YoungPastor
JF-Expert Member
- Sep 18, 2018
- 437
- 674
Alianzaga vizuri lakin... sijui kwasasaKuna huyu anaitwa Tony Kapola ndiyo yupoyupo tu. Yaani hamna neno ila ujanjaujanja tu.
kutoa muhimu mkuu.. changamoto ni kama madhabahu haina moto.Somo la utoaji Lina zungumziwa Sana kuliko chochote ...
Haya nakujibu kwa takwimu.Ni wakati gani ndani ya miaka 100 iliyopita hapakuwahi kuwa na vita, njaa, matetemeko ya ardhi au ndugu kugombana. Ninaheshimu sana imani za watu wengine lakini uongo mwingi pia sio uungwana.
Kadri watu wanavyokuwa wengi na matatizo/changamoto ndio huongezeka. Hii mbona inajulikana. It's the law of nature.Haya nakujibu kwa takwimu.
Vipi bado hujaridhika?
Nimetamani nipate message hii kwa what's up yangu ili nimtumie jamaa yangu mmoja ambaye ni mfia Imani na ni mzinzi pia, hataki kuacha uzinzi, anaenda navyo vyote..Kanisa la sasa limejaa motivational speakers na social commentators dizaini ya akina Tonny Kapola na Daniel Mugogo; na mrundikano wa manabii na mitume wenye tamaa ya pesa. Ugalatia unapitia kipindi kigumu sana!
👇👇👇👇👇👇👇
MWENYE SIKIO LA KUSIKIA ALIYE KANISANI ASIKIE LEO
Bwana YESU KRISTO atukuzwe ndugu yangu.
Karibu nikujuze ufunuo huu nilioambiwa kwa ajili ya watu wa Kanisa.
â– Nianze kwa kusema hivi Usipobadilika utaende jehanamu huku unaimba pambio, wewe mwimbaji ila mwasherati na mzinzi.
â– Usipobadilika utaenda jehanamu na sauti yako yenye upako, wewe mhubiri ila mzinzi na mwasherati.
â– Usipobadilika utaenda jehanamu huku nyimbo zako mwenyewe zikikusindikiza, kwa sababu tu wewe ni mwimbaji maarufu wa nyimbo za injili ila mwasherati na mzinzi.
1 Wakorintho 6:9 " Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa MUNGU? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa MUNGU, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,"
â– Uaskofu huku unaendelea na uzinzi wewe ni wa jehanamu, hata kama unaheshimika vipi hapa duniani.
â– Uchungaji wa viwango lakini ni mzinzi, wewe ni wa jehanamu na sio mbinguni.
â– Kuitwa Mtume au Nabii au Mwinjilisti au Mwalimu lakini huku wewe ukiendelea na uzinzi na uasherati wewe hakika ni wa jehanamu.
â– Ukiwa mtoaji safi, mshirika sana na bado wewe ni mzinzi na mwasherati tambua kwamba YESU anasema
Mathayo 7:21-23 "Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni. Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu."
â—ŹNdugu Mtumishi si unaendelea na uzinzi au usherati?
Ni rahisi sana kwamba YESU KRISTO atakuambia siku ukifa kwamba "Sikukujua wewe kamwe; ondoka kwangu, wewe mtendao maovu"
â—ŹWewe uliyetumwa na shetani ili utembee na watu wa Kanisa wenzako ili wewe na wao mkose uzima wa milele.
â—ŹWewe Mchungaji wa kondoo ambaye badala ya kuchunga kondoo wewe unatafuna kondoo mmoja mmoja wasio na akili.
â– Usipobadilika utaenda jehanamu hata kama kwa sasa unaitwa mzee wa Kanisa au shemasi au kiongozi wa vijana au kiongozi wa wamama au Mwalimu wa kwaya au mwanakwaya au Mwalimu wa watoto.
â– Usipotubu na kuacha uchafu wako ujue siku ile YESU Mwokozi atakuambia kwamba hakukujua kamwe.
â—ŹWewe Mchungaji unayetangaza Kanisani kwamba unaenda mbali kufanya huduma kumbe unaenda kwa hawara yako.
â—ŹEnyi wanakwaya ambao mmegeuzana chakula kila mwanakwaya.
MUNGU amenituma nisema na inawezekana hii ndio nafasi yako ya mwisho umepewa.
Kuna makanisa ni zaidi ya danguro.
Kuna makanisa ni zaidi ya chuo cha kujifunza ukahaba.
Kuna makanisa uzinzi na uasherati uko kiwango sawa na kwa wapagani.
1 Wakorintho 5:1 " Yakini habari imeenea ya kuwa kwenu kuna zinaa, na zinaa ya namna isiyokuwako hata katika Mataifa, kwamba mtu awe na mke wa babaye."
â—ŹKuna wamama wachungaji ni wazinzi na huwasaidia mabinti wa Kanisa kutoa mimba.
Kuna mabinti walishawahi kutoa hadi mimba za watumishi.
Ndugu, ni wakati wa kujikana na kujipambanua hata kama wanakwaya wenzako wote wameoza kwa uasherati na uzinzi.
Wewe usifanye dhambi hizo.
Ni wakati wa kujipambanua hata kama wabinti wenzako Kanisani ni waasherati.
Ndugu, kumbuka Neno la MUNGU linasema Wagalatia 6:5 " Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe."
Wengine watabeba mafurushi yao kwenda jehanamu na sio mbinguni.
Wewe mtoto wa Mchungaji wala hutaenda mbinguni kwa sababu baba yako au babu yako ni Mchungaji au Askofu.
Ndugu, umepewa nafasi ya kutubu wewe binafsi, ukiichezea nafasi yako ujue watu wa aina yako wataenda jehanamu.
Kuna watu wako Kanisani hata miaka zaidi ya 10 lakini watu hao hawajawahi kuwa kondoo bali wao ni mbuzi tu siku zote, ndugu kuna jehanamu ya moto kwa waovu.
Nilipewa maandiko manne kwa ufunuo huu ili mwenye sikio la kusikia asikie Leo na kuacha dhambi zote hasa uzinzi na uasherati.
Neno la MUNGU mwenyezi linasema
Ufunuo 2:11 "Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo ROHO ayaambia makanisa. Yeye ashindaye hatapatikana na madhara ya mauti ya pili."
Ufunuo 2:29 "Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo ROHO ayaambia makanisa."
Ufunuo 3:22 "Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo ROHO ayaambia makanisa."
Ufunuo 3:6 "Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo ROHO ayaambia makanisa."
Mimi nimekuambia Leo.
â– Yule aliye na sikio la kusikia asikie Leo na kuacha uzinzi na uasherati.
â—ŹKuna watu wengi sana wakiwa jehanamu wataaanza kuwalalamikia wachungaji wao kwamba kwanini hawakuwaonya wala kuwakemea, watawalaumu wachungaji wao kwa nini walihubiri mafanikio tu na sio toba.
Ndugu uliye wa Kanisa Mimi najua ni neema ya MUNGU mwenyewe ili ujifunze ujumbe huu kisha uache uzinzi na uasherati.
Mimi Peter Mabula ninamshukuru Bwana YESU maana alichoniambia kusema nimesema.
"Asante Eee Mwokozi wangu YESU KRISTO.
Mwenye sikio la kusikia atatubu na kuacha uzinzi na uasherati kuanzia Leo."
Natamani niseme mengi mno lakini naamini mwenye kuelewa ameelewa.
MUNGU akubariki kwa kujifunza somo hili muhimu.
Asante kama umelielewa Neno la MUNGU la siku ya leo ila nina neno moja la mwisho kwako leo.
Bwana YESU Amekaribia Kurudi.
Je, Umejiandaaje?
Je, Unaendeleza Dhambi Ili Siku Ile Uachwe Na Bwana YESU? Je, Umeshika Wokovu Na Utakatifu Hata Unyakuliwe Siku Ile Kwa Ajili Ya Kwenda Uzima Wa Milele?
Majibu Sahihi Yako Moyoni Mwako Ila Nakusihi Mpokee Bwana YESU Kama Hujampokea Na Nakusihi Ishi Maisha Matakatifu Ukiwa Ndani Ya Wokovu. Vya Dunia Tulivikuta Na Tutaviacha.
Ndugu, Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Kuokoka.
Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Wokovu Wa Bwana YESU Kwako.
By Mwl Peter Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la Bwana YESU.
+255714252292 (Sadaka na WhatsApp)
Ubarikiwe
AhahahahaKadri watu wanavyokuwa wengi na matatizo/changamoto ndio huongezeka. Hii mbona inajulikana. It's the law of nature.
Hivi sasa nyumba za ibada zinakazia mambo mawiliInjili ya kale ya akina Petro ilikuwa Rhema.
Rhema ni neno la Mungu kwa wakati husika. Yaani Mungu anasema kwa kinywa cha mtu. Anaweza kutumia neno hili la kila siku (logos) ila anaposema Mungu mwenyewe hulitia uzima na kutimiza kusudi lake kwa haraka kama umeme.
Ndio maana ukisoma kitabu cha Matendo ya mitume kimejaa matendo makuu mpaka kitabu kikaitwa MATENDO YA MITUME na si mausia au maneno ya mitume.
Anania na safira walipofanya udanganyifu Petro alitamka neno Rhema na ikawa vivyohivyo.
Sasa hivi wewe hata ukipeleka sadaka pesa uliyofanya ujambazi sawa, ulifanya ukahaba sawa.
Neno kutoka kwa BWANA (RHEMA) halipo.
Sasa hivi mtu akiuza mafuta ya upako hata kahaba anamuuzia tu hakuna shida maana ni biashara kama biashara zingine.
Mafundisho yanayofundishwa makanisani sasa ni mepesi na ya kawaida. Mtu yeyote anayeweza kuongea anaweza kuhubiri bila wasiwasi.
Unaangalia tu nini kinatrendi kwasasa unalinganisha na maandiko ya kwenye Biblia unashangiliwa mchezo umeisha.
Wale wahubiri ambao hawasimami madhabahuni kuhubiri mpaka wasikie sauti ya Mungu ikiwaambia waseme nini sasa hawapo.
Ni mazoea tu. Mtu akikumbuka niliwahi kufundisha somo fulani nilipata credit basi atalibeba akafundishe mahali pengine.
Kanisa limegeuka mahali pa kuanzisha vikundi vya kusaidiana na vya kikabila.
Mungu aliponye kanisa.
Muhubiri anapitia YouTube mahubiri ya wahubiri wengine naye huyabeba kanisani kwake.
Iko wapi kazi ya Roho wa Mungu?
Watu wametengana kwa dhambi ya uzinzi mpaka sasa wameona hakuna namna uzinzi usiwe dhambi ya kutengana maana kanisa Zima limejaa uzinzi.
Kanisa ambalo halina NENO HAI (RHEMA) ni kichaka cha uzinzi, uchawi, majungu na kila aina ya dhambi.
Cain na Abel hawakugombanaCain na Abel waligombana wakati gani??
Huo sio ugomvi. Ni mmoja alimuonea wivu mwenzako Hadi akamuua. Abeli hakuna na ubaya na Cain, ndio maana Mungu alienda kuongea na Cain.Kuweka rohoni wivu, huo sio ugomvi? Mpaka kufikia hatua ya kumuua ndugu yake?
Maana yake vimezidi.Ni wakati gani ndani ya miaka 100 iliyopita hapakuwahi kuwa na vita, njaa, matetemeko ya ardhi au ndugu kugombana. Ninaheshimu sana imani za watu wengine lakini uongo mwingi pia sio uungwana.
Sasa Kama unaona ni uongo, ungekaa pembeni mada haikuhusu. Unataka kuharibu uzi.Who told you I'm looking for victory here?? Technological advancement imekuwa kubwa sana ndio maana hata kuna implantation ya hizo figo na ongezeko la magari. Kusema eti kuna mtu alipaa juu na sasa anasubiriwa kushuka, huo ni uongo according to me.
Sio kweli.Kadri watu wanavyokuwa wengi na matatizo/changamoto ndio huongezeka. Hii mbona inajulikana. It's the law of nature.
Maneno mengi kumbe ndio walewale tu..By Mwl Peter Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la Bwana YESU.
+255714252292 (Sadaka na WhatsApp)
Ubarikiwe
Utakaa sana ubishi wako!Who told you I'm looking for victory here?? Technological advancement imekuwa kubwa sana ndio maana hata kuna implantation ya hizo figo na ongezeko la magari. Kusema eti kuna mtu alipaa juu na sasa anasubiriwa kushuka, huo ni uongo according to me.
Kanisa la sasa limejaa motivational speakers na social commentators dizaini ya akina Tonny Kapola na Daniel Mugogo; na mrundikano wa manabii na mitume wenye tamaa ya pesa. Ugalatia unapitia kipindi kigumu sana!
👇👇👇👇👇👇👇
MWENYE SIKIO LA KUSIKIA ALIYE KANISANI ASIKIE LEO
Bwana YESU KRISTO atukuzwe ndugu yangu.
Karibu nikujuze ufunuo huu nilioambiwa kwa ajili ya watu wa Kanisa.
â– Nianze kwa kusema hivi Usipobadilika utaende jehanamu huku unaimba pambio, wewe mwimbaji ila mwasherati na mzinzi.
â– Usipobadilika utaenda jehanamu na sauti yako yenye upako, wewe mhubiri ila mzinzi na mwasherati.
â– Usipobadilika utaenda jehanamu huku nyimbo zako mwenyewe zikikusindikiza, kwa sababu tu wewe ni mwimbaji maarufu wa nyimbo za injili ila mwasherati na mzinzi.
1 Wakorintho 6:9 " Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa MUNGU? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa MUNGU, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,"
â– Uaskofu huku unaendelea na uzinzi wewe ni wa jehanamu, hata kama unaheshimika vipi hapa duniani.
â– Uchungaji wa viwango lakini ni mzinzi, wewe ni wa jehanamu na sio mbinguni.
â– Kuitwa Mtume au Nabii au Mwinjilisti au Mwalimu lakini huku wewe ukiendelea na uzinzi na uasherati wewe hakika ni wa jehanamu.
â– Ukiwa mtoaji safi, mshirika sana na bado wewe ni mzinzi na mwasherati tambua kwamba YESU anasema
Mathayo 7:21-23 "Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni. Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu."
â—ŹNdugu Mtumishi si unaendelea na uzinzi au usherati?
Ni rahisi sana kwamba YESU KRISTO atakuambia siku ukifa kwamba "Sikukujua wewe kamwe; ondoka kwangu, wewe mtendao maovu"
â—ŹWewe uliyetumwa na shetani ili utembee na watu wa Kanisa wenzako ili wewe na wao mkose uzima wa milele.
â—ŹWewe Mchungaji wa kondoo ambaye badala ya kuchunga kondoo wewe unatafuna kondoo mmoja mmoja wasio na akili.
â– Usipobadilika utaenda jehanamu hata kama kwa sasa unaitwa mzee wa Kanisa au shemasi au kiongozi wa vijana au kiongozi wa wamama au Mwalimu wa kwaya au mwanakwaya au Mwalimu wa watoto.
â– Usipotubu na kuacha uchafu wako ujue siku ile YESU Mwokozi atakuambia kwamba hakukujua kamwe.
â—ŹWewe Mchungaji unayetangaza Kanisani kwamba unaenda mbali kufanya huduma kumbe unaenda kwa hawara yako.
â—ŹEnyi wanakwaya ambao mmegeuzana chakula kila mwanakwaya.
MUNGU amenituma nisema na inawezekana hii ndio nafasi yako ya mwisho umepewa.
Kuna makanisa ni zaidi ya danguro.
Kuna makanisa ni zaidi ya chuo cha kujifunza ukahaba.
Kuna makanisa uzinzi na uasherati uko kiwango sawa na kwa wapagani.
1 Wakorintho 5:1 " Yakini habari imeenea ya kuwa kwenu kuna zinaa, na zinaa ya namna isiyokuwako hata katika Mataifa, kwamba mtu awe na mke wa babaye."
â—ŹKuna wamama wachungaji ni wazinzi na huwasaidia mabinti wa Kanisa kutoa mimba.
Kuna mabinti walishawahi kutoa hadi mimba za watumishi.
Ndugu, ni wakati wa kujikana na kujipambanua hata kama wanakwaya wenzako wote wameoza kwa uasherati na uzinzi.
Wewe usifanye dhambi hizo.
Ni wakati wa kujipambanua hata kama wabinti wenzako Kanisani ni waasherati.
Ndugu, kumbuka Neno la MUNGU linasema Wagalatia 6:5 " Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe."
Wengine watabeba mafurushi yao kwenda jehanamu na sio mbinguni.
Wewe mtoto wa Mchungaji wala hutaenda mbinguni kwa sababu baba yako au babu yako ni Mchungaji au Askofu.
Ndugu, umepewa nafasi ya kutubu wewe binafsi, ukiichezea nafasi yako ujue watu wa aina yako wataenda jehanamu.
Kuna watu wako Kanisani hata miaka zaidi ya 10 lakini watu hao hawajawahi kuwa kondoo bali wao ni mbuzi tu siku zote, ndugu kuna jehanamu ya moto kwa waovu.
Nilipewa maandiko manne kwa ufunuo huu ili mwenye sikio la kusikia asikie Leo na kuacha dhambi zote hasa uzinzi na uasherati.
Neno la MUNGU mwenyezi linasema
Ufunuo 2:11 "Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo ROHO ayaambia makanisa. Yeye ashindaye hatapatikana na madhara ya mauti ya pili."
Ufunuo 2:29 "Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo ROHO ayaambia makanisa."
Ufunuo 3:22 "Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo ROHO ayaambia makanisa."
Ufunuo 3:6 "Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo ROHO ayaambia makanisa."
Mimi nimekuambia Leo.
â– Yule aliye na sikio la kusikia asikie Leo na kuacha uzinzi na uasherati.
â—ŹKuna watu wengi sana wakiwa jehanamu wataaanza kuwalalamikia wachungaji wao kwamba kwanini hawakuwaonya wala kuwakemea, watawalaumu wachungaji wao kwa nini walihubiri mafanikio tu na sio toba.
Ndugu uliye wa Kanisa Mimi najua ni neema ya MUNGU mwenyewe ili ujifunze ujumbe huu kisha uache uzinzi na uasherati.
Mimi Peter Mabula ninamshukuru Bwana YESU maana alichoniambia kusema nimesema.
"Asante Eee Mwokozi wangu YESU KRISTO.
Mwenye sikio la kusikia atatubu na kuacha uzinzi na uasherati kuanzia Leo."
Natamani niseme mengi mno lakini naamini mwenye kuelewa ameelewa.
MUNGU akubariki kwa kujifunza somo hili muhimu.
Asante kama umelielewa Neno la MUNGU la siku ya leo ila nina neno moja la mwisho kwako leo.
Bwana YESU Amekaribia Kurudi.
Je, Umejiandaaje?
Je, Unaendeleza Dhambi Ili Siku Ile Uachwe Na Bwana YESU? Je, Umeshika Wokovu Na Utakatifu Hata Unyakuliwe Siku Ile Kwa Ajili Ya Kwenda Uzima Wa Milele?
Majibu Sahihi Yako Moyoni Mwako Ila Nakusihi Mpokee Bwana YESU Kama Hujampokea Na Nakusihi Ishi Maisha Matakatifu Ukiwa Ndani Ya Wokovu. Vya Dunia Tulivikuta Na Tutaviacha.
Ndugu, Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Kuokoka.
Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Wokovu Wa Bwana YESU Kwako.
By Mwl Peter Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la Bwana YESU.
+255714252292 (Sadaka na WhatsApp)
Ubarikiwe
Wanatumia ujanjaujanjaHivi sasa nyumba za ibada zinakazia mambo mawili
- Masuala ya ndoa na mahusiano ili ku draw attention ya watu hata wasio waumini wa maeneo husika
- Sadaka na utoaji ili kuneemesha watumishi
Sawa, ngoja niendelee kukaa sana na ubishi wangu.Utakaa sana ubishi wako!