Beatrice Kamugisha
JF-Expert Member
- May 18, 2019
- 762
- 6,984
Jana nilipitia taarifa ya Jeshi la Polisi Dar kuhusu ujambazi na kukamatwa kwa majambazi. Lakini leo nimeambiwa kuna vijana wanashiba bangi wanajipanga hadharani kwenda kuiba huku mchana kutwa wakiwa kwenye bar na vijiwe vya bangi wakibugia vilevi. Niwaomba wazazi, msiwalazimishe Polisi wakawasaidia kulea maana wakiamua kuwalea watoto tutawazika wengi.
Polisi ya Leo si Polisi ya miaka ya nyuma, watu wanakuchoma kwa RPC kupitia namba zilizotolewa hivi karibuni. Mzazi unayemtakia mema mwanao mkanye. Jirani unayecheka naye ndiye mlinzi wa amani wa serikali tusiendelee kuamini kwamba maisha yatasonga tu kwa kupiga tukio na kujificha. Simu za camera zinatumika sana kufichua waalifu, mkanye mwanao.
Nayasema haya kwa sababu nafahamu kijana kabetuliwa kwenye tukio juzi kati kanda ya ziwa baada yakutunishiana misuli na dola. Pls walindeni ndugu zenu kwa kuwachoma kwenye vyombo vya dola lakini pia kuwakanya
Polisi ya Leo si Polisi ya miaka ya nyuma, watu wanakuchoma kwa RPC kupitia namba zilizotolewa hivi karibuni. Mzazi unayemtakia mema mwanao mkanye. Jirani unayecheka naye ndiye mlinzi wa amani wa serikali tusiendelee kuamini kwamba maisha yatasonga tu kwa kupiga tukio na kujificha. Simu za camera zinatumika sana kufichua waalifu, mkanye mwanao.
Nayasema haya kwa sababu nafahamu kijana kabetuliwa kwenye tukio juzi kati kanda ya ziwa baada yakutunishiana misuli na dola. Pls walindeni ndugu zenu kwa kuwachoma kwenye vyombo vya dola lakini pia kuwakanya