Wayahudi wanavyojipenyeza wizara za elimu duniani kufuta kutajwa vibaya

Wayahudi wanavyojipenyeza wizara za elimu duniani kufuta kutajwa vibaya

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Saudi Arabia imechapisha upya vitabu vyote vya shule za nchi hiyo na kuondoa vipengele vilivyokuwa vikiwataja kwa ubaya Wayahudi pamoja na Wakristo. Baadhi ya vipengele hivyo ni kama vile utabiri wa kuzuka vita hapo baadae ambapo waislamu watawapiga vibaya mayahudi na kuwashinda. Kipengele kingine ni kuwa mayahudi ni maadui wa dini ya uislamu.

Vitabu vya awali pia vinawataja Wayahudi na Wakristo kuwa ni makafiri na kwamba matendo yao mema yote yataishia hapa duniani na kwamba huko akhera wataingia moto wa jahanamu milele.

Mbali na hayo ambayo ni mahasusi kwa mayahudi na wakristo, vitabu hivyo vipya vimekwenda mbali kwa kufuta adhabu ya mashoga na wachawi kuwa ni kuuliwa.

Mafanikio hayo yamekuja kufuatia juhudi za muda mrefu na za kichinichini za taasisi ya kiyahudi iitwayo IMPACT SE ambayo ni maalumu kwa kufuatilia mitaala ya nchi mbali mbali duniani hasa za kiislamu kuhakikisha kuwa maandishi yanayowataja vibaya mayahudi yanafutwa.

Pamoja na kwamba juhudi hizo ni za muda mrefu lakini zimetajwa kupata nguvu zaidi wakati wa uraisi wa Donald Trump wa Marekani na hasa baada ya kuchukua madaraka kwa mtoto wa mfalme Mohammed bin Suleiman wa Saudi Arabia.

Kwa mujibu wa mmoja wa viongozi wa taasisi hiyo Marcus Sheff , mafanikio hayo si makubwa sana lakini kwa ujumla yanakwenda kwenye mstari na malengo yao.

Katika mkakati wa kupima mafanikio ya kazi zao taasisi hiyo inatambua kuwa takriban thuluthi mbili ya idadi ya wananchi wa Saudi Arabia wana umri ulio chini ya miaka 30 na kwamba bado viongozi wengi wa juu wa nchi hiyo na wanazuoni wa nchi hiyo wamekuwa ni kikwazo kutokana na misimamo yao ya kulinda dini na tamaduni zao.

Vitabu vinavyochapwa na wizara ya elimu vya nchi hiyo vinatumika na mashule takriban 30,000 yaliyo ndani ya nchi hiyo na nje ya nchi.

1608896782318.png
 
Wakiweza kupenya kwenye education system ya Iran itakua vizuri zaidi.
 
Saudi Arabia imechapicha upya vitabu vyote vya shule za nchi hiyo na kuondoa vipengele vilivyokuwa vikiwataja kwa ubaya mayahudi pamoja na wakristo .Baadhi ya vipengele hivyo ni kama vile utabiri wa kuzuka vita hapo baadae ambapo waislamu watawapiga vibaya mayahudi na kuwashinda.Kipengele kingine ni kuwa mayahudi ni maadui wa dini ya uislamu.
Vitabu vya awali pia vinawataja mayahudi na wakristo kuwa ni makafiri na kwamba matendo yao mema yote yataishia hapa duniani na kwamba huko akhera wataingia moto wa jahanamu milele.
Mbali na hayo ambayo ni mahasusi kwa mayahudi na wakristo,vitabu hivyo vipya vimekwenda mbali kwa kufuta adhabu ya mashoga na wachawi kuwa ni kuuliwa.
Mafanikio hayo yamekuja kufuatia juhudi za muda mrefu na za kichinichini za taasisi ya kiyahudi iitwayo IMPACT SE ambayo ni maalumu kwa kufuatilia mitaala ya nchi mbali mbali duniani hasa za kiislamu kuhakikisha kuwa maandishi yanayowataja vibaya mayahudi yanafutwa. Pamoja na kwamba juhudi hizo ni za muda mrefu lakini zimetajwa kupata nguvu zaidi wakati wa uraisi wa Donald Trump wa Marekani na hasa baada ya kuchukua madaraka kwa mtoto wa mfalme Mohammed bin Suleiman wa Saudi Arabia
Kwa mujibu wa mmoja wa viongozi wa taasisi hiyo Marcus Sheff ,mafanikio hayo si makubwa sana lakini kwa ujumla yanakwenda kwenye mstari na malengo yao.
Katika mkakati wa kupima mafanikio ya kazi zao taasisi hiyo inatambua kuwa takriban thuluthi mbili ya idadi ya wananchi wa Saudi Arabia wana umri ulio chini ya miaka 30 na kwamba bado viongozi wengi wa juu wa nchi hiyo na wanazuoni wa nchi hiyo wamekuwa ni kikwazo kutokana na misimamo yao ya kulinda dini na tamaduni zao.
Vitabu vinavyochapwa na wizara ya elimu vya nchi hiyo vinatumika na mashule takriban 30,000 yaliyo ndani ya nchi hiyo na nje ya nchi.
View attachment 1658917
Ulipaswa kutoa pongezi kwa kazi nzuri ya hilo shirika la Israel kama kweli ndio wahusika. Badala ya kufundisha watoto mambo ya maana unawafundisha kuhusu chuki za kidini. Mafundisho haya potofu ndio kitovu cha ugaidi.

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
 
Ulipaswa kutoa pongezi kwa kazi nzuri ya hilo shirika la Israel kama kweli ndio wahusika. Badala ya kufundisha watoto mambo ya maana unawafundisha kuhusu chuki za kidini. Mafundisho haya potofu ndio kitovu cha ugaidi.

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
Wayahudi ni watu wa njama daima na kupokea tu,hakuna wanachotoa.Wanapenda watajwe vyema lakini wanatenda uovu. Wanataka uhusiano mzuri na ndugu wa Wapalestina na wakati huo huo wanawakandamiza na kuwavunjia majumba yao bila haya.
 
Ndondocha katika ubora wake..

Yaani madini haya[emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Usipoyaelewa vzr ya anaweza kukufanya upigane vita na ndugu zake kisa kuyatetea.

Nilikuwa nigeria kipindi flani eti msikiti wanapanga njama kuwapiga wakristo eti na kanisani wanapanga njama kuwapiga waislamu..

Unasema majitu haya si bora yawe mapagani kuwe na amani tu maana hizo dini hata kuzielewa wameshindwa[emoji30][emoji30][emoji30]
 
Qur'an imeandika hivyo.

So hao wanakaririshwa hivyo.


Hivi mtu akisema

Wakristo..

Na akisema Mikristo utaelewa nini? .

Hakuna sehem qurain imekaririsha jambo hilo.

Wanapotajwa kwa ubaya ndy huitwa mayahudi.
Miyahudi.

Wakitajwa kwa wema huitwa ,
--wayahudi.
--Myahudi.

Mfano

--Mwizi.
--Majizi.
--Mijizi.

Yote ktk kutaja jambo kwa ubaya.
 
Saudi Arabia imechapicha upya vitabu vyote vya shule za nchi hiyo na kuondoa vipengele vilivyokuwa vikiwataja kwa ubaya mayahudi pamoja na wakristo .Baadhi ya vipengele hivyo ni kama vile utabiri wa kuzuka vita hapo baadae ambapo waislamu watawapiga vibaya mayahudi na kuwashinda.Kipengele kingine ni kuwa mayahudi ni maadui wa dini ya uislamu.
Vitabu vya awali pia vinawataja mayahudi na wakristo kuwa ni makafiri na kwamba matendo yao mema yote yataishia hapa duniani na kwamba huko akhera wataingia moto wa jahanamu milele.
Mbali na hayo ambayo ni mahasusi kwa mayahudi na wakristo,vitabu hivyo vipya vimekwenda mbali kwa kufuta adhabu ya mashoga na wachawi kuwa ni kuuliwa.
Mafanikio hayo yamekuja kufuatia juhudi za muda mrefu na za kichinichini za taasisi ya kiyahudi iitwayo IMPACT SE ambayo ni maalumu kwa kufuatilia mitaala ya nchi mbali mbali duniani hasa za kiislamu kuhakikisha kuwa maandishi yanayowataja vibaya mayahudi yanafutwa. Pamoja na kwamba juhudi hizo ni za muda mrefu lakini zimetajwa kupata nguvu zaidi wakati wa uraisi wa Donald Trump wa Marekani na hasa baada ya kuchukua madaraka kwa mtoto wa mfalme Mohammed bin Suleiman wa Saudi Arabia
Kwa mujibu wa mmoja wa viongozi wa taasisi hiyo Marcus Sheff ,mafanikio hayo si makubwa sana lakini kwa ujumla yanakwenda kwenye mstari na malengo yao.
Katika mkakati wa kupima mafanikio ya kazi zao taasisi hiyo inatambua kuwa takriban thuluthi mbili ya idadi ya wananchi wa Saudi Arabia wana umri ulio chini ya miaka 30 na kwamba bado viongozi wengi wa juu wa nchi hiyo na wanazuoni wa nchi hiyo wamekuwa ni kikwazo kutokana na misimamo yao ya kulinda dini na tamaduni zao.
Vitabu vinavyochapwa na wizara ya elimu vya nchi hiyo vinatumika na mashule takriban 30,000 yaliyo ndani ya nchi hiyo na nje ya nchi.
View attachment 1658917
Huyo jamaa kamuua Kashoggi kikatili sana.

Kama ana dini, basi dini yake haifaiiii.

Dino ya kweli dunia hii ni UTU na UBINADAMU tu.
 
Hivi mtu akisema

Wakristo..

Na akisema Mikristo utaelewa nini? .

Hakuna sehem qurain imekaririsha jambo hilo.

Wanapotajwa kwa ubaya ndy huitwa mayahudi.
Miyahudi.

Wakitajwa kwa wema huitwa ,
--wayahudi.
--Myahudi.

Mfano

--Mwizi.
--Majizi.
--Mijizi.

Yote ktk kutaja jambo kwa ubaya.
Asante sana kwa ufafanuzi...heb ajiulize badala ya kusema "Waislamu" tungesema "Miislamu" au "Maislamu"ingekuwaje? C ugomvi huo?
 
Asante sana kwa ufafanuzi...heb ajiulize badala ya kusema "Waislamu" tungesema "Miislamu" au "Maislamu"ingekuwaje? C ugomvi huo?
Hakuna ugomvi wowote kwenye kukazia jambo..

Mbona haukuwa ugomvi inapohusishwa kwa kutajwa na kuilisha maneno Qur'an kwenye mada za kipuuzi.
 
Back
Top Bottom