Uchaguzi 2020 Watumishi wenzangu tuliotumbuliwa kwa sakata la vyeti feki tumchague Magufuli 2020

Uchaguzi 2020 Watumishi wenzangu tuliotumbuliwa kwa sakata la vyeti feki tumchague Magufuli 2020

wankuru nyankuru

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2019
Posts
495
Reaction score
775
Mimi ni mmoja wa watumishi wa Serikali tuliobainika kuwa na vyeti feki kwenye zoezi la uhakiki wa vyeti feki lililofanyika mwaka 2016.

Nakumbuka takribani watumishi 9000 tulikumbwa na hili sakata la kuwa na vyeti feki. Kwa tathimini iliyofanyika kupitia kundi la sogosi la watumishi tuliokutwa na vyeti feki mwaka 2016 inaonesha kuwa zaidi ya 80% ya watumishi hao waliokutwa na vyeti feki hawana kinyongo na mgombea urais kupitia CCM na wanadai kuwa wangetamani watumishi wenzao waliokutwa na vyeti feki wamuunge mkono mgombea kupitia CCM ili aendelee kuinyoosha nchi iliyokuwa imeoza kwa masuala ya ufisadi, janja janja kwa baadhi ya vigogo waliokuwa wanatumia nafasi zao kuwaingiza ndugu zao serikalini bila kufuata taratibu za Serikali.

Wakaenda mbali kwa kusema na kukiri kuwa in kweli waliwazibia nafasi za ajira serikalini watoto wa maskini waliosoma lakini hawakupata ajira Serikalini kutokana na sababu za baadhi ya wahuni kuziba nafasi.

Kufuatia mjadala unaondelea huko kwenye kundi la sogosi wengi ( majority) wanatoa maoni kuwa watamchagua Magufuli tarehe 28/10/2020 ili aendelee kuinyoosha nchi.

Wengine pia wameomba watumishi ambao wanasema hawajapandishwa madaraja wasiwe na wasi wasi na wamuunge mkono Magufuli kwani tayari ameshaahidi kuwapandisha madaraja na kuwaongezea mishahara minono kabla kipindi chake kuisha.
 
Hata kama mlitumbuliwa kwa vyeti feki, lakini wehuoni kwamba basi mlipaswa mlipwe stahiki zenu kwa utumishi wenu ulio tukuka kabla hamja tumbuliwa..??
NA wewe je utamlipa nini huyo maskini aliye kosa nafasi ya ajira miaka hiyo yote? Ulihonga na ukapata ajira kwa cheti feki, mwenzako akalazwa na njaa na familiya yake kwa kumkosesha nafasi yake ya halali, JE UTAMLIPA NINI?

KIsheria mnatakiwa mshtakiwe na mlipe fidia...
 
Kwa vyote vile hata wakipiga kura ya hapana kwake jumla yao ni 9000 unafikiri watamuondoa la hasha. Mimi nitampa kura ya ndiyo aendelee kudhibiti
Hesabu zako sio halisia. Watumishi 9000×watoto wao×wenza wao×ndugu tegemezi wao× wasamaria wema= ...............

Hivyo kundi lenye hasira za watumishi kutimuliwa bila ingalau kulipwa mafao ni zaidi ya watumishi husika wenyewe
 
Ushauri fair kabisa. Hii ndo maana halisi ya kuwajibika kwa mambo ya kipuuzi uliyoyafanya.. Wanaoponda kwenye comments watakuwa nao waghushi vyeti
 
Hesabu zako sio halisia. Watumishi 9000×watoto wao×wenza wao×ndugu tegemezi wao× wasamaria wema= ...............

Hivyo kundi lenye hasira za watumishi kutimuliwa bila ingalau kulipwa mafao ni zaidi ya watumishi husika wenyewe
Walichokipata kwa njia ya udanganyifu,kiliwatosha, mafao yanini kwa wadanganyifu🤔?
 
Kwahiyo ulitaka uendelee kubaki kazini n vyeti vyako feki .?

Kwani waliokua na vyeti feki ni wahutu?au wanyarwanda?kipo wapi mbona hata kuajiri watu wapya hamna?tofautisha ukatili na kua strict,hebu niambie nchi imenufaika na kipi kwa kuwatumbua vyeti feki?

Hebu niambie nani alitengeneza hizo loop holes?natumai kuna chama kilitawala hapo katikati tofauti na CCM?natumai Hawa victims hawakufanya kazi na jitihada zao hazikujenga Taifa ,Natumai hili kosa wao wenyewe ndio waliifanya serikali i paralyse mifumo yake isifanye kazi ili wapate kazi ,natumai maelfu ya watendaji wa serikali hawakushiriki,natumai pia Hawa watu hawakua wanachangia mafao ya mfuko wa jamii ambayo serikali hukopaga ,na Nadhani pia serikali walikua hawakati paye as you earn bila kusahau hela hizi walikua wanatumia kenya ,Uganda,Rwanda au nje ya nchi wakiutengeneza uchumi wa huko

Hivi unafahamu serikali inaweza ikaanzisha program hata Kama haina faida ili mradi tu wapunguze unemployment rate na kuchochea uchumi?

Hamna sheria isiyokua na exception hapa ndio maana ya busara inakuja
 
Back
Top Bottom