Wazazi mnaolinda sana watoto kupitiliza, mnawaandaaje kukabiliana na maisha halisi ya hapa Bongo?

Wazazi mnaolinda sana watoto kupitiliza, mnawaandaaje kukabiliana na maisha halisi ya hapa Bongo?

G Tank

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2023
Posts
2,297
Reaction score
8,760
Watoto wana haki ya kudeka na kufaidi matunda ya wazazi lakini ni muhimu pia wao wajifunze kuwajenga uwezo wa kujisimamia bila backup ya mzazi.

Kwa maisha ya kiuhalisia ya hapa bongo lolote laweza tokea ila angalau mtu ajue kujifulia nguo, kuweza kutumia usafiri wa umma, kuweza kula vyakula kama ugali, kuweza kujitetea anapoonewa, kuweza kumingle na watu wa matabaka mbali mbali, kuweza kufanya kazi za nyumbani bila msaada wa house girl, n.k.

Inashangaza kuona kuna watoto:
  • Hawajui kujifulia, Ni mpaka house girl au mashine
  • Hawawezi kufika sehemu ya mbali hadi wafikishwe,
  • Hawawezi kula ugali, Haya nimeshuhudia kwa macho yangu
  • Wakionewa hawawezi kujitetea hadi mzazi aje
  • Ngumu kumingle na watu wa matabaka ya kawaida
  • House girl asipokuwepo wanaweza kulala njaa, n.k.
 
Ndio maana kila siku nawaambiaga hapa watoeni watoto wenu shule za English Mediums waleteni Kayumba wajifunze uhalisia wa maisha na waishi maisha yao ya utoto " child hood" to the fullest
 
Ni hatar sana, wanaweza wasielewe unachosema.

Dunia haina huruma, bora kukosa huruma huko uanze wewe kuwaonyesha kwa kuwasurubu mapema. Maana utawasurubu kwa upendo.

Na hii itawajenga. Unauma huku unapumuliza. Siku ukiondoka wanakua sio wageni na shuruba za maisha
 
Kikubwa ni mzazi kutambua nafasi yake kwa mtoto.

Hii ndio maana kwasisi wazazi tunamlea na kumlinda mtoto kwa namna ya tofauti ladiri anavyo ongezeka umri.

Hapa namaanisha hauwezi mwambia mtoto wa miaka 3 aoshe chombo alicho kulia chakula, pia huwezi mwambia mtoto wa miaka 5 ajifulie nguo za shuleni, kadhalina hauwezi ukamwambia mtoto wa miaka 8 apike chakula cha nyumba nzima, napia hauwezi mwambia mtoto wa miaka 10 kuhusu mahusiano na ukuwaji.
 
Ndio maana kila siku nawaambiaga hapa watoeni watoto wenu shule za English Mediums waleteni Kayumba wajifunze uhalisia wa maisha na waishi maisha yao ya utoto " child hood" to the fullest
kuna watoto wengi tu wanasoma english medium wanaishi maisha halisi ya bongo, hata shule za serikali za english zipo.

English medium ni muhimu kwasababu ya kurahisisha elimu na mazingira mazuri kwa mtoto kusoma kuanzia madawati, usafi vyooni, kujifunza kwa lugha ya kimataifa, mzazi kupewa taarifa za mara kwa mara, n.k.
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Masikini wana matatizo ya akili
Badala ya kupambana na hali yake, kutwa kufatilia maisha ya watu wengine
Hao watoto watamaliza shule, kazi wataikuta na muendelezo utaendelea watawawekea watoto wao hausugeli
Hii cycle haikusu wewe hasira zako mmalizie mzazi wako alieamua kuzaa wakati hajajipata
una mtazamo mwembamba sana. huwezi kufikiria nje ya box.

Over protective parent sio lazima awe tajiri,.

kuna wazazi kufariki / kuanguka kiuchumi, hakuna ajuae kesho

Hapa bongo hakuna guarantee ya ajira kwasababu zipo chache, kuna watu wengi wazazi wao walikuwa wana vyeo lakini wamemaliza vyuo hawana ajira
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
una mtazamo mwembamba sana. huwezi kufikiria nje ya box.

Over protective parent sio lazima awe tajiri,.

kuna wazazi kufariki / kuanguka kiuchumi, hakuna ajuae kesho

Hapa bongo hakuna guarantee ya ajira kwasababu zipo chache, kuna watu wengi wazazi wao walikuwa wana vyeo lakini wamemaliza vyuo hawana ajira
Niamini mimi whatever the situation wata adopt tu, why do you care kuhusu maisha ya wengine? Unaonea wivu hao watoto au?
 
Ndio maana kila siku nawaambiaga hapa watoeni watoto wenu shule za English Mediums waleteni Kayumba wajifunze uhalisia wa maisha na waishi maisha yao ya utoto " child hood" to the fullest
Kule English Medium hakuna uhalisia wa maisha ya kumjenga mtoto. Wanaweka bidii kukaririsha mtoto masomo apate 'A' tu na ajue kiingereza. Lkn Stadi za Maisha (Life Skills) hafifu sana.
 
Kule English Medium hakuna uhalisia wa maisha ya kumjenga mtoto. Wanaweka bidii kukaririsha mtoto masomo apate 'A' tu na ajue kiingereza. Lkn Stadi za Maisha (Life Skills) hafifu sana.
Shule hailei mtoto,
Kuna life skills atazipata shuleni nyingine mzazi anachukua nafasi Kwa malezi ya nyumbani,
Pesa isizuie kufikiri Kwa mtu focus ni Kwa kilicho Bora.

Tuwe wawazi asilimia kubwa ya watoto wanaosoma Kayumba ni wanatokea Katika familia zenye kipato kidogo, unataka kuniambia kipato kidogo ndio uwezo mkubwa wa kuwa na life skills za kutosha?
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Malezi ni kitu kizuri sana huku ukubwani unaweza kukutana na mtu alielelewa hovyo mambo anayofanya ni aibu tupu.
 
kila mwanadamu ameumbwa na uwezo wa kuadapt mazingira kwa namna ya kipekee sana wala usihofu, worry urself with some other stuffs.
Fungal theads anaona mtt wa kihindi au kiarabu wanaenda shule privately car anaona yy atamshinda maidha dah
 
Kule English Medium hakuna uhalisia wa maisha ya kumjenga mtoto. Wanaweka bidii kukaririsha mtoto masomo apate 'A' tu na ajue kiingereza. Lkn Stadi za Maisha (Life Skills) hafifu sana.
Hakuna cha life skills wala nini, sema tu unaskini mbaya sana.

Kila mzazi anatamani mtoto wake asome shule yenye viwango vyote sio shule mavumbi.

Ufukara ndio kikwazo na kupelekea watu kujifariji
 
Watoto wana haki ya kudeka na kufaidi matunda ya wazazi lakini ni muhimu pia wao wajifunze kuwajenga uwezo wa kujisimamia bila backup ya mzazi.

Kwa maisha ya kiuhalisia ya hapa bongo lolote laweza tokea ila angalau mtu ajue kujifulia nguo, kuweza kutumia usafiri wa umma, kuweza kula vyakula kama ugali, kuweza kujitetea anapoonewa, kuweza kumingle na watu wa matabaka mbali mbali, kuweza kufanya kazi za nyumbani bila msaada wa house girl, n.k.

Inashangaza kuona kuna watoto:
  • Hawajui kujifulia, Ni mpaka house girl au mashine
  • Hawawezi kufika sehemu ya mbali hadi wafikishwe,
  • Hawawezi kula ugali, Haya nimeshuhudia kwa macho yangu
  • Wakionewa hawawezi kujitetea hadi mzazi aje
  • Ngumu kumingle na watu wa matabaka ya kawaida
  • House girl asipokuwepo wanaweza kulala njaa, n.k.
Ukiona Mzazi anamlinda sana mtoto wake ujue ujanani kwake alikua on fireee sasa apo mawazo kila wakati kwa wanawe wasijefanyiwa yale aloyafanya yy
 
Back
Top Bottom