nimeona hapo kwenye model SM-G928T, siku nyingne ukiona samsung yyt inayoishia na herufi tofauti na F/DS mf SM-G928F/DS au haina heruf nyuma ni namba tu kimbia, mf SM-G9280, ujue unauziwa unlocked na mtumba iliyotumika kwa angalau 2 yrs, na shida yake kubwa inakua kwenye network, unaweza usigundue kama upo sehem yenye network nzur , ila ukienda sehem yenye shda kdg tu ya network yako itasumbua ila nyingne zitapga kazi,
kwa ufup ni zile simu ambazo kwa huku bongo tunasema zimeflashiwa, au kwa lungha nyingne ni kama zile simu zinazouzwa kwa promotions na tigo ambapo lain lazima iwe ya tigo/inasoma tigo tu, sasa ili utumie lain za mitandao yote unaenda kwa wajanja wanaiflash,
kimbembe cha ku flash simu najua weng tunakifaham,
Hivyo epuka simu zinazmishia na heruf kama T, V, AT&T n.k hizo herufi ni majina ya zile kampuni za simu zilizoingia ubia na samsung: T- for T-mobile, V- for Verizon, AT&T- for american telephone and telegram.
pili epuka samsung yoyote ambayo imeandikwa jina kwa nyuma chini mf galaxy s6+ tofaut na neno samsung kwa nyuma juu, inatakiwa juu kue na neno samsung, chini kue na info za simu kwa maandisi madogo mf model(na hapa ndio unatakiwa ujue ile model kama ni hayo ma T, au F/DS) imei n.k au kama ni lain mbili watakuandikia neno DUOS juu ya hayo maandish madogo, kwaio ukiona tofaut na hvyo kimbia, na pia kama hakujaandikwa chochote kbsa pia anza kutumia akili yako vzr.
Mara nying refubs ndio zinakua na haya mapicha picha.