Wauguzi walimwambia anawasumbua akajifungua sakafuni, kichanga chafariki

Wauguzi walimwambia anawasumbua akajifungua sakafuni, kichanga chafariki

Walimwambia tu samahani,mtoto ametushinda.....yeye ni C-section....alipojisikia uchungu akakimbilia hospital njian alijisikia kupush,lakini Mwenyezi Mungu alimfikisha hospital salama,wauuguz wakampokea ingali anaendelea kupiga kelele kuwa anataka kupush,kumwingiza leba nesi mmoja akasema huyu ni C-section akapasuliwe nadhani baada ya kuona ule mshono....wakaleta kitanda chao apelekwe chumba husika ...kile kitendo cha kunyanyua mguu apande mtoto akazaliwa na kudondoka chini kwa kuangukia kichwa(mwisho wa siku wakaishia kusema sema "samahani mtoto ametushinda).....ukitaka kisa kingine nikuhadithie nilichoshuhudia mtoto wa kilo 5 alivyokufa mbele ya macho yangu kwa uzembe wa manesi wakati nikijisubiria leba(usiwe mkali tu,kila sekta haikosi watu wazembe ndugu)
Daahh...poleni sanaa...Mimi nimeshuhudia Amana mtu akizaa chooni kabisaa miaka Ile na nesi anaitwa anajibu hakuna nesi wa chooni ukimaliza kuzaa uje huku tukuhudumie,haya mwingine akizaa pale chini akasaidiwa na wajawazito wenzio ndo wakaja...manesi wa bongo kichomi
Mimi nashukuru nikifika Cha kwanza mkono natanguliza fastaa na sichelewi leba nkifika nimezaa ndo napata treatment za kistaf balaa... maana najua Mimi ndo ntapoteza kiumbe mwisho wa siku wao hawajali hata chembe,manesi wengi ni wakala wa shetani
 
Hospitali ni ya wilaya, nesi anayetuhumiwa kufanya uzembe ni wa hospitali ya wilaya, anayeunda tume ni mganga mkuu wa hospitali ya wilaya....!!! Yaani mtuhumiwa anaunda tume kujichunguza..!! Halafu kabisaa tunangoja majibu ambayo yakiwa mabaya yanaweza yakala kichwa cha muunda tume..!!! AJABU NA KWELI
Hakuna tume na hakuna wa kufukuzwa hakuna watu wanaolindana kama kada ya afya na hivi wanaaminika ndo usiseme
 
Haya mambo yapo sana kwenye vituo vya KUTOLEA huduma vya SERIKALI.. Sijui BAADHI YA WATUMISHI WA UMMAH NANI AMEWALOGA .... Ukienda kujifungua private watafanya maandalizi yote LAKINI serikalini utakuta mtu unamwambia nakaribia kusukuma LAKINI YEYE ATAKOMAA BADO AKIREJEA MUDA WAKE ALIOUKADIRIA!!!!! MBAYA ZAIDI UNAKUTA HAMA HATA CHA MAANA ANACHOKIFANYA NA WAKATI MWINGINE UNAKUTA YUKO BUSY NA SIMU..


sasa mziki unakuja mtu anataka kusukuma kweli MARA WATAANZA KUITANA NAOMBA MKASI, NAOMBA KIBANIO CHA KITOVU CHA MTOTO, MARA NAOMBA KADHAA N.K.
. Unajiuliza mtu amefika muds mrefu anakwambia anajisikia vibaya kwanini usimuhudumie???

Tanzania ina wasomi wa kutosha kwa sasa ifike wakati watu ambao hawako tayari kuwahudumia WATANZANIA watafute sehemu nyingine ya kupatia UGALI!!!! Mbona private hukuti hayo manyangamanyanga???

Dawa ni kufukuza kuanzia Mgdanga mfawidhi, katibu wa Afya, Matron, section incharge na wahusika wote!!!!!

Rudisha mtaani na kuleta watu wapya!!!

WATUMISHI wetu wa ummah wanaamini ukiipata kazi ya serikali BASI WEWE NI MFANYAKAZI WA MILELE!!!

Ndiyo maana unakutana na WATUMISHI walevi na tena we anakuwa wamelewa wakati wa KAZI na bado hakuna hatua stahiki zinachukuliwa!!!!!

Kwa utumishi huu productivity na efficiency ni ndogo sana!!! Ifike wakati huu mfumo ufanyiwe upholstery....

Leo Mashirika yetu ya UMMA kama TBA, TEMESA, WAKALA WA MELI, NDEGE n.k yanaendeshwa huku productive na efficiency zikiwa chini mno ni kwa sababu ya MFUMO MBAYA WA UTUMISHI WA UMMAH...

Watu wanapanda madaraja KWA MUDA WALIOTUMIKIA NA SIYO UFANISI, UTEUZI WA VIONGOZI NA WATENDAJI WAKUU UNAANGALIA UNAZI KWENYE CHAMA KWA KIWANGO KIKUBWA NA SIYO KUTANGULIZA UTENDAJI, Je katika mazingira HAYA TUTEGEMEE NINI?

Hapo mganga Mfawidhi atawafunika watumishi wake na STORY INAISHIA HAPO....

Mishahara iwe based on performance au kazi zote ziwe za MIKATABA renewable based on performance UONE KAMA KUNA MTU ATAZEMBEA!!!!

Serikali inafanya KAZI NZURI SANA YA KUJENGA MIUNDOMBINU NA KUAJIRI LAKINI WANAOAJIRIWA WAKISHATHIBITISHWA KAZINI BASI WANAANZA KUFANYA KAZI KWA MAZOEA....

SO SAD.......

Mpaka unajiuliza na haya nayo yanamsubiria RAIS ATOE MATAMKO??????
Hai. Mkazi wa Wilaya ya Hai, Happiness Massawe (39), amegoma kuchukua mwili wa kichanga hospitalini kwa wiki moja akidai kifo cha mtoto wake kimetokana na uzembe wa baadhi ya wauguzi.

Happiness, aliyejifungua katika Hospitali ya Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro alisema Oktoba 31 mwaka huu alipohisi dalili za uchungu alikwenda hospitalini hapo kwa ajili ya kujifungua na alipofika alipokewa na wauguzi.
Hata hivyo, alisema alipopata uchungu hakupewa ushirikiano badala yake alijifungulia sakafuni.

Juzi, Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Hai, Itikija Msuya alithibitisha kuwapo kwa tukio hilo akisema ameunda kamati ya kuchunguza ili kubaini kilichotokea siku hiyo.

“Kwa taarifa nilizopewa mtoto alizaliwa zero beating (akiwa amekufa) japo kuna dalili za uzembe ulifanywa na watoa huduma. Nimeunda kamati kuchunguza na watakaobainika hatua za kisheria zitachukuliwa,” alisema Dk Msuya.

Akizungumzia hali ilivyokuwa, Happiness alisema baada ya kupokewa hospitalini hapo alifanyiwa vipimo vyote ikiwamo ultra sound na kuambiwa itabidi alazwe asubiri wiki moja iishe kama hatojifungua kawaida, basi atafanyiwa upasuaji.

Hata hivyo, alisema Novemba 2 mwaka huu hali ilipobadilika alitoa taarifa kwa muuguzi aliyekuwa zamu, alimpima na kumjibu hasikii mapigo ya moyo ya mtoto na kumpeleka kwenye chumba cha ultra sound tena.
“Tulipofika huko yule muuguzi alimwambia mwenzake nisaidie kumpima huyu mama kwa kuwa sisikii mapigo ya mtoto na ana dalili za kujifungua. Akamjibu mnasumbua; huyu jana si alikuja hapa na nilimpima,” alisimulia Happiness.

Alidai muuguzi aliyempeleka akamwambia, “wewe mpime nataka uhakika, ndio yule muuguzi akanipima huku akisema mnasumbua. Akamuita (muuguzi) njoo usikilize si mtoto anacheza na unasikia mapigo yake. Yule (muuguzi) niliyeenda naye akaniambia nifanye mazoezi ya kutembea, nikawa nafanya hivyo, baadaye hali ikabadilika damu zikawa zinatoka mabongebonge huku nikiwa na uchungu mkali.”

Alisema alipoona hali hiyo alikwenda chumba cha kujifungulia na kumwambia muuguzi aliyekuwepo kuwa anasikia kusukuma mtoto na anatokwa damu nyingi. “Yule muuguzi alinijibu umeweka pamba usije chafua kitanda, nikamwambia ndio nimeweka pamba lakini akaniambia niache kusumbua niendelee kutembea.”

Alisema wakati anarudi wodini kwenye kitanda alichokuwa amelala alishindwa kutembea na kumlazimu kukaa chini huku akiomba msaada kwa kuwa alikuwa akisikia dalili zote za mtoto kutoka na damu ziliendelea kumtoka.
“Manesi walikuja wakaanza kuniambia sukuma huku nikiwa chini sakafuni, nilijitahidi lakini nikawa nasikia nguvu zinaniishia, mmoja wa wauguzi akawa anamwambia mwenzake pokea mtoto si unaona kichwa kile pale.

“Mwenzake akamjibu hapana huyu hasukumi napokea nini? Nikiwa nimelala pale chini wao wako kwa pembeni wananiangalia huku wakiniambia sukuma kwa zaidi ya nusu saa nikajitahidi mtoto akatoka akaanguka chini ndipo wakamnyanyua na kuniwekea kifuani huku wakiniambia niheme kwa kuwa mtoto hakulia alivyotoka ila alianguka chini sakafuni.”

“Baada ya dakika tano bado nikiwa chini sakafuni wakaenda kumuita daktari, huku wanaendelea kumkagua yule mtoto baada daktari kuja ndio akawambia wanitoe pale chini ndipo wakaniweka kitandani na kuanza kunifanyia usafi.”

Mwanamke huyo aliiomba Serikali kuwachukulia hatua wauguzi hao akidai kifo cha mwanaye ni uzembe wa wakunga na angepewa msaada wangeokoa mtoto huyo.

Mwananchi
 
Hata hivyo, alisema Novemba 2 mwaka huu hali ilipobadilika alitoa taarifa kwa muuguzi aliyekuwa zamu, alimpima na kumjibu hasikii mapigo ya moyo ya mtoto na kumpeleka kwenye chumba cha ultra sound tena.
“Tulipofika huko yule muuguzi alimwambia mwenzake nisaidie kumpima huyu mama kwa kuwa sisikii mapigo ya mtoto na ana dalili za kujifungua. Akamjibu mnasumbua; huyu jana si alikuja hapa na nilimpima,” alisimulia Happiness.


Alidai muuguzi aliyempeleka akamwambia, “wewe mpime nataka uhakika, ndio yule muuguzi akanipima huku akisema mnasumbua. Akamuita (muuguzi) njoo usikilize si mtoto anacheza na unasikia mapigo yake.

inafikirisha
Hapa kama hakueleweki fungua kesi mahakamani....
 
Ni evil spiritual au?
Yes inawezekana pia
Hawa ni zaidi ya ushetani na wengine ni kuzidiwa labda na mambo wanayoyaona kila siku hapo kama vifo na mateso wanayopitia watu

Kwa kweli ni mambo mengi yanayowapelekea kufanya haya ingawa kuna wengine ni down to earth
Wana tabia nzuri na ukarimu mwingi wa kusaidia watu

Najua nesi mmoja yeye hata akimaliza kazi anapita kusalimia wazee na wagonjwa walioko manyumbani

Ila kuna wauwaji wengi pia wanaojificha kwa mwili wa binadamu
To be honest I don't like hospitals
 
Aloo hii habari imenikumbusha wakati namsindikiza dada angu kwenda kujifungua vile tunafika kujiandikisha tu yule nesi kutuona kasonya (maana mda wake ulikuwa umekwisha anajianda kutoka ) tukajiuliza kama huduma ndo hizi tunanyaliwa na kusonywa namna hii na nesi itakuaje ?tukajipa moyo tukajiandikisha vizuri japo alijua kabisa tumeona alichokifanya..basi akawekwa chumba cha uangalizi kusubiri kuingia leba rum alikaa mle hakuna nesi alifika mpaka chupa ikapasuka akaita nesi bila msaada badae kajitokeza mmoja kaja lkn mtt alikuwa amekaribia kutoka(kichwa kinaonekana )akatembea kwa kujikaza hivo hivo hadi leba rum ilibaki kidogo mtt adondoke sakafuni..hawa manesi baadh yao hawana huruma ndo maana wanastaafu na laana za wazazi..tena kama wanawake manesi baadhi yao wanaroho mbaya mno
 
Jinsi mimba zinavyotesa jamani mtu umeteseka miezi 9 eti unampoteza mtoto wako kwa uzembe wa watu eeeh Mungu tusaidie jamani. Manesi baadhi wamekuwa na roho mbaya sana sijui kwanini ingawa wenye roho nzuri wapo.

Kama unajijua unaroho mbaya kwanini usomee sekta ya afya?? Hatua zichukuliwe kina mama wanateseka sana hasa hospitali za serikali

Sent using Jamii Forums mobile app
Wengine hata kuzipata tu hizo mimba ni kudra za mwenyezi Mungu, unaweza mtafuna mtu, manesi wengine wanakuwaga kama mawakala
 
Japo kuna uwezekano mtoto alikuwa kafa kabla hajazaliwa
Wangefanya kazi yao vizuri hata Mama mwenyewe asingekuwa na shaka nao, lakini kama wamefanya hayo hata kama ungekuwa wewe!
 
Daahh...poleni sanaa...Mimi nimeshuhudia Amana mtu akizaa chooni kabisaa miaka Ile na nesi anaitwa anajibu hakuna nesi wa chooni ukimaliza kuzaa uje huku tukuhudumie,haya mwingine akizaa pale chini akasaidiwa na wajawazito wenzio ndo wakaja...manesi wa bongo kichomi
Mimi nashukuru nikifika Cha kwanza mkono natanguliza fastaa na sichelewi leba nkifika nimezaa ndo napata treatment za kistaf balaa... maana najua Mimi ndo ntapoteza kiumbe mwisho wa siku wao hawajali hata chembe,manesi wengi ni wakala wa shetani
Sure aisee,baadhi yao ni kama wametumwa kuangamiza
 
Daahh...poleni sanaa...Mimi nimeshuhudia Amana mtu akizaa chooni kabisaa miaka Ile na nesi anaitwa anajibu hakuna nesi wa chooni ukimaliza kuzaa uje huku tukuhudumie,haya mwingine akizaa pale chini akasaidiwa na wajawazito wenzio ndo wakaja...manesi wa bongo kichomi
Mimi nashukuru nikifika Cha kwanza mkono natanguliza fastaa na sichelewi leba nkifika nimezaa ndo napata treatment za kistaf balaa... maana najua Mimi ndo ntapoteza kiumbe mwisho wa siku wao hawajali hata chembe,manesi wengi ni wakala wa shetani
Sure aisee,baadhi yao ni kama wametumwa kuangamiza
Bad experience. Dah pole na pole kwa huyo mama jamani inauma sana kukosa mtoto wakati angezaliwa vzr tuu
Mbaya sana
 
Haya mambo yapo sana kwenye vituo vya KUTOLEA huduma vya SERIKALI.. Sijui BAADHI YA WATUMISHI WA UMMAH NANI AMEWALOGA .... Ukienda kujifungua private watafanya maandalizi yote LAKINI serikalini utakuta mtu unamwambia nakaribia kusukuma LAKINI YEYE ATAKOMAA BADO AKIREJEA MUDA WAKE ALIOUKADIRIA!!!!! MBAYA ZAIDI UNAKUTA HAMA HATA CHA MAANA ANACHOKIFANYA NA WAKATI MWINGINE UNAKUTA YUKO BUSY NA SIMU..


sasa mziki unakuja mtu anataka kusukuma kweli MARA WATAANZA KUITANA NAOMBA MKASI, NAOMBA KIBANIO CHA KITOVU CHA MTOTO, MARA NAOMBA KADHAA N.K.
. Unajiuliza mtu amefika muds mrefu anakwambia anajisikia vibaya kwanini usimuhudumie???

Tanzania ina wasomi wa kutosha kwa sasa ifike wakati watu ambao hawako tayari kuwahudumia WATANZANIA watafute sehemu nyingine ya kupatia UGALI!!!! Mbona private hukuti hayo manyangamanyanga???

Dawa ni kufukuza kuanzia Mgdanga mfawidhi, katibu wa Afya, Matron, section incharge na wahusika wote!!!!!

Rudisha mtaani na kuleta watu wapya!!!

WATUMISHI wetu wa ummah wanaamini ukiipata kazi ya serikali BASI WEWE NI MFANYAKAZI WA MILELE!!!

Ndiyo maana unakutana na WATUMISHI walevi na tena we anakuwa wamelewa wakati wa KAZI na bado hakuna hatua stahiki zinachukuliwa!!!!!

Kwa utumishi huu productivity na efficiency ni ndogo sana!!! Ifike wakati huu mfumo ufanyiwe upholstery....

Leo Mashirika yetu ya UMMA kama TBA, TEMESA, WAKALA WA MELI, NDEGE n.k yanaendeshwa huku productive na efficiency zikiwa chini mno ni kwa sababu ya MFUMO MBAYA WA UTUMISHI WA UMMAH...

Watu wanapanda madaraja KWA MUDA WALIOTUMIKIA NA SIYO UFANISI, UTEUZI WA VIONGOZI NA WATENDAJI WAKUU UNAANGALIA UNAZI KWENYE CHAMA KWA KIWANGO KIKUBWA NA SIYO KUTANGULIZA UTENDAJI, Je katika mazingira HAYA TUTEGEMEE NINI?

Hapo mganga Mfawidhi atawafunika watumishi wake na STORY INAISHIA HAPO....

Mishahara iwe based on performance au kazi zote ziwe za MIKATABA renewable based on performance UONE KAMA KUNA MTU ATAZEMBEA!!!!

Serikali inafanya KAZI NZURI SANA YA KUJENGA MIUNDOMBINU NA KUAJIRI LAKINI WANAOAJIRIWA WAKISHATHIBITISHWA KAZINI BASI WANAANZA KUFANYA KAZI KWA MAZOEA....

SO SAD.......

Mpaka unajiuliza na haya nayo yanamsubiria RAIS ATOE MATAMKO??????
Uishi Maisha marefu madam
 
Japo kuna uwezekano mtoto alikuwa kafa kabla hajazaliwa
Context hapa ni uzembe wa manesi katika kumhudumia mgonjwa.

Wangewajibika ipasavyo pasingelikuwa na lawama, maana hayo mengine ni matokeo ya kawaida kwa wajawazito wakati wa kujifungua "labor".
 
Hivi habari kama hii Mtu kama Rais au Waziri Mkuu hawaioni, au ni habari ndogo sana kwao?
Hawajui Manesi kama hawa wamesababisha vifo vya watoto wangapi!?

Kwa habari kama hii ndo nnapomkumbuka Magufuri, japo sikuwahi kukubaliana nae kwa baadhi ya mambo lakini ikija habari ya mwananchi Masikini kunyanyasika, alikubari kusemwa kuwa hafati utawala wa sheria.
Waziri ataingilia ikiwa tu panampunga mwingi au kuna mtu amelengwa kukatwa kichwa
 
Hai. Mkazi wa Wilaya ya Hai, Happiness Massawe (39), amegoma kuchukua mwili wa kichanga hospitalini kwa wiki moja akidai kifo cha mtoto wake kimetokana na uzembe wa baadhi ya wauguzi.

Happiness, aliyejifungua katika Hospitali ya Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro alisema Oktoba 31 mwaka huu alipohisi dalili za uchungu alikwenda hospitalini hapo kwa ajili ya kujifungua na alipofika alipokewa na wauguzi.
Hata hivyo, alisema alipopata uchungu hakupewa ushirikiano badala yake alijifungulia sakafuni.

Juzi, Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Hai, Itikija Msuya alithibitisha kuwapo kwa tukio hilo akisema ameunda kamati ya kuchunguza ili kubaini kilichotokea siku hiyo.

“Kwa taarifa nilizopewa mtoto alizaliwa zero beating (akiwa amekufa) japo kuna dalili za uzembe ulifanywa na watoa huduma. Nimeunda kamati kuchunguza na watakaobainika hatua za kisheria zitachukuliwa,” alisema Dk Msuya.

Akizungumzia hali ilivyokuwa, Happiness alisema baada ya kupokewa hospitalini hapo alifanyiwa vipimo vyote ikiwamo ultra sound na kuambiwa itabidi alazwe asubiri wiki moja iishe kama hatojifungua kawaida, basi atafanyiwa upasuaji.

Hata hivyo, alisema Novemba 2 mwaka huu hali ilipobadilika alitoa taarifa kwa muuguzi aliyekuwa zamu, alimpima na kumjibu hasikii mapigo ya moyo ya mtoto na kumpeleka kwenye chumba cha ultra sound tena.
“Tulipofika huko yule muuguzi alimwambia mwenzake nisaidie kumpima huyu mama kwa kuwa sisikii mapigo ya mtoto na ana dalili za kujifungua. Akamjibu mnasumbua; huyu jana si alikuja hapa na nilimpima,” alisimulia Happiness.

Alidai muuguzi aliyempeleka akamwambia, “wewe mpime nataka uhakika, ndio yule muuguzi akanipima huku akisema mnasumbua. Akamuita (muuguzi) njoo usikilize si mtoto anacheza na unasikia mapigo yake. Yule (muuguzi) niliyeenda naye akaniambia nifanye mazoezi ya kutembea, nikawa nafanya hivyo, baadaye hali ikabadilika damu zikawa zinatoka mabongebonge huku nikiwa na uchungu mkali.”

Alisema alipoona hali hiyo alikwenda chumba cha kujifungulia na kumwambia muuguzi aliyekuwepo kuwa anasikia kusukuma mtoto na anatokwa damu nyingi. “Yule muuguzi alinijibu umeweka pamba usije chafua kitanda, nikamwambia ndio nimeweka pamba lakini akaniambia niache kusumbua niendelee kutembea.”

Alisema wakati anarudi wodini kwenye kitanda alichokuwa amelala alishindwa kutembea na kumlazimu kukaa chini huku akiomba msaada kwa kuwa alikuwa akisikia dalili zote za mtoto kutoka na damu ziliendelea kumtoka.
“Manesi walikuja wakaanza kuniambia sukuma huku nikiwa chini sakafuni, nilijitahidi lakini nikawa nasikia nguvu zinaniishia, mmoja wa wauguzi akawa anamwambia mwenzake pokea mtoto si unaona kichwa kile pale.

“Mwenzake akamjibu hapana huyu hasukumi napokea nini? Nikiwa nimelala pale chini wao wako kwa pembeni wananiangalia huku wakiniambia sukuma kwa zaidi ya nusu saa nikajitahidi mtoto akatoka akaanguka chini ndipo wakamnyanyua na kuniwekea kifuani huku wakiniambia niheme kwa kuwa mtoto hakulia alivyotoka ila alianguka chini sakafuni.”

“Baada ya dakika tano bado nikiwa chini sakafuni wakaenda kumuita daktari, huku wanaendelea kumkagua yule mtoto baada daktari kuja ndio akawambia wanitoe pale chini ndipo wakaniweka kitandani na kuanza kunifanyia usafi.”

Mwanamke huyo aliiomba Serikali kuwachukulia hatua wauguzi hao akidai kifo cha mwanaye ni uzembe wa wakunga na angepewa msaada wangeokoa mtoto huyo.

Mwananchi
hata kama sikuwepo eneo la tukio na simjui huyu dada na ao wauguzi ila nasema hivi " HUYO DADA NDO MSEMA KWELI NA IKO KITU KAFANYIWA KWELI"
 
Back
Top Bottom