa rangi kwenye kidole ili kuwabaini wale wote ambao hawakushiriki.
 
Upuuzi mtupu
 
Mbona rahisi sana kuepukana na hiyo Adhabu?! Ukidakwa hapo labda hukugelezeaga shuleni πŸ˜‚

Ink-pad zote hizo zilizojaa na kalamu mnashindwa kujijaza mawino kwenye vidole ndugu zangu?! πŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒ
Huyo RAS amefirisika kifikra.

Mtu kutumia haki yake (Kupiga Kura) ni hiari.
 
Kweli nchi imefilisika, huyo naye yuko kwenye kundi la wenyeakili!
 
she is very right,
lazima wote watakaothibitika kutokupiga kura wachukuliwe hatua za kinidhamu ili iwe fundisho..
watu kama hao ni muhimu wastaafishwe mapema kwa lazima. huo ni utovu wa nidhamu na uhujumu demokrasia wa kuwango cha juu sana, usio vumilika...

huko ni kukosa uzalendo na, ni sawa na uhaini tu,
 
Kama tupo North Korea.
 
Watumishi wa umma hii nchi wanashida sana daaah. Mtu anaamka tu na komwe lake anaanza kutoa matamko ya kipuuzi. πŸ˜†πŸ˜†πŸ˜† ubaya na mkoa wenyewe Songwe lazima watumishi watakiona
 
Niache kula bia niende nikapige kura, WTF. Kuna watumishi wanaonewa sana
 
πŸ’©πŸ’©πŸ’©πŸ’©πŸ’©πŸ’©
 
Kupiga kura ni kama masuala ya chanjo ya korona...ni hiari, ilitakiwa ushawishi ndio utumike zaidi
 
Mshamba tu huyo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…