Wazazi hawakuelewana Mahari, Binti anataka atoroke Nyumbani aje kwangu

Wazazi hawakuelewana Mahari, Binti anataka atoroke Nyumbani aje kwangu

holoholo

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2023
Posts
1,859
Reaction score
2,986
Wakuu
Mimi ni kijana wa umri wa kuoa (miaka kati ya 23-30),mwezi wa nane mwaka jana nilienda kuchumbua katika kijiji jirani,

Nilienda na mwenyeji wangu,NA zoezi la kuchumbia lilikamilika na kishika uchumba tuliacha Tsh.10,000(kwa wale wasukuma watakubaliana na mimi kuhusu mchakato wa kuchumbia),

Badae wazazi wangu na wa mchumba wangu wakakutana kupanga mahari,lakini kiukweli hawakuelewana,wazazi wa binti walisema ng'ombe 12 lakini wazazi wangu walisema ni milioni mbili na laki mbili tu,hivyo hawakuelewana na wakapotezeana.

Lakini binti akazisaka namba zangu mpaka akazipata, tukawa tunawasiliana,anasema ananipenda na anataka tuoane tu licha ya wazazi kutoelewana,anataka kutoroka nyumbani kwao aje kwetu kuolewa,licha ya kumchenga chenga kuwa asubili lakini imefikia hatua binti analia anasema anakuja.
Na nikikataa atajinyonga

Mwishowe nikashawishika, akaniambia nimtumie hela ya kuja kwetu,ndo juzi nimemtumia elfu kumi atoroke aje kwetu

Wajuvi wa mambo mnanishauri/mnanisaidia vipi katika hili?

Karibuni.
 
Kwa nini atotoroke au umtoroshe.

Angetakiwa hayo maamuzi ayatoe siku ileile palepale mbele za wazazi wake wakiwepo na mashahidi.
Na wewe utoe Msimamo wako hapohapo.

Wasingeweza kufanya lolote.
Ila hiki kinachoenda kutokea ni Uhuni na kugeukana ni dakika Mbili
 
  • Kama hayupo tayari kuwatii wazazi wake ambao wamemlea tangu azaliwe; jiandae zamu yako ikifika
  • Kama anatishia kujiua haujamuoa; uwezekano mkubwa mkipata changamoto atajiua akiamini ndio suluhisho pekee

Maoni yangu: hakuna mwanamke hapo, endelea kutafuta.
 
Wakuu
Mimi ni kijana wa umri wa kuoa (miaka kati ya 23-30),mwezi wa nane mwaka jana nilienda kuchumbua katika kijiji jirani,

Nilienda na mwenyeji wangu,NA zoezi la kuchumbia lilikamilika na kishika uchumba tuliacha Tsh.10,000(kwa wale wasukuma watakubaliana na mimi kuhusu mchakato wa kuchumbia),

Badae wazazi wangu na wa mchumba wangu wakakutana kupanga mahari,lakini kiukweli hawakuelewana,wazazi wa binti walisema ng'ombe 12 lakini wazazi wangu walisema ni milioni mbili na laki mbili tu,hivyo hawakuelewana na wakapotezeana.

Lakini binti akazisaka namba zangu mpaka akazipata, tukawa tunawasiliana,anasema ananipenda na anataka tuoane tu licha ya wazazi kutoelewana,anataka kutoroka nyumbani kwao aje kwetu kuolewa,licha ya kumchenga chenga kuwa asubili lakini imefikia hatua binti analia anasema anakuja.
Na nikikataa atajinyonga

Mwishowe nikashawishika, akaniambia nimtumie hela ya kuja kwetu,ndo juzi nimemtumia elfu kumi atoroke aje kwetu

Wajuvi wa mambo mnanishauri/mnanisaidia vipi katika hili?

Karibuni.
Duh....
Usimruhusu, utakuja kunishukuru baadae
 
Mpokee huyo mkeo kisha tuma mjumbe akawape taarifa kuwa wasimtafute yuko mahala salama kisha tulia. Fanya hivi ndani ya siku mbili.
Baada ya hapo watakuja wenyewe na wewe wape ng'ombe mmoja hadi watatu wa mchenya na habari yao yao inakuwa imeishia hapo. Wakimbeba binti mtoroshe tena. Hizo ndio desturi za kisukuma.
Pullaga nyanda chuuuh.
 
Back
Top Bottom