Wengi wetu hawajui historia ya Tz kuwakumbusha machungu na makovu ambayo Wazanzibar wamesababishiwa na muungano huu wa kiinimacho ambao unachezewa na warasimu wanapoweza kutaka kufanya hivyo katikati ya kiapo cha taasisi ya jeshi iliyoapa kuulinda muungano wenyewe.
Katika awamu hii, muungano umejeruhiwa kwa kusababishiwa majeraha mengi yatokanayo na utendaji dhalimu wa warasimu ambao ndiyo wana dhamana ya kuulinda na hivyo hatuoni sababu ya kuwaenzi waasisi wake kinafiki.
Kumbe kiapo cha jeshi letu hodari na mahiri; cha kulinda muungano kinaweza kumaanisha kulinda wahujumu muungano!
Wakati Watanganyika wanalazimisha mtazamo wao kuwa muungano unawafaidisha Wazanzibar zaidi ya wao, hawana budi kujifunza kujuwa madhila ya muungano kwa Wazanzibar pia ambayo nadhani ni makubwa kuliko faida ambazo Wazanzibar wamewahikupewa na huu muungano. Hakika Wazanzibar ni wavumilivu kuliko Watanganyika.
Yafuatayo ni madhila makubwa ya muungano kwa Wazanzibar:-
1. Muungano huu umeweza kuwapora Wazanzibar haki yao ya kuwa na kiongozi wao waliyemchaguwa wenyewe kwa kura. Hii imehujumu dhana nzima ya demokrasia. Rais wa Zanzibar Sheikh Aboud Jumbe Mwinyi alichukuwa hatamu katika mazingira yanayofanana na ya rais SSH (vifo vya marais) Aprili 7, 1972 hadi Januari 30, 1984 alipopokelewa kijiti na rais Ali Hassan Mwinyi. Mwl. Nyerere kupitia muungano wake huu aliouasisi alidiriki kumvua rais Jumbe urais wake na kumpandikiza rais Ali Hassan Mwinyi. Mwl alimng'oa rais wa kile alichokiita na kukiamini kuwa ni nchi (siyo mkoa) Zanzibar. Rais Jumbe alikuja baada ya 1972 kuchaguliwa kwenye chaguzi zilizofuata kidemokrasia. Kumvua na kumuweka kizuizini rais wa watu huru na nchi huru ni kufedhehesha, kutweza, kubeza na kuhujumu haki za Wazanzibar, uhuru wao, taifa lao na serikali yao. Rais wa Watanganyika angeng'olewa kwa staili hii na rais wa Zanzibar sijui ingekuwaje? Wazanzibar ni wavumilivu wa madhila ya muungano kwao.
2. Muungano huu umeweza kuwapora Wazanzibar Makamu wao wa rais Abdullah Kassim Hanga aliyewahi pia kuwa Naibu Katibu Mkuu wa ASP na Waziri Mkuu kwa miezi 3. Huu ni muungano pekee duniani ambao umeweza kushuhudia Tz ikiandika historia ya ajabu kwenye sayari ya Makamu wa Rais kupotezwa na watu wasiojulikana kwa miaka 54 sasa tangu 1969 kwa tuhuma (ambayo haikufikishwa kortini ya kula njama kumpindua rais Karume). Hakuna kaburi lake, hakuna cheti cha kifo chake kwa Kabidhi Wasii Mkuu wa serikali wala hakuna kumbukumbu ya RB Polisi. Hata walinzi wake hawakujuwa alipotokea baada ya kuwasili kwenye makazi yake rasmi. Makamu wa Rais wa Watanganyika angepotea kwa staili hii chini ya rais wa muungano toka Znz sijui ingekuwaje? Wazanzibar ni wavumilivu wa madhila ya muungano kwao.
Sent from my SM-A260F using
JamiiForums mobile app