holoholo
JF-Expert Member
- May 10, 2023
- 1,859
- 2,986
Wakuu
Mimi ni kijana wa umri wa kuoa (miaka kati ya 23-30),mwezi wa nane mwaka jana nilienda kuchumbua katika kijiji jirani,
Nilienda na mwenyeji wangu,NA zoezi la kuchumbia lilikamilika na kishika uchumba tuliacha Tsh.10,000(kwa wale wasukuma watakubaliana na mimi kuhusu mchakato wa kuchumbia),
Badae wazazi wangu na wa mchumba wangu wakakutana kupanga mahari,lakini kiukweli hawakuelewana,wazazi wa binti walisema ng'ombe 12 lakini wazazi wangu walisema ni milioni mbili na laki mbili tu,hivyo hawakuelewana na wakapotezeana.
Lakini binti akazisaka namba zangu mpaka akazipata, tukawa tunawasiliana,anasema ananipenda na anataka tuoane tu licha ya wazazi kutoelewana,anataka kutoroka nyumbani kwao aje kwetu kuolewa,licha ya kumchenga chenga kuwa asubili lakini imefikia hatua binti analia anasema anakuja.
Na nikikataa atajinyonga
Mwishowe nikashawishika, akaniambia nimtumie hela ya kuja kwetu,ndo juzi nimemtumia elfu kumi atoroke aje kwetu
Wajuvi wa mambo mnanishauri/mnanisaidia vipi katika hili?
Karibuni.
Mimi ni kijana wa umri wa kuoa (miaka kati ya 23-30),mwezi wa nane mwaka jana nilienda kuchumbua katika kijiji jirani,
Nilienda na mwenyeji wangu,NA zoezi la kuchumbia lilikamilika na kishika uchumba tuliacha Tsh.10,000(kwa wale wasukuma watakubaliana na mimi kuhusu mchakato wa kuchumbia),
Badae wazazi wangu na wa mchumba wangu wakakutana kupanga mahari,lakini kiukweli hawakuelewana,wazazi wa binti walisema ng'ombe 12 lakini wazazi wangu walisema ni milioni mbili na laki mbili tu,hivyo hawakuelewana na wakapotezeana.
Lakini binti akazisaka namba zangu mpaka akazipata, tukawa tunawasiliana,anasema ananipenda na anataka tuoane tu licha ya wazazi kutoelewana,anataka kutoroka nyumbani kwao aje kwetu kuolewa,licha ya kumchenga chenga kuwa asubili lakini imefikia hatua binti analia anasema anakuja.
Na nikikataa atajinyonga
Mwishowe nikashawishika, akaniambia nimtumie hela ya kuja kwetu,ndo juzi nimemtumia elfu kumi atoroke aje kwetu
Wajuvi wa mambo mnanishauri/mnanisaidia vipi katika hili?
Karibuni.