SoC01 Wazazi tuache kuharibu ndoa za wenetu

SoC01 Wazazi tuache kuharibu ndoa za wenetu

Stories of Change - 2021 Competition
Joined
Jul 29, 2021
Posts
81
Reaction score
158
Habari za wakati huu wan JF. Nimekuja na kitu kingine, sio kipya ila nilikiandika kwa sehemu tu na nikaona imepata mwitikio mkubwa sana, hivyo nikaona kuwa nina wajibu wa kuandika zaidi ili kudadavua uzi wangu.

Imekuwa ni kawaida kwa watu wanapooana kwa ndugu kuja kukaa na Wana ndoa hao hasa kama wana maisha mazuri kidogo. Huwa Jambo hili linachukuliwa kirahisi sana, lakini lina uzito wake na tena uzito mkubwa sana. Na Jambo hili huweza hata kuleta mfarakano na limeshaharibu ndoa nyingi.

Baada ya muda katika ndoa, mwanaume atamleta mama yake au ndugu zake katika nyumba ambapo wana ishi na mke wake. Sikatai kwamba mwanaume asimlete mama yake nyumbani la hasha. Ila Kuna sababu ambazo zitamfanya mzazi aje aishi nyumbani kwa mwanae. Mfano mama Ni mgonjwa Sana na hana mtu wa kumuhudumia huko alipo, maisha magumu sana, au nizee sana,hawezi kujihudumia na anahitaji msaada.

Lakini kama mzazi ana nguvu, anaweza kulima (kama ni mkulima ) au kufanya kazi zake za kawaida ni makosa makubwa kuja kuishi moja kwa moja kwenye nyumba ya mwanao ambaye ameoa.

Ninasema hivi kwasababu, mzazi kama mzazi anakuwa na mtazamo na fikra za tofauti kidogo ya jinsi mwanao wa kiume anavyotakiwa kuwa katika ndoa yake , kwakuwa yeye ni baba wa nyumba. Mfano, mzazi atategemea awe anapikiwa , anafanyiwa kila kitu na mkewe, hasa zile kazi za nyumbani. Sasa unaenda kuishi pale, unakuta labda kila siku za jumapili mwanao wa kiume anapika, anafua nguo na mingineyo. Au unakuta ana vaa mavazi kama suruali, taiti na vi hot pants. Au zaidi kabisa unakuta mke hajui kupika.

Wewe kama mzazi lazima uingilie, utaona kama unatatua tatizo lakini kumbe unaharibu kabisa mahusiano yao. Nyakati hizi ni tofauti, Kuna mabadiliko mengi kutokana na tekinolojia. Na pia kabla ya kuingilia jiulize kwani kabla sijaja kuishi hapa walikuwa wanaishije, ukishagundua hayo, utakuwa umepata jibu.

Na wanawake wengi huwa hwako tayari kwa mzazi wa mume aje kuishi nyumbani na siyo kwamba hampendi mama wa mumewe hapana, ila tu wanahofia na wanajaribu kukwepa ugomvi na mipishano inayoweza kutokea. Nilimuuliza mwanamke mmoja kuhusu hili na aliniambia kitu ambacho kilinishtua kidogo.

Aliniambia kuwa mama yake husema, “hapendi kwenda kwenye nyumba ya mwana mwanawe wa kike kwasababu anakuwa hana uhuru, ila ingekuwa mwanae Ni wa kiume, ndio angejisikia Uhuru kwasababu angekuwa na nguvu”.

Haya maneno yalinishtua sana kwasababu yana ukweli Sana. Na atakama huwa haya semwi, hujidhirisha kwa vitendo. Hebu fikiria wakati manaishi na mama nyumbani, alafu ugomvi utokee kati ya mama yako na mkeo, wewe utakuwa upande wa nani?

Jibu lipo wazi kabisa ya kuwa utakuwa upande wa mama, bila hata ya kujua chanzo utakuwa upande wake tu. Na ndiyo hiki ambacho wanachokihofia na ndio maana hawako tayari, hatakama huwa hawasemi. Na wanawake wengi huwa hawasemi kuwa hawako tayari kwa hili kwasababu wanaogopa kuonekana wana roho mbaya na hawapendi wa mume.

Lakini mzazi, kama mzazi anayejielewa kama hana sababu ya muhimu, hawezi kuja kukaa kwenye nyumba ya mwanae ambaye ana mke wake. Ni makosa, kitamaduni na hata kifikra.
 
Upvote 2

Wazazi tuache kuharibu ndoa za wenetu.​

Mtoa mada uzi ni mzuri ila umeubana sana, yaani unahitajika uchambuliwe zaidi ya hapo .
Kwenye suala zima la wazazi kuharibu ndoa watoto wao ni kubwa na lipo katika apects tofauti tofauti , ikiwemo maslahi binafsi ya mzazi au wazazi kwa vijana wao ambao wapo kwenye ndoa tayari huchangia kwa sehemu kubwa kuharibu ndoa za vijana wao .
 
Habari za wakati huu wan JF. Nimekuja na kitu kingine, sio kipya ila nilikiandika kwa sehemu tu na nikaona imepata mwitikio mkubwa sana, hivyo nikaona kuwa nina wajibu wa kuandika zaidi ili kudadavua uzi wangu.

Imekuwa ni kawaida kwa watu wanapooana kwa ndugu kuja kukaa na Wana ndoa hao hasa kama wana maisha mazuri kidogo. Huwa Jambo hili linachukuliwa kirahisi sana, lakini lina uzito wake na tena uzito mkubwa sana. Na Jambo hili huweza hata kuleta mfarakano na limeshaharibu ndoa nyingi.

Baada ya muda katika ndoa, mwanaume atamleta mama yake au ndugu zake katika nyumba ambapo wana ishi na mke wake. Sikatai kwamba mwanaume asimlete mama yake nyumbani la hasha. Ila Kuna sababu ambazo zitamfanya mzazi aje aishi nyumbani kwa mwanae. Mfano mama Ni mgonjwa Sana na hana mtu wa kumuhudumia huko alipo, maisha magumu sana, au nizee sana,hawezi kujihudumia na anahitaji msaada.

Lakini kama mzazi ana nguvu, anaweza kulima (kama ni mkulima ) au kufanya kazi zake za kawaida ni makosa makubwa kuja kuishi moja kwa moja kwenye nyumba ya mwanao ambaye ameoa.

Ninasema hivi kwasababu, mzazi kama mzazi anakuwa na mtazamo na fikra za tofauti kidogo ya jinsi mwanao wa kiume anavyotakiwa kuwa katika ndoa yake , kwakuwa yeye ni baba wa nyumba. Mfano, mzazi atategemea awe anapikiwa , anafanyiwa kila kitu na mkewe, hasa zile kazi za nyumbani. Sasa unaenda kuishi pale, unakuta labda kila siku za jumapili mwanao wa kiume anapika, anafua nguo na mingineyo. Au unakuta ana vaa mavazi kama suruali, taiti na vi hot pants. Au zaidi kabisa unakuta mke hajui kupika.

Wewe kama mzazi lazima uingilie, utaona kama unatatua tatizo lakini kumbe unaharibu kabisa mahusiano yao. Nyakati hizi ni tofauti, Kuna mabadiliko mengi kutokana na tekinolojia. Na pia kabla ya kuingilia jiulize kwani kabla sijaja kuishi hapa walikuwa wanaishije, ukishagundua hayo, utakuwa umepata jibu.

Na wanawake wengi huwa hwako tayari kwa mzazi wa mume aje kuishi nyumbani na siyo kwamba hampendi mama wa mumewe hapana, ila tu wanahofia na wanajaribu kukwepa ugomvi na mipishano inayoweza kutokea. Nilimuuliza mwanamke mmoja kuhusu hili na aliniambia kitu ambacho kilinishtua kidogo.

Aliniambia kuwa mama yake husema, “hapendi kwenda kwenye nyumba ya mwana mwanawe wa kike kwasababu anakuwa hana uhuru, ila ingekuwa mwanae Ni wa kiume, ndio angejisikia Uhuru kwasababu angekuwa na nguvu”.

Haya maneno yalinishtua sana kwasababu yana ukweli Sana. Na atakama huwa haya semwi, hujidhirisha kwa vitendo. Hebu fikiria wakati manaishi na mama nyumbani, alafu ugomvi utokee kati ya mama yako na mkeo, wewe utakuwa upande wa nani?

Jibu lipo wazi kabisa ya kuwa utakuwa upande wa mama, bila hata ya kujua chanzo utakuwa upande wake tu. Na ndiyo hiki ambacho wanachokihofia na ndio maana hawako tayari, hatakama huwa hawasemi. Na wanawake wengi huwa hawasemi kuwa hawako tayari kwa hili kwasababu wanaogopa kuonekana wana roho mbaya na hawapendi wa mume.

Lakini mzazi, kama mzazi anayejielewa kama hana sababu ya muhimu, hawezi kuja kukaa kwenye nyumba ya mwanae ambaye ana mke wake. Ni makosa, kitamaduni na hata kifikra.
Si kweli kwamba mzazi ni mpaka aishi kwako ndipo aalibu ndowa yako, ila niukweli usiyo pingika kuwa wazazi wamekuwa nisehem ya kuvunja ndowa za watoto wao hususan hawa mama zetu

Baba hata akiona Jambo ambalo hajalipenda kwa mkeo hawezi kumueleza moja kwa moja mkeo kuwa unacho fanya hiki unakosea lah
Baba Sana sana atakacho kifanya nikumuita kijana wake pembeni na kumpa ushauli au mbinu za kulitatua tatizo au kero ambayo anahisi inaweza leta tatizo kwenye ndoa yake

Lakini wa mama hawana Subira
Tena mkeo akibughi kidogo tu mbele yake ni palepale anakutana na za uso yaani majibu yake ni pale pale

Tena usio mbee kijana wake akaingia mda huo shosti kazi unayo lazima vumbi litimke pale, na dowa itaanzia hapo kutengeneza nyufa tena ni nyufa zisizo zibika
 
Ulisemalo n kweli mkuu,kuna mwanangu kbs golikipa wa timu mojawapo za kibongo hapaa alikuwa anaishi na mwanamke anayempenda sana na Wana mtt mmoja ,lkn bi mkubwa wa mwana ajawahi mpenda mkwe wake hata kdg amemfanyia viojaa dada wa watu mpk mdadaa akaamua kuondoka ingali wanapendana na bi mkubwa anamwambia Kijana wake ole wako uku analamba ardhi ukirudiana na huyo mwanamkeee labda cjakuzaa mm,na ukiangalia jamaa nyumba kajenga yy ingali kiwanjaa kilikuwa tyr mama alinunuaa,jamaa allipambana sana lkn mwishowe aligonga mwambaa maana aliamua kumwacha b mkubwa pale hom ili akapange arudiane na mkewe lkn alipomwambia b mkubwaa weeeeeee kilinukaa ,mwishowe jamaa akatuliaa na dada wawatu kaendaa kuwa single mother kisa mkwe wakee,kiukwel kuna baadhi ya mama zetu wanatuwekea nuksi ktk maisha yetu ya mahusiano
 
Uko sahihi, kuna wazazi wanawashwa washwa na viherehere
 
Ndoa zina vikwazo aiseee. Pole yao wanaopitia changamoto hizo
 
Back
Top Bottom