Watumishi wa Umma waombwa na Hazina kuorodhesha Dini na Kabila zao. Rais Samia na Wasaidizi wako, haya yanafanyika kwa lengo gani?

Mimi nauliza tu, kwani dini ni kristo na uislamu tu? Kuna hindu, sikh, bahai na kadhalika.
 
sijui hio form ila nashangaa mbona ni miaka ming particulars huwa kuna sehem ya tribe, religion ni muda mrefu kweli lipi limekua la ajabu
 
Data is power

Watu hawataki dini zao zijulikane, wanataka kuficha nini?

Iacheni serikali ipate takwimu sahihi ili kama kuna ubaguzi wa kidini katika ajira iweze kurekebisha hilo tatizo kwa ajili ya umoja na mshikamano wa kitaifa
 
Mgalitaya amechanganyikiwa. Ndio mambo mkuu Keki ya Taifa ni ya wote
 
Upuuzi wa mama.
 
Mungu aliipenda Sana Tz kwa kutupa Nyerere kua baba wa Taifa maana bila hivyo nchi hii ingekua imegawanyika kikabila/kidini mbaya kabisa.

Asante Sana Mungu.
Na tusipo ungana kukataa kwa nguvu viashiria vya kutugawa kuna siku tutalia na kusaga meno
 
Kwamba hadi gesiti hausi huu utaratibu upo tokea kitambo
 
sijui hio form ila nashangaa mbona ni miaka ming particulars huwa kuna sehem ya tribe, religion ni muda mrefu kweli lipi limekua la ajabu
Haya mambo yanaanzia jikoni, huenda walioyavujisha wanajua kinachoendelea ndio maana wanalalamika...
 

Hoja ya kishamba zilizokwisha pitwa na wakati
 
Siku Taifa hili likiparaganyika mikononi mwako, hao unaowaona, watakukataa.

Sidhani Kama Samia anaijua vizuri historia ya nchi anayoingoza kwani kama angeijua hii leo asingekuwa anavalishwa ngozi za wanyama na kuushabikia Uchifu nchini!!
Nyerere alitoka ukoo wa Chief wa wazanaki na hata hivyo alifanikiwa kupigachini uchifu kwasababu alijua kwa undani kuwa hiyo taasisi haileti umoja katika nchi bali kuigawa nchi!! Umoja wa nchi hii umewezeshwa pamoja na mambo mengine kwa kuutokomeza ukabila hivyo Hangaya kuwapigia chepuo hao machifu wa zamani ni kutaka kuligawa TAIFA!! Mama jitahidi kusoma historia ya nchi ili angalau upate kuifahamu ingawa hujajaliwa kuvitembelea vijiji vingi hapa nchini!!!
 
Mi naona hakuna shida yoyote hivo vitu kuulizwa kwani sio vyako hivo vilivyoulizwa? Kuna ubaya gani mwajiri kukufahamu vizuri mtumishi wake?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…