Wazazi wangu wakija kwangu wanafanya maamuzi ya nini kifanyike!

Wazazi wangu wakija kwangu wanafanya maamuzi ya nini kifanyike!

suzieq

New Member
Joined
Sep 10, 2022
Posts
2
Reaction score
26
Habari wanajamvi,

Kwa muda sasa kuna jambo limekua linaniumiza na nimekosa pa kuliongelea kwa uhuru ila naamini humu nitapata hekima na busara zangu.

Kama ilivyo ndoto ya kila mzazi anaesomesha mtoto ni ili mtoto ajisimamie na awe msaada kwa wazazi na nduguze baadae. Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwangu nimesomeshwa vizuri na nimepata kazi nzuri ambau=yo imeniwezesha kufanya makubwa kwetu ikiwemo kumaliza ujenzi wa nyumba ya wazazi , kuwakatia bima na kuhakikisha wanapata matumizi yao ya kila mwezi kwa kifupi wanaishi maisha comfortable.

Wakati huo pia na mimi kama binti najiendeleza kimaisha maana tayari nina familia japo mwezangu palitokea mgogoro tukatengena.

Shida ipo hivi: Tangu nimeachana na mwenzangu ( kiukweli hakuna aneingia kwenye ndoa achane japo matatizo mengine hayavumiliki) ni kama wazazi wangu ni kitu walichokua wanakitaka maana wana access na mimi na wana nicontrol kama wanavyotaka jambo ambalo kwangu halijakaa sawa kuwaambia siwezi ila mimi pia kama mtu mwenye mji wangu kuna mambo ambayo naamini nimeyavuka nje ya control ya wazazi.

Kwa mfano bi mkubwa akija kwangu bila kuuliza ataingia kabatini na kuvaa nguo zangu magauni, kanga etc sioni kama limekaa sawa japo sisemi. Akija pia nakua sina uhuru na kwangu atapanga kila kitu tuleje, tuishije etc na sio mara moja nimesharudi toka kazini nikakuta sijawekewa chakula nyumbni kwangu mwenyewe mama akiwepo!!

Ikiwa nimepata la deal kazini na bi mkubwa akajua ataniambia nisipeleke pesa kwenye ujenzi bali niwape wao waweke kwenye biashara au watatue issue fulani( ikumbukwe hapo mimi huwapa pesa kila mwezi atleast 200k ama zaidi wakati mwingine mbali na kununua mahitaji, umeme etc) .Ikumbuke issue nyingine za kifamilia misiba, shuhuli etc nimebeba mie japo pia ninao ndugu wengine ila mimi ndio 70% wengine hizo zilizo baki.

Kiuhalisia mbali na kuwahudumia na mimi lazima maisha yaendelee tayari nina mji wangu, kuna wakati alininunia alipojua nimepata hela sijamuambia nikapeleka site. Bi mkubwa ameenda mbali zaidi akija hapa nyumbani hujenga mazoea na watu kiasi kwamba muda wote unakuta nyumba ina watu wengine hata siwafahamu na sio ndugu kitu ambacho sio sawa kwa usalama na privacy. ( Mfano wauza mboga, mara fundi cherehani mara watu wasaluni yani wote atataka awazoeeee kupitiliza)

Najitahidi sana wakija wazazi friji ipendeze na jikoni pawe vizuri wale wanachopenda ila atakula kisha atasema kabisa sijaridhika ikumbukwe yeye ndo ameamua kipikwe nini!! Hapo nitamuuliza nipike nini tena angalau afurahie.....daaaaah naumia kuna wakati mzee alikuja napika chakula saa ingine hagusi au anakula kidogo kisha anamwambia bi mkubwa sijala hapo ntapigiwa simu nisemweeee. Yani wakati mwingine najifungia ndani nalia tu.

Najua kwa baadhi sitaeleweka ila kuna pattern niiliisoma nikaumia kwamba kwa namna fulani huenda shida katika nyumba yangu ilisababishwa na wao kwasabau kwa bahati mbaya yule mwenzangu hakua vizuri sana kwa hiyo ni kama waliona hawanifaidi vya kutosha kwa hivyo kwa namna fulani hivi nilivyo kwao ni fursa.
Najua wengi mnaweza kunisema ila pia ni kitu nimekaa nacho zaidi ya miaka mili kinanisumbua. Naomba mnisaidie naishije ama nafanyaje?

Naomba mnisamehe kwa nitakao wakwaza au kuwaumiza na kuona sina shukrani kwa wazi ila kwa kwli najitahidi sana ila kuna namna fulani naumizwa pia.
 
Ndio maana ulivunja ndoa yako ya kwanza. Una gubu,umimi. Badirika

Pia kila jambo litazame in positive way. Ata kama limekuchefua kiasi gani
 
Habari wanajamvi,

Kwa muda sasa kuna jambo limekua linaniumiza na nimekosa pa kuliongelea kwa uhuru ila naamini humu nitapata hekima na busara zangu.

Kama ilivyo ndoto ya kila mzazi anaesomesha mtoto ni ili mtoto ajisimamie na awe msaada kwa wazazi na nduguze baadae.
Kwa nafasi uliyo nayo n ngumu kufanya au kupata huo uhuru na control yko binafsi kwa sbb moja ty huna mwanaume ambae watu wakiwa wnkuja kwko wnjua kbx pale Kuna mwanaume.

Kwaio kitu Cha kfnya ulshkosea toka mwanzo inwezekana ulkua na kbur kwa jmaa kw sbb una mzd kipato au hkumpa uongoz mty wako pia mybe ulkua unwapa economic status ya mmeo wzaz wako wakaon n foolish kwko.

Kwaio xx Ili hiyo istokee tena tafta men olewa au hta kma kmrdia yule up to u alafu mpe uongozi km mwanaume hamia kwake hata kma umejenga uanze upya n ngumu mwanamk kusimama pkeake hata angemiliki millions of dollars[emoji120][emoji120]
 
Habari wanajamvi,

Kwa muda sasa kuna jambo limekua linaniumiza na nimekosa pa kuliongelea kwa uhuru ila naamini humu nitapata hekima na busara zangu.
Kuwa na msimamo na maisha yako.Vitu vingine ambavyo hupendi ni vizuri kuwaeleza kwa utulivu. Usiwe mpole kupitiliza umeshakuwa mtu mzima sasa wazazi wako wasikuchukulie kama mtoto mdogo.
 
Tafuta mwanaume mtata. Kwa namna umejielezea unaonekana hauna jeuri ya kuwadhibiti wazazi wako kwa tabia za ajabu wanazokufanyiwa.

Ni jambo zuri kuwapa wazazi fadhila na kuwatendea mema ila si sehemu ya wajibu wako ingawa inaweza kuwa sehemu ya majukumu unafanya.

Unatakiwa kuwapa sapoti ya kifedha wazazi wako na kuwasaidia pale inapobidi. Ila hata vitabu vya imani vinawaagiza wazazi kulea na kukuza watoto ili waweze kuja kuwa na maisha bora baadae na kuwabariki kwa utii wao na kuwaombea mema bila kutegemea fadhila au malipo.

Ndio maana hata vijana wasasa wanaendeleza michezo hii hii ya kupata watoto na kuwageuza kitega uchumi au uwekezaji wa kuja kuvuna baadae. Hii ni mbaya sana na si jambo la kistaarabu hata kidogo kwa watu waliostaarabika au wanaojitambua.

Tena walitakiwa kukushuruku sana kwa bidii umeonyesha kuwajengea nyumba, kuwakatia bima ya afya na kuwapa bajeti ya matumizi. Huo sio wajibu wako hata kidogo. Unatakiwa kuwa na familia na kuanza kuipanga muda huu.

Sasa waweke kikao na uongee nao kwa lugha ya kistaarabu kuwa ni muda sasa wakupe nafasi na wewe ufanye maisha. Au kama lugha ni ngumu kuongea. Then watishe tu kuwa kazi umesimama kwa muda unatakiwa kurudi masomoni hivyo utahamia hostel au kwa mwenzako ili kufocus na masomo.

Hawawezi kukulazimisha kufanya mipango yako. Na utafute mtu imara ambaye mtaweza kushauriana vema. Hao wazazi wako wanaonekana sio sampuli ya watu wastaarabu. Na ukiwaendekeza watakufelisha kufanya maisha yako binafsi na utashindwa kupiga hatua kimaisha.
 
Ati sijaridhika? Yamakuwa mapenzi hayo mridhishane? Siku zote wema usizidi uwezo wala wema usigeuke kero. Beba anaebebeka na muonye asipengee kamasi mgongoni abebwapo
 
Habari wanajamvi,

Kwa muda sasa kuna jambo limekua linaniumiza na nimekosa pa kuliongelea kwa uhuru ila naamini humu nitapata hekima na busara zangu.
Sijui kwa nini nimekuonea huruma sana niliposoma andiko hili. Inaonekana wazazi wako ni aina ya wazazi ambao ni controlling sana, they like and enjoy to take charge na ku control maisha ya watoto wao. Inawezekana pia wao wamechangia kwa kiasi fulani ndoa yako kupata matatizo na kuvunjika.

Inawezekana pia ndio sababu hata ndugu zako uliozaliwa nao wamejiweka mbali nao kwa sababu wanajua kuwa wazazi wao ni watu wa aina gani, hivyo wamechagua kuwaweka mbali wabaki tu kama wazazi, kuwahudumia hapa na pale na kuwatembelea hapa na pale na kuwapigia simu, na sio kuwaweka karibu kiundani kama unavyofanya wewe.

Inaonekana wewe either umechelewa kugundua hilo, au unalijua ila una huruma sana hivyo unashindwa kufanya lolote, na wao wanajua kabisa hiyo weakness yako na wanatembea nayo hiyo hiyo (ndio tabia ya watu ambao ni controlling).

Ushauri:
Je, unaweza kuhama huo mkoa uliopo sasa ambao pia wazazi wako wapo? Kama ni wajiriwa, unaweza kuomba uhamisho kazini kwako ukahamia mkoa mwingine? Kama ndio, fanya hivyo, anza process za uhamisho uhame mkoa kwa kisingizio chochote kile, na ukikamilisha uwaage uwaambia umepata uhamisho inabidi uhame, itakua ni hatua muhimu sana kwako katika safari ya kuondoa hiyo control. Kama ofisi yenu suala la kuhama mkoa haliwezekani, basi pia angalia uwezekano wa kutafuta kazi ofisi nyingine ambayo itakua nje ya mkoa ulioko sasa na wazazi wako.
 
Tatizo lenu wanawake mkiwa na pesa kuliko waume zenu mnaanza kuleta dharau naamini ndo maana mumeo mlitengana kwa sababu ulimletea dharau kwa kumzidi kipato.

Sasa pambana na familia yako mwenyewe

Naomba bimkubwa na mshua masta waendelee kukutesa hivyohivyo. Utalia sana wewe mwanamke mbinafsi, mchoyo, mwenye kiburi, kisirani na gubu

Huyu sio wa kuonewa huruma hata kidogo
 
Tatizo lenu wanawake mkiwa na pesa kuliko waume zenu mnaanza kuleta dharau naamini ndo maana mumeo mlitengana kwa sababu ulimletea dharau kwa kumzidi kipato.

Sasa pambana na familia yako mwenyewe

Naomba bimkubwa na mshua masta waendelee kukutesa hivyohivyo. Utalia sana wewe mwanamke mbinafsi, mchoyo, mwenye kibur, kisirani na gubu

Huyu sio wa kuonewa huruma hata kidogo
Dah mkuu sioni sababu ya wewe kumkasirikia bidada namna hiyo?
 
Pole Sana dada yangu....pamoja na mema yote unayo wafanyia wazazi wako lkn hawakutendei haki....na kibaya Zaidi ni kama wanakufanyia makusudi vile.

Na kibaya Zaidi huenda kwakutojua ulikuwa muwazi Sana Kwa mama yako kiasi hata dili za kazini unamwambia,ingetakiwa baada ya kujua wazazi wako sio wastaarabu usingefunguka mambo yako mengi kwao,Hilo ni kosa ukifanya.

Na hata ukipata mwanaume wa kukuoa tarajia vipingamizi toka kwao kwakuwa watashindwa kukutawala,hivyo ukipata mwanaume wa kukuoa uwe imara Sana kufanikisha ndoa yako.

Mwisho hao ni wazazi wako endelea kuwa heshimu na kuwapa msaada Ila angalia namna ya kupunguza kukutawala,kama unadhani hela zako ndo zinawafanya wakutawale,tengeneza mazingira kuonyesha kazini Hali sio nzuri, badilisha mfumo wa Maisha Kwa Mda,wakikuona Hali yako ya kifedha sio nzuri watakuona huna maana na kukupa nafasi.

Na kama ni ujenzi fanya mambo yako Kwa Siri,kwasababu ushajua wazazi wako ni tatizo tayar hakuna dhambi juu ya Hilo maadamu hujawakosea heshima wala kukataa kuwatunza.

Be strong girl yatapita Tu.
 
Pole sana dada ,najua itakuwa swala gumu kuwaeleza ukweli wazazi wako mpaka wakuelewe cha zaidi watakuona umewachoka,

Nakushauri ufanye maamuzi ya kuishi na mwenza wako ambaye unahisi ni chaguo lako,maana unavyoishi mwenyewe usitegemee hizo tabia zitakoma,ikibidi kama inawezekana hama katika hiyo nyumba yako na uipangishe,mhamie nyumba nyingine kwa kufanya hivo nyumba itakuwa na heshima kwa sababu uangalizi wa familia utakuwa chini ya baba,

Tofauti na hapo ule msemo wa 'mtoto hakui kwa mama' utaendelea kuwa kitendawili kwako
 
Kwa nafasi uliyo nayo n ngumu kufanya au kupata huo uhuru na control yko binafsi kwa sbb moja ty huna mwanaume ambae watu wakiwa wnkuja kwko wnjua kbx pale Kuna mwanaume.
Kwaio kitu Cha kfnya ulshkosea toka mwanzo inwezekana ulkua na kbur kwa jmaa kw sbb una mzd kipato au hkumpa uongoz mty wako pia mybe ulkua unwapa economic status ya mmeo wzaz wako wakaon n foolish kwko.
Kwaio xx Ili hiyo istokee tena tafta men olewa au hta kma kmrdia yule up to u alafu mpe uongozi km mwanaume hamia kwake hata kma umejenga uanze upya n ngumu mwanamk kusimama pkeake hata angemiliki millions of dollars[emoji120][emoji120]
Unaonekana ni high IQ ila hujui kuandika. I like the content tho.
 
Back
Top Bottom