Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 76,107
- 160,001
Polisi wa Uganda wamemkamata Mwanaume mmoja Barabara ya Kampala baada ya kukutwa akiichapa viboko sanamu akidai sanamu hiyo inafanana na Mtu ambae amehusika kuvuruga Uchaguzi wa Uganda na anastahili adhabu kwa makosa aliyoyafanya.
Polisi nchini Uganda Jumatatu waliwakamata wanaume wawili ambao walichapa viboko picha ya Rais Yoweri Museveni kwenye barabara yenye shughuli nyingi katika mji mkuu, Kampala.
Wawili hao, Luta Ferdinand Male na Nsereko Asharf, walijitambulisha kwa polisi kuwa wao ni wanaharakati. Walimshtaki rais kwa udanganyifu katika uchaguzi wa tarehe 14 mwezi Januari, ingawa Bwana Museveni hapo awali alikanusha madai hayo.
Msemaji wa polisi jijini Kampala Patrick Onyango amethibitisha kukamatwa kwa watu hao. Watakabiliwa na mashtaka ya kusababisha kero kwa Umma.
Gazeti la Daily Monitor lilichapisha picha za kukamatwa kwa watu hao kwenye mtandao wa Twitter:
Uchaguzi mkuu uliokuwa na ushindani mkubwa nchini Uganda ulimfanya Rais Museveni kutawala kwa muhula mwingine Mpinzani wake wa karibu, mwanamuziki aliyegeuka-mwanasiasa Bobi Wine, anapinga matokeo ya uchaguzi mahakamani.
Wiki iliyopita, bunge la Umoja wa Ulaya lilitaka vikwazo dhidi ya watu binafsi na mashirika yaliyohusika na ukiukaji wa haki za binadamu wakati wa uchaguzi - ambayo walisema hayakuwa ya kidemokrasia na hayakuwa na uwazi
Polisi nchini Uganda Jumatatu waliwakamata wanaume wawili ambao walichapa viboko picha ya Rais Yoweri Museveni kwenye barabara yenye shughuli nyingi katika mji mkuu, Kampala.
Wawili hao, Luta Ferdinand Male na Nsereko Asharf, walijitambulisha kwa polisi kuwa wao ni wanaharakati. Walimshtaki rais kwa udanganyifu katika uchaguzi wa tarehe 14 mwezi Januari, ingawa Bwana Museveni hapo awali alikanusha madai hayo.
Msemaji wa polisi jijini Kampala Patrick Onyango amethibitisha kukamatwa kwa watu hao. Watakabiliwa na mashtaka ya kusababisha kero kwa Umma.
Gazeti la Daily Monitor lilichapisha picha za kukamatwa kwa watu hao kwenye mtandao wa Twitter:
Uchaguzi mkuu uliokuwa na ushindani mkubwa nchini Uganda ulimfanya Rais Museveni kutawala kwa muhula mwingine Mpinzani wake wa karibu, mwanamuziki aliyegeuka-mwanasiasa Bobi Wine, anapinga matokeo ya uchaguzi mahakamani.
Wiki iliyopita, bunge la Umoja wa Ulaya lilitaka vikwazo dhidi ya watu binafsi na mashirika yaliyohusika na ukiukaji wa haki za binadamu wakati wa uchaguzi - ambayo walisema hayakuwa ya kidemokrasia na hayakuwa na uwazi