Watumishi wa TRA Waliochaji Rushwa ya Tsh 30 Billion, Kisha Kumfungulia Huyu Mama Kesi ya Uhujumu Uchumi, Washughulikiwe

Watumishi wa TRA Waliochaji Rushwa ya Tsh 30 Billion, Kisha Kumfungulia Huyu Mama Kesi ya Uhujumu Uchumi, Washughulikiwe

TRA kuna baadhi ya watumishi wanaonra sana wivu wafanyabiashara.
TRA kuna wengine imekuwa kichaka cha wababaishaji na watu wanaodhulumu wengine kwa kujidai wanatimiza sheria.
Wengi ni wala rushwa wakubwa. Na cha kushangaza, they always seem to get away with it.

Haya bwana......
Tunawasubiri tuwape fremu nao wafanye biashara baada ya kustaafu.
 
Kuna jamaa mmoja alitoa malalamiko yake kwa waziri mkuu kipindi Magufuli akiwa hai. Magufuli akaagiza wahusika washughulikiwe. Ilipigwa dana dana na jamaa karibia angeuawa. Mara ya mwisho nilisikia walikuwa wamemgeuzia kibao. Nataka tu kukuambia kuwa hii mitandao inahusisha mpaka mawaziri na vyombo vya dola. Dawa ni kuiondoa CCM.
Kuiondoa CCM na Katiba Mpya
 
Kidata anafanya vizuri wamwache aisee!

Nasikia ako na maono mazuri sana ya hiyo TRA.

Hizo tuhuma zichunguzwe iwapo ikithibitika kuna ukweli wahusika wachukuliwe hatua stahiki.

Sio kila tatizo ufukuze kiongozi , ni afadhali kushughulikia tatizo kwa kushirikiana na uongozi badala ya kutimua kiongozi.
Inakuwaje Kidata hayaoni haya sasa mpaka yanakuja kutamkwa mbele ya Waziri Mkuu?
 
Inakuwaje Kidata hayaoni haya sasa mpaka yanakuja kutamkwa mbele ya Waziri Mkuu?



Kwa sasa ni ngumu kuthibitisha kama madai yale yana ukweli kiasi gani au la !

Wengi waliongea kwa mihemko zaidi than facts.

Sasa watu wanakataa hadi kutumia mashine za kutokea receipts unawaonaje?

In the first place ni kutaka udanganyifu?

EFD receipts hawataki kutoa na enforcement hawataki?! [emoji848][emoji848]

Hivi kuna u-serious kweli kwenye hilo?

Bongo kazi ya kukusanywa kodi ikifanyika kama Kenya hali itakuwa ngumu maradufu kuliko sasa.

Hao wakariakoo washukuru hali ilivyo sasa , afadhali ni kubwa mno.

Hata hivyo nilisikia amekuwa akichukua hatua Na kufanyia kazi Maswala ya ukiukwaji wa maadadili, ni jambo endelevu sizani kwamba alikuwa amekaa tu bila kuwa na mikakati ya kudhibiti.
 
Rais Samia alikwisha piga marufuku kudai hizo kodi accumulated zaidi ya miaka 2
Ni miaka mitano sio miwili, mitano kwenda nyuma kuanzia siku aliyotoa tamko hilo.

Japo Rais hana mamlaka kusimama jukwaani kufuta kodi! Ukimpa Rais au watendaji wa umma mamlaka ya kufuta kodi kwa mdomo basi mmewapa pia mamlaka ya kutunga kodi kwa mdomo!

Hawa marais wakiwa nyumbani kwao huwa wanatucheka sana tulivyo mambumbumbu wa dunia, yani tunamwongezea kiongozi madaraka ya mdomo ambayo kimakaratasi hana! Ndio maana maafisa wa TRA wanawaambia wafanyabiashara amri za majukwaani ni kauli za uongo, hadaa za wanasiasa.

Kwa hiyo, kwa tamaduni za kodi za Tanzania, ukikwepa kodi miaka miwili mpaka mitano, deni linaenda linapotezewa kwa huruma ya Rais mpya! Biashara ikikushinda kwa kodi achana nayo fanya mengine baadae ibuka tena itakuwa imesamehewa, ndio hicho Samia alichonuia kuki encourage ??? Hakuna nchi inayoendeshwa hivyo!

Tunalalamika tunataka Katiba Mpya ya kupunguza mamlaka ya Rais wakati huo huo tunampa madaraka ambayo hata kwenye Katiba ya sasa hana!
 
Mh Rais na viongozi wote kwa ujumla embu tungeni adhabu ya kuwanyonga maofisia wanao fanya mambo yakinyama kama haya kweli huyu mwanamke amefanyiwa haya yote kwa fitina hao walio mtengenezea fitina wanajulikana why kukaa kimya?
Naongea yeye hajamsikia kamishna kidata nae taarifa alinazo kuhusu huyo mwanamama zimekaaje? Tumesikia upande 1 huyo mfanyabiashara
 
Kwamba, hivi huyu mama anaweza kuwa na biashara kubwa kiasi gani ya kutoa rushwa ya TZS 30bn au 15bn au 10bn na bado akaendelea ku - survive katika game ya biashara?
Msikilize vizuri. Hajasema aliombwa rushwa ya bilion 30. Na hajatamka neno rushwa. Huyu mleta mada wetu ndio ame introduce rushwa.

Kodi ndio ilikuwa bilioni 30. Amesema "TRA wakatoa assessment ya bilioni 30." Assessment maana yake kodi, sio rushwa. Makadirio ya kodi.

Mfanyabiashara ndio anajua ndani ya makontena 20 kulikuwa na nini. Na ndio maana wala hakubisha kiasi cha kodi, yeye kasema "sikuwa na hela." She knows what she brung to the country. Ni hadithi ya upande mmoja wa mfanyabiashara. Hatujasikia claims za TRA.
 
Huyu Mama ni mmoja kati ya walioongea jana mbele ya PM. Alidaiwa kodi ya Tsh 30 Billion kwa containers zake 10 alizo import. Baada ya kuonyesha kuwa hana hizo fedha akatengenezewa mashtaka ya uhujumu uchumi. Waliosokia kikao cha PM wakamfutia shtaka la uhujumu uchumi. Na kisha usiku wa kuamkia mkutano wa PM wakamuita akatoe mzigo.

Hivi ni vitendo vinavyorudisha nyuma maendeleo ya wafanyabiashara na nchi kwa ujumla. Nashauri vyombo vya dola vishughulike na Meneja TRA wa Mkoa wa Ilala pale Kipata na wengine wote waliohusika
View attachment 2626036
Skandali.....
 
Hao maafisa walitaka rushwa Kwa huyo mama, in short hao ma officer ni wahuni na washenz.i na wahujumu uchumi na Hawana utu wangetakiwa wamsaidie, Huwa nawaza why Watanzania tunapenda kukomoana hivi, huyu mama kumfungia kumeharibu uchumi na kuathiri aliowaajiri na kumtegemea, na hao ma officer hawakufikiria kweli multiplier effect yake. Saa ingine watu watumie busara kuangalia mambo Kwa upana faida na hasara then wa negotiate
Tunapotaka somo la "KUKURU" liingizwe katika MITAALA ya shule za msingi kwa kushirikiana TAKUKURU-WIZARA YA ELIMU tunamaanisha.....

Tuna safari ndefu bado......
 
Huyu Mama ni mmoja kati ya walioongea jana mbele ya PM. Alidaiwa kodi ya Tsh 30 Billion kwa containers zake 10 alizo import. Baada ya kuonyesha kuwa hana hizo fedha akatengenezewa mashtaka ya uhujumu uchumi. Waliosokia kikao cha PM wakamfutia shtaka la uhujumu uchumi. Na kisha usiku wa kuamkia mkutano wa PM wakamuita akatoe mzigo.

Hivi ni vitendo vinavyorudisha nyuma maendeleo ya wafanyabiashara na nchi kwa ujumla. Nashauri vyombo vya dola vishughulike na Meneja TRA wa Mkoa wa Ilala pale Kipata na wengine wote waliohusika
View attachment 2626036
Hakika hao TRA wanastahiri kinachowahusu.

Lakini hapo hapo, huyo mama ni sehemu muhimu wa tatizo lenyewe.

Huyu ni mfanya biashara mzoefu, hadi kapata uwezo wa kuingiza kontena zote hizo, ni wazi anao uzoefu kwenye kazi hiyo.

Sasa swali la kujiuliza ni, je, alipoagiza hakujua kwamba mzigo wake ungehitaji kulipiwa ushuru stahiki?

Inavyoonekana, alishakuwa na uzoefu wa njia za mkato, kwa njia moja au nyingine, safari hii kakuta mtu wake hayupo, na waliokuwepo wakaona fursa yao kumtoa upepo.

Haya ndiyo madudu yanayotakiwa kuondolewa kwenye mfumo mzima wa kodi.

Pasiwepo na mtu yeyote kujitungia tu taratibu zake pembeni.

Taratibu zilizopo zifuatwe na ziimarishwe zaidi ili zifanye kazi ipasavyo.

Kodi ya "kukadiriwa na mtu" bila ya mwongozo wa kufanya hivyo unaoeleweka ndiyo njia ya kuvuruga kazi za TRA.
 
Wetu wanajua sana kucomment!Taarifa zilizopo yule mama ni Mjanja Mjanja sana!Hivi tangia lini mfanyabiashara amekuwa rafiki wa kodi?

Taarifa za yule Mama zipo wazi sana muda,bahati mbaya ndio mnamsikia leo!Ni tycoon wa michezo ya kumkwepa zakayo!

Sent from my Infinix X6511B using JamiiForums mobile app
Wewe hata hujielewi, wale wafanyabiashara wamekiri kukwepa kodi kwasababu kodi sio rafiki. Tanzania kodi ni kubwa mno inabidi waweke kodi rafiki biashara ifanyike bila vikwazo
 
Back
Top Bottom