Wawekezaji baada ya kutengeneza faida lukuki wameamua kutufilisi kwa kufungua kesi huko Mahakama za kimataifa. Wanasheria wetu wanafanya nini?

Wawekezaji baada ya kutengeneza faida lukuki wameamua kutufilisi kwa kufungua kesi huko Mahakama za kimataifa. Wanasheria wetu wanafanya nini?

Pamoja na hasara kubwa tuliyopata kwenye mikataba ya madini na rasilimali nyingine ikiwemo gesi hali ya kuifilisi Tanzania inayoendelea huko mahakama za kimataifa inatia kinyaa

Kinachoendelea sasa hivi; mwekezaji akigombezwa kidogo tu na serikali anakwenda kufungua kesi nje. Akifungua kesi Tanzania tunaajiri mawakili wa kigeni kututetea wakishirikiana na mawakili wachache wa Tanzania.

Pamoja na kuajiri wageni hao kututetea kesi asilimia kubwa tunashindwa na kutakiwa kulipa fidia. Hakuna mtu anayekubali kesi tunazo shindwa zifahamike kwa watanzania zote ni siri hadi ziwe published huko nje.

1. Kama hatuna wanasheria wazawa wakututea tunaposhtakiwa kwa kukiuka masharti ya mikataba, tumepata wapi wanasheria wakiingia mikataba?

2. Tutaendelea kushtakiwa na kulipa fidia hadi lini?

3. Haiwezekani fedha nyingi zinazotokana na mkataba kama wa bandari zikatumika kulipa madeni tunayodaiwa kwa kuvunja mkataba?

4. Kama ndivyo, ni lini kama Taifa tutaamua kusubiri tuandae watu wakutusaidia kuingia mkataba na pia kutetea mikataba yetu hasa ya rasilimali zetu?

Pia soma: - Tanzania yashindwa kwenye kesi, yaamuriwa kulipa fidia ya zaidi ya Tsh. Bilioni 260
Suluhisho ni hili walilokuja nalo wanasheria kwenye huu mkataba wa DPW, kwanza wameanzia bungeni ili kupata ulinzi wa kikatiba.

Pili wameweka kifungu namba 20 ambacho kinasema iwapo patatokea kutoelewana mbele ya safari tatizo litaanza kutatuliwa kwa kutumia amicable settlement na ikishindikana itaundwa kama ndogo ya IGA negotiation committe ili kutatua tatizo husika.

JPM alitanguliza akili ya kugombana na hawa wawekezaji na kuamua kuvunja mkataba moja kwa moja, hakujali hasara ambayo ilitusubiri mbele ya safari, na ndio hii imefika sasa.

Lipo somo la kujifunza upande wa wanasiasa, kuheshimu mikataba bila ya kutanguliza akili za kuburuza pande zote mbili zinazokubaliana kwenye kuingia makubaliano.
 
Back
Top Bottom