Wazanzibari waliumbua Bunge! Taasisi 7 zilinyimwa fursa kutoa maoni katika rasimu ya katiba!

Wazanzibari waliumbua Bunge! Taasisi 7 zilinyimwa fursa kutoa maoni katika rasimu ya katiba!

Maige
alishambulia Bunge

Wakati
wabunge wa CCM wakiwashambulia wenzao wa kambi rasmi ya upinzani
waliosusia muswada huo, Mbunge wa Msalala, Ezekil Maige (CCM),
amelishambulia Bunge, hususan kiti cha Spika kwa kushindwa kutumia
busara kuepusha vurugu bungeni.


Katika taarifa yake aliyoitoa kupitia mtandao wa Kijamii wa Wanabidii,
Maige ambaye amepata kuwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, alisema
kuwa alitazama kwa mshangao na kutoamini kuhusu kilichojiri bungeni
juzi.


Alisema kwa bahati mbaya hakuwepo Dodoma siku hiyo kwani alikuwa mjini
Arusha kikazi, lakini hakuona sababu kabisa ya kufikia hapo kwani hali
hiyo ingeweza kuepushwa na kiti cha
Spika.

“Ingewezekana
kabisa kuahirisha muswada na kutoa nafasi kwa Kamati ya Katiba na
Sheria kwenda Zanzibar kupata maoni ya wenzetu wa
huko.

“Najua
kuna maelezo mazuri ya kushirikishwa kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Lakini kikanuni, Baada ya Muswada kusomwa mara ya kwanza, unakuwa
mikononi mwa Bunge na kamati ndiyo inayokusanya maoni si serikali,”
alisema Maige.


Maige ambaye anakuwa mbunge wa kwanza wa CCM kukosoa kiti cha Spika,
alisema kwa kuwa hakuna ushahidi wa ‘public hearing’ kufanyika Zanzibar
na kuwasikia Wazanzibari wa kawaida (nje ya serikali), basi kulikuwa na
hoja kabisa ya kurekebisha kasoro hiyo kwa kutoa nafasi kwa kamati
kwenda Zanzibar.

“Suala
la Katiba ni kubwa hivyo ni vema zikafanyika jitihada za kutosha
kuhakikisha tunakwenda pamoja (na wenzetu hasa wenye mtazamo tofauti na
sisi) badala ya kutumia wingi wetu kwani mwisho wa safari tukienda hivi
wapo watakaodai Katiba Mpya si yao, hivyo kuikosesha ‘social
legitimacy’,” alisema.


Kwa mujibu wa Maige, hatua ya Ndugai kutomsikiliza Kiongozi Mkuu wa
Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, nako kulitibua mambo bila
sababu.

“Mbowe
angepewa nafasi ya kusikilizwa, hata kama hoja yake isipokubaliwa
ingekuwa nafuu sana na shari na aibu ya jana
ingeepukika.

“Tumesameheana,
lakini tujifunze na tujitahidi sana kwenda kwa maelewano,” alisema
Maige katika taarifa hiyo.

CC
chama

hana lolote maige. anaonesha hasira za kuvuliwa Urais. fisadi mkubwa huyu
 
maadam wamekiri kuwa serikali ya umoja wa kitaifa zanzibar imeshirikishwa, tunaamini kuwa zanzibar imeshirikishwa. jukumu la kutunga sheria ni la Bunge na wengine hushirikishwa pale inapoona inafaa hususan wadau muhimu

Serikali ndiyo inayoleta mswada bungeni, serikali haipipitishi mswada kuwa sheria bali wahusika katika mswada huo hushirikishwa kutoa maoni yao na hayo maoni ndiyo ya wadau wahusuka hupelekwa bungeni.

Kwamba serikali ya Mapinduzi Zanzibar ilipokea mswada huo na kuupa baraka za kufikishwa bungeni ni ubakaji wa sheria kwa sababu serikali hupeleka mswada bungeni na ni bunge ndilo linalofanyia kazi mswada si serikali.

Hapa
Lizabon unacheza lizombe tu ndugu yangu.
 
maadam wamekiri kuwa serikali ya umoja wa kitaifa zanzibar imeshirikishwa, tunaamini kuwa zanzibar imeshirikishwa. jukumu la kutunga sheria ni la Bunge na wengine hushirikishwa pale inapoona inafaa hususan wadau muhimu

kwani katiba ni ya serikali..
 
maadam wamekiri kuwa serikali ya umoja wa kitaifa zanzibar imeshirikishwa, tunaamini kuwa zanzibar imeshirikishwa. jukumu la kutunga sheria ni la Bunge na wengine hushirikishwa pale inapoona inafaa hususan wadau muhimu
Acha ujinga ushakua mtu mzima.,Serikali kushirikishwa inahusiana nini na KATIBA???Katiba ni ya wananchi wewe unaleta habari zako za kilukuvilukuvi hapa Jf.Nyoo.
 
Hiki ndo akina Hamisi Andrew Kigwangallah wamemtukania mh. Mbowe
 
Lizaboni unajua mchakato sheria inapopita kabla ya kuingia bungeni?
 
Last edited by a moderator:
kwani katiba ni ya serikali..

Tatizo watu wanajibu kimipasho badala ya kikanuni. Serikali hupeleka mswada bungeni, msawa wa sheria ukishakuwa mikononi mwa bunge serikali haina haki nao, hivyo basi bunge ndilo linalofanyia kazi mswada huo kuwafikia wadau au taasisi husika kupata maoni yao kabla ya kufikia hatua ya kupigia kura.

Kilichofanywa na serikali ya Mapinduzi kuridhia mswada huo na kuupeleka bungeni kama alivyosema Makamu wa Pili wa Rais wa serikali ya Mapinduzi Zanzibar ni ubakaji wa sheria na katiba kwa sababu ni bunge ndilo lilitakiwa kuufikisha kwa watoa maoni husika na wala si serikali.

Hapa tatizo ni kwamba Kamati ya Bunge ya sheria iko chini ya wabunge wa CCM na ndio walio na wajumbe wengi katika kamati hiyo, kwa vyo vyote kuipindisha kwa malengo yao ni rahisi zaidi kwa vile ndio wanaokalia na kuyatunza yale ma-folders.
 
Kauli ya Dk. Slaa
Naye Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa, alisema walichofanya wabunge wa CCM kupitisha muswada huo juzi ni kielelezo kuwa Katiba inayoandaliwa ni mali ya CCM, kwani inatengenezwa kwa maoni ya CCM.

Akizungumza na gazeti hili jana, Dk. Slaa alisema kuna upotoshaji unaofanywa na viongozi wa Bunge kwa kushirikiana na serikali katika hoja ya ushiriki wa Wazanzibari.


Dk. Slaa aliwashangaa wabunge wa CCM kwa kushindwa kujadili jambo zito lililokuwa mbele yao na badala yake wakaishia kuwashambulia wabunge wa CHADEMA na CUF.


Alisema anaamini kuwa hali hiyo ina msukumo kutoka nje ya Bunge, na akatahadharisha juu ya mhimili mmoja kuingilia uamuzi wa muhimili mwingine. Alisema hali hii itawafanya Watanzania wasipate Katiba waliyoitarajia.


Alisema madhara ya hali hiyo yamejionesha katika sura mbili kwa wabunge kuonesha ushabiki wa kichama zaidi badala ya kupigania masilahi ya taifa.

“Lissu alisema Wazanzibari hawajashirikishwa, sasa hawa wanakuja na barua ya serikali. Tunafahamu walipata maoni ya baadhi ya viongozi wa serikali wanaotokana na CCM lakini hawajawafikia Wazanzibari wengi wa kawaida,” alisema Dk. Slaa.

Kutokana na hali hiyo, alisema wananchi wameshaanza kuchanganyikiwa juu ya dhamira ya serikali katika kuheshimu maoni ya wananchi kupitia rasimu ya Katiba iliyoandaliwa na Jaji Joseph Warioba.


Akizungumzia udhalilishaji aliofanyiwa Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, Dk. Slaa alisema Tanzania inafuata kanuni za mabunge ya Jumuiya ya Madola ambayo nafasi ya kiongozi wa upinzani bungeni ni sawa na waziri mkuu kwa upande wa serikali.

“Kwa maana hiyo, anaposimama Kiongozi wa Upinzani bungeni au Waziri Mkuu lazima jicho la anayeongoza kiti cha Spika limtupie jicho kwa kuwa ni lazima atakuwa na hoja ya kusikilizwa.
“Nilishasema katika hili Ndugai alikuwa hatumii akili yake alikuwa anaongozwa kutoka nje ya Bunge na hili Watanzania wanapaswa watambue mabavu yaliyotumika ni kielelezo cha wazi cha ukosefu wa demokrasia nchini,” alisema Dk. Slaa.

Alisema waliopitisha rasimu hiyo wameua matumaini ya Watanzania na sasa ni jukumu la wananchi kuamua hatima ya nchi yao.


Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Zanzibar Hamad Masoud, alisema hawana taarifa yoyote ya wananchi kushirikishwa katika muswada huo wa mabadiliko ya sheria ya Katiba.


Alisema hali hiyo inadhihirisha nia mbaya ya serikali katika kutatua matatizo ya wananchi kupitia Katiba huku akilaumu uamuzi wa kamati kufanya mambo yake kwa siri.
 
Pindi Chana .....anasema wameshirikishwa JAHAZI ASILI....kwa niaba ya wa zanzibar ....na eti moani ya CUF yapo kwenye serekali kwa maana serekali ni ya mseto .....duuuuuuu

JAHAZI ASILIA ni chama kama vyama vingine na ilisajiliwa dar es salaam baada ya kupata saini za bara na zanzibar. So haiwakilishi wazanzibar tu. mia
 
hii nchi itakuja tujutie ikingia kwenye machafuko, hili ndio tatizo kuwa na viongozi waliotokana na mbio za mwenge ni aibu ilioje, imefika hatua hata hawajijui kama wao ndio viongozi na kutakiwa kuwa dira ya maendeleo na kuwaheshimu wananchi kama wao tunavowaita waheshimiwa, ccm hata katiba mnaichakachua hivi tunanchi kweli na viongozi wanaweza fanya upuuzi kama huu, huu ni uhuni na inadhihirisha wazi jinsi wasivojali katika kuweka maslahi yao mbele tena katika chombo cha sharia kama bunge na wananchi wakiona live, then wakiwa na imani kuwa bado wa Tz ni wajinga na wao watabaki madarakani milele. kuna matumaini tena ya hii katiba au ndo bora liende tu. kama raia nashauri wananchi wezangu ccm haitufai ni bora ufe ukitetea nchi yako kuliko kuishi chini ya ccm aibuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu
 
Mbunge gani wa ccm mwenye busara?hivi wasira yupogo?lukuvi pinda komba mwigulu mama yangu,naunga hoja %ila naomba mniletee maji jimbon kwangu jamani hakuna hata nguzo ya umeme watu wanakunywa maji na fisi huku singida na yanafanana na maziwa kabisa foleni inaanza sa kumi za usiku mpaka fisi waondoke ndo tuchote maji mh spika naunga hoja mkono %
 
haya sasa......

Mkuu samahani,out of topic kidogo.
Hivi hujafikiria kubadilisha ID yako baada ya jamaa kutangaza kwamba sio riziki?me mwenyewe nlikuwa shabaki wake sana.samahan lakini kama ntakuwa nimekukwaza
 
hana lolote maige. anaonesha hasira za kuvuliwa Urais. fisadi mkubwa huyu

Mi nadhani kiti kinafaa kuendeshwa kwa busara zaidi ya pupa, so Maige ana ushaur mzur na siyo kumbeza kwani kama ni ufisadi almost all magamba wapo kapuni
 
Haya sasa, Watanzania mnaodanganywa na kina Lukuvu, Werema,Pindi Chana wakilindwa na Ndugai ma polisi, waulizeni walikutana wapi na hao Wazanzibari? Hapa nni nani muongo? ni Lissu au Ccm? Mtakubali kudanganywa hadi lini? Miaka 50 bado haiwatoshi? Acheni kuishabikia Ccm, jaina mia njema na Tanzania

[[
UKWELI unaosemwa na CDM ndio utaiweka Tanzania HURU kwa miaka mia ijayo. Usanii wa CCM utatuulia nchi.
]/QUOTE[/PHP]]
 
Haya sasa, Watanzania mnaodanganywa na kina Lukuvu, Werema,Pindi Chana wakilindwa na Ndugai ma polisi, waulizeni walikutana wapi na hao Wazanzibari? Hapa nni nani muongo? ni Lissu au Ccm? Mtakubali kudanganywa hadi lini? Miaka 50 bado haiwatoshi? Acheni kuishabikia Ccm, jaina mia njema na Tanzania

Sio siri tena kuwa, UKWELI unaosemwa na CDM ndio utaiweka Tanzania HURU kwa miaka mia ijayo. Usanii uliyoonyeshwa bungeni ni wa kulinda mauzauza waliyoyazoea. Lakini mwisho ndio ushafika.......we are now on the count down......
 
Back
Top Bottom