Wazazi wakataa sadaka ya kuchinja iliyotolewa na Waarabu, wakidai watoto wao watatolewa kafara

Sasa hiyo ya kuwachinjia mbuzi zaidi ya 130 Kwa siku moja itaondoa hiyo shida ya njaa shuleni?
Ni ujuha kuwachinjia wanafunzi ng'ombe 400 na mbuzi 135 Kwa siku moja tena ati sadaka.
 
hili swala ni gumu wakristo wamelichukua kwa kuvumilia tu halina win win situation mwisho wa siku tukakubali kutokukubaliana wacha mchinje watu walijaribu kususa kile mnachofanya nyinyi effect zake tunazikumbuka tukawatia hasara watu.
lakini si busara sana kula unachojua ni sadaka ya wengine usiojua madhumuni yao.
 

Kuna wakristo hawali nyamafu,,,kuku, mbuzi, ng'ombe n.k atampelekea muislamu amchinjie, na co mkristo. Allaahu akbar
 

Kwaiyo ishu hapa ni waarabu co! Wangelikuwa wazungu wenu mcngekereka eti 😁 na misaada yao hao wazungu munaipokea kwa mikono miwili eti! 😁

haya bwana,,endeleeni kuamini hivyo,,,ila mjuwe waarabu hawana huo ujinga wa kutoa watu kafara kama wafanyavyo hapa,, hawana nia mbaya kwenye utoaji wa sadaka, hizo ni imani zenu zinawa2ma muwafikirie ivyo,,,na waarabu tumekuwanao, tumeishinao karne na karne.
 
Kama kweli wana nia njea watoe hiyo mifugo ikiwa hai kama sadaka then kamati ya shule itafute wateja pesa itakayopatikana ijenge ukuta au library ila wakigoma mpaka wachinjwe na waliwe na wanafunzi basi wakataliwe watafute maeneo mengine ambapo watakubali.Wapeleke hapo handeni watagombewa na mashule
 
Wenzetu wa mlengo huo hawajielewi, wao wanawaza kula tu. Toa msaada ambao utakuwepo na kesho, jenga ukuta au madarasa, au nunua madawati au vitabu.
Alafu si Kuna shule za kiislamu, kwa nini wasipeleke huko?
 
😀😀😀 mwisho wa siku tukubali hawa jamaa wametugawa!
 
Kuna wakristo hawali nyamafu,,,kuku, mbuzi, ng'ombe n.k atampelekea muislamu amchinjie, na co mkristo. Allaahu akbar
🤣🤣🤣🤣 ninyi si ndio mna leseni ya kuua (wanafanya hivyo kwa ajili ya mahusiano na jamii tu) kwangu nafuga nyati nafikiri nikualike uje mchinje!
 
🤣🤣🤣🤣 ninyi si ndio mna leseni ya kuua (wanafanya hivyo kwa ajili ya mahusiano na jamii tu) kwangu nafuga nyati nafikiri nikualike uje mchinje!

Nialike mkuu nimchinje kisha tumle kwa pamoja 🤣🤣🤣🤣
 
Kaka wamekula siku moja wameenda toilet kesho nani atawapa tena nyama ya mbuzi? Ungekua ni msaada endelevu hata kwa miaka5 sawa.
Ukuta unakaa miaka mia kaka,hao wazazi wanawaza mbali

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Kumbuka huo ni msaada hujatoa hata senti yako hivyo ni hiari yako kupokea au kukataa lakini sio kumpangia anayetoa msaada ni kipi cha kukufanyia, ni issue ndogo ila mnaikuza kama kuna waliyolazimishwa kula.
 
Mwarabu huko Rufiji aliambiwa na mwindaji baada ya kumjeruhi Nyati awahi amchinje alitukana matusi yote! chezea kifo!

Hahhaaa,,,hapo alitakiwa aongezewe risasi nyingine ya kichwa kisha wamchinje. Hao wanyama ni hatari mno
 
Mkuu huo ni msaada tu ni hiari ule au uache ila sio akili kumpangia mtu kwa pesa yake akufanyie nini.
Kama wana shida ya ukuta wangeomba wajengewe ila sio mtu kaja anakupa kitu chake hajachukua hata mia yako unaanza kumpangia vipaumbele vyako kwenye shida zako sasa inahusiana vp? we acha mwenye kutaka kula hiyo nyama atakula mwenye kusubiri ajengewe ukuta asubiri ni simple tu.
 
kwanini hizo mbuzi zisitolewe nzima nzima kwa hiyo shule na shule ikawa na mradi wake wa kufuga mbuzi..
Au wapewe mashine za kufyatua matofali ili wajenge kuta wazitakazo maana si ndio kipaumbele chao ukuta.
 
Ni upumbavu tuu watanzania wa leo sio wale..kwel ufunge safar kuja kutusaidia a single meal seriously?????tena shule mjin???
Halafu kitu kingine.... Tokea lini tukaanza kulazimishana kupokea sadaka/ misaada??

Kama walengwa wamekataa.... What's the logic ya kuanza kulazimishana kupokea sadaka za nyama ya mbuzi na ngombe🤣😂
 
Kama ni kula nyama tumeanza kula nyama toka tunapondewa na mama zetu miezi Tisa huko mpaka sasa.... Na umri tulionao tunaendelea kula nyama.... 🤣😂
 
Kwa nini msipeleke madrassa au msikitini? Au huko kote wana uwezo wa kula nyama?
Hata huko misikitini nyama huwa inapelekwa sana tu mkuu, na sio nyama tu kuna visima pia n.k kwa kifupi nyama ni sehemu tu ya hiyo misaada kutoka huko kwa hao wenzetu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…