Wazazi wangu wakija kwangu wanafanya maamuzi ya nini kifanyike!

Wazazi wangu wakija kwangu wanafanya maamuzi ya nini kifanyike!

Ndio maana ulivunja ndoa yako ya kwanza. Una gubu,umimi. Badirika

Pia kila jambo litazame in positive way. Ata kama limekuchefua kiasi gani
"Badirika" ndio nini? Mbona huko kwingine umeandika vizuri?

Ndio maana hakuna la maana ulilochangia humu.
 
Kwa nafasi uliyo nayo n ngumu kufanya au kupata huo uhuru na control yko binafsi kwa sbb moja ty huna mwanaume ambae watu wakiwa wnkuja kwko wnjua kbx pale Kuna mwanaume.
Kwaio kitu Cha kfnya ulshkosea toka mwanzo inwezekana ulkua na kbur kwa jmaa kw sbb una mzd kipato au hkumpa uongoz mty wako pia mybe ulkua unwapa economic status ya mmeo wzaz wako wakaon n foolish kwko.
Kwaio xx Ili hiyo istokee tena tafta men olewa au hta kma kmrdia yule up to u alafu mpe uongozi km mwanaume hamia kwake hata kma umejenga uanze upya n ngumu mwanamk kusimama pkeake hata angemiliki millions of dollars[emoji120][emoji120]
Umeshafanya homework yako? Kesho shule....na ukajifunze kuandika.
 
Dada... sio lazma mwanaume. Kaa mbali na wanaokukera, wasaidie unapoweza kuwasaidia, waheshimu. Lakini kaa mbali, punguza mazoea. Kwa sababu, wana ubinafsi, usitegemee watakuelewa ukiwaambia. Sana sana watakuumiza zaidi pale utakapojaribu kuzungumza nao.

Utasikia kauli kama, "mimi ni mama yako", sijui oooh! "Nimekulea tumboni"....mara "mimi ndio nimekusomesha"
 
Najitahidi sana wakija wazazi friji ipendeze na jikoni pawe vizuri wale wanachopenda ila atakula kisha atasema kabisa sijaridhika ikumbukwe yeye ndo ameamua kipikwe nini!! Hapo nitamuuliza nipike nini tena angalau afurahie.....daaaaah naumia kuna wakati mzee alikuja napika chakula saa ingine hagusi au anakula kidogo kisha anamwambia bi mkubwa sijala hapo ntapigiwa simu nisemweeee. Yani wakati mwingine najifungia ndani nalia tu.
Pole sana Dada yangu. Ikumbukwe hawa ni binadamu na wana tabia nzuri na mbaya. Sio kwa sababu ni wakubwa basi tabia mbaya waliacha.La hasha ziko pale pale.

Kama unaweza hamia sehemu nyingine ikiwa unapoishi sio mjengo wako.

Umesoma kwa bidii na kufanya kazi kwa bidii naelewa mafanikio yako ni jitihada zako 80%.

Ni wakati na wewe unyoi maisha. Ulete Boy wako unayempenda mchakatane kisawa sawa kwa uhuru.

Hao wazee ni wazazi wako na u awapenda sana ila wasikupotezee furaha yako.

Jambo Lingine ikiwa wewe ni mtu wa Dini kama mimi Rastaman basi jaribu kuliombea hilo pepo liwatoke.

Naona kama wanaendeshwa na roho za vyura.
 
Pambana wazazi wote wa kibongo ndo wapo hvyo ukiona kwako kwaungua jua kwa mwenzio kwateketea
 
Pole sana dada.
........Tatizo lako ni kuwa una huruma sana, una roho nzuri na unajali sana.
Hii hulka ( tabia ) imenimaliza sana kiasi kwamba hivi sasa natafuta Chuo cha Kufundisha Uchoyo, Roho Mbaya na Ukatili ili nikasome.

99% ya Watu ambao nimekuwa nikiwapenda, nikiwaonea Huruma, nikijitoa kwa hali na Mali Kwao na hata Kuwasaidia iwe kwa Fikra ( Mawazo ) na hata Pesa kama nikiwa nayo ndiyo Wanaoongoza Kuniumiza, Kunichafua, Kunichukia na zaidi Kunifitinisha na Watu.

Kuna muda huwa namlaumu sana Mwenyezi Mungu kuwa ni kwanini Kaniumba kuwa mwenye Huruma, Utu, Upendo, Uaminifu na Ukweli halafu baadae hizi tabia zinageuka kuwa Fimbo ya Kunichapia na Kuniangamizia Kimaisha?
 
Ndio maana ulivunja ndoa yako ya kwanza. Una gubu,umimi. Badirika

Pia kila jambo litazame in positive way. Ata kama limekuchefua kiasi gani
Kichwa chako kibovu sana.
Huoni mzazi alivyo vululu vululu?
Mzazi hapaswi kukosa mipaka kiasi hiki.
Huyo mama ni mharibifu bila shaka ni Mmarangu au mrombo
 
Mi nilimwambia mama nimefukuzwa kazi

Nikapunguza baadhi ya karaha, sijui Kwa nini baadhi ya wamama hufanya hivi hasa Kwa watoto wa kike

Hizi case nimekutana nazo nyingi, yupo tayari akusemee mbovu Kwa mwenzio kama anaona hana maslahi nae ili tu mfarakane ale pesa zako mwenyewe.[emoji20]
1. Baadhi ya wamama wa kimeru
2. Wamarangu ni 90%
3. Warombo 40%

Wazazi hao niliowataja wanashida sana
 
Nawashukuru sana wotee ambao mmechukua muda wenu kusoma na kunishauri , nawashukuru mno na hekima na busara zenu zimenipa mwanga kwa namna fulani. Toka jana moyo wangu umekua mzito mno kuna wakati najifungia ndani nalia ili nipate relief maana naogopa hata kusema kwa ndugu zangu.
Kuna wakati ndugu yangu alimtambulisha mchumba wake wakawa wanawasiliana matokeo yale mama siku nyingine akawa anaomba hela kwa huyu mchumba hilo jambo lilituumiza sana ila ndugu yangu alipata ujasiri wa kumwambia kua hapendi hiyo tabia.
Kwa wale mliosema mimi naonekana nina gubu ama jeuri kwa wanaume...naomba kuwaambia sipo hivyo nipo tofauti kabisa. Ni aina ya mwanamke ambae naweza kumpa mwanaume kadi yangu ya benki ili tu asijione mnyonge endapo mambo yake hayajakaa sawa, naweza kununua au kufanya kitu kwa hela yangu ila nikiulizwa nitasema mume ndio amefanya.... ni mtu wa kumfichia aibu mwenzangu( nisingependa kumuongelea sana kwasabau sio jambo la msingi kwa mada yangu hii)
Hayo niliyoeleza ni mambo machache kati ya mengi ambayo napitia .
Kuna wakati ilifika nikadhamiria kuacha kazi kwasababu kazi nzuri niliyoipata nikategemea itakua baraka kwangu na kwa familia yangu imegeuka huzuni. Sijawahi ku disclos nalipwa kiasi gani ila sijui ni kwa namna gani walifahamu kwa hiyo kuna wakati wanapoomba wanataka uwape walichotaja sio ulichonacho wewe. Anyways ni mambo mengi lakini nashukuru nimepata nguvu ya kushare haya machache na nyinyi na mkaweza kunishauri, nimepokea kwa mikono miwili na Mungu awabariki.
Kwa mlionifuata PM pia asanteni kwa kuguswa na jambo langu na kunishauri na shukuru pia kwa mnaoniombea. Mwisho wa yote nawatakia baraka, furaha na amani katika maisha yenu.
Suzieq
Maza ni Mmarangu au Mrombo?
Huwa hilo tatizo lipo sana
 
Dada ukiendekeza ndugu, wazazi na kujibebesha mizigo utakufa masikini.
Wazee wako local kinoma Mana wanademand more ht ufanyeje hao piga Ban. Weka mipaka kwa kila Jambo / eneo Kuanzia pesa na mengineyo.
Shida Ni wewe kujikabidhi kwao, mwili wako akili yako mikononi mwao.
#Unapowavumilia unawafundisha namna ya kukutendea
 
Habari wanajamvi,

Kwa muda sasa kuna jambo limekua linaniumiza na nimekosa pa kuliongelea kwa uhuru ila naamini humu nitapata hekima na busara zangu.

Kama ilivyo ndoto ya kila mzazi anaesomesha mtoto ni ili mtoto ajisimamie na awe msaada kwa wazazi na nduguze baadae. Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwangu nimesomeshwa vizuri na nimepata kazi nzuri ambau=yo imeniwezesha kufanya makubwa kwetu ikiwemo kumaliza ujenzi wa nyumba ya wazazi , kuwakatia bima na kuhakikisha wanapata matumizi yao ya kila mwezi kwa kifupi wanaishi maisha comfortable.

Wakati huo pia na mimi kama binti najiendeleza kimaisha maana tayari nina familia japo mwezangu palitokea mgogoro tukatengena.

Shida ipo hivi: Tangu nimeachana na mwenzangu ( kiukweli hakuna aneingia kwenye ndoa achane japo matatizo mengine hayavumiliki) ni kama wazazi wangu ni kitu walichokua wanakitaka maana wana access na mimi na wana nicontrol kama wanavyotaka jambo ambalo kwangu halijakaa sawa kuwaambia siwezi ila mimi pia kama mtu mwenye mji wangu kuna mambo ambayo naamini nimeyavuka nje ya control ya wazazi.

Kwa mfano bi mkubwa akija kwangu bila kuuliza ataingia kabatini na kuvaa nguo zangu magauni, kanga etc sioni kama limekaa sawa japo sisemi. Akija pia nakua sina uhuru na kwangu atapanga kila kitu tuleje, tuishije etc na sio mara moja nimesharudi toka kazini nikakuta sijawekewa chakula nyumbni kwangu mwenyewe mama akiwepo!!

Ikiwa nimepata la deal kazini na bi mkubwa akajua ataniambia nisipeleke pesa kwenye ujenzi bali niwape wao waweke kwenye biashara au watatue issue fulani( ikumbukwe hapo mimi huwapa pesa kila mwezi atleast 200k ama zaidi wakati mwingine mbali na kununua mahitaji, umeme etc) .Ikumbuke issue nyingine za kifamilia misiba, shuhuli etc nimebeba mie japo pia ninao ndugu wengine ila mimi ndio 70% wengine hizo zilizo baki.

Kiuhalisia mbali na kuwahudumia na mimi lazima maisha yaendelee tayari nina mji wangu, kuna wakati alininunia alipojua nimepata hela sijamuambia nikapeleka site. Bi mkubwa ameenda mbali zaidi akija hapa nyumbani hujenga mazoea na watu kiasi kwamba muda wote unakuta nyumba ina watu wengine hata siwafahamu na sio ndugu kitu ambacho sio sawa kwa usalama na privacy. ( Mfano wauza mboga, mara fundi cherehani mara watu wasaluni yani wote atataka awazoeeee kupitiliza)

Najitahidi sana wakija wazazi friji ipendeze na jikoni pawe vizuri wale wanachopenda ila atakula kisha atasema kabisa sijaridhika ikumbukwe yeye ndo ameamua kipikwe nini!! Hapo nitamuuliza nipike nini tena angalau afurahie.....daaaaah naumia kuna wakati mzee alikuja napika chakula saa ingine hagusi au anakula kidogo kisha anamwambia bi mkubwa sijala hapo ntapigiwa simu nisemweeee. Yani wakati mwingine najifungia ndani nalia tu.

Najua kwa baadhi sitaeleweka ila kuna pattern niiliisoma nikaumia kwamba kwa namna fulani huenda shida katika nyumba yangu ilisababishwa na wao kwasabau kwa bahati mbaya yule mwenzangu hakua vizuri sana kwa hiyo ni kama waliona hawanifaidi vya kutosha kwa hivyo kwa namna fulani hivi nilivyo kwao ni fursa.
Najua wengi mnaweza kunisema ila pia ni kitu nimekaa nacho zaidi ya miaka mili kinanisumbua. Naomba mnisaidie naishije ama nafanyaje?

Naomba mnisamehe kwa nitakao wakwaza au kuwaumiza na kuona sina shukrani kwa wazi ila kwa kwli najitahidi sana ila kuna namna fulani naumizwa pia.
Kwanza kabisa pole sana, binafsi nimekuelewa sana sana, ninachokiona chanzo kikubwa cha kuachana na mume wako kimechangiwa kwa kiasi kikubwa na wazazi wako. Hujasema kisa cha kuachana ila inaonyesha wazazi wako wamechangia kwa asilimia kubwa, ukitaka kuelewa hili mrudiane na mume wako utaona hilo vizuri.
Tabia za wazazi kama hawa nimewahi kuona kwa baadhi ya watu, wapo wazazi wana shida hii, sijajua ni nini ila ni tabia zinazokera sana.
Shida ipo kwao, wanashindwa kuelewa mipaka yao, wanafikiri wanaweza kufanya wanachojua wao. Kinachosumbua zaidi baba na mama ni kitu kimoja, angekuwa mama peke yake ungeweza kumsaidia kwa urahisi.
Wazo langu watumie watu wanaoaminika na wazazi wako waeleze kisa na mkasa, kisha wajue namna ya kuongea nao pasipo kujua uhusika wako.
Ukishindwa kuwapata hao watu watumie viongozi wako wa dini, wanaweza kuandaa semina ya wazazi kuwa na mipaka kwa watoto wao.
Usipofanya hivyo utapata mwanaume mwingine utaingia kwenye shida ile ile ya kuachana. Wanaume wachache watavumilia matendo ya wazazi wako wengine hawawezi.
Chumba chako kiwe na mipaka, funga chumba chako, wazazi waishie kwenye vyumba vyao ulivyowapa. Suala la mzazi kuingia chumbani kwako kuchukua nguo anayotaka sio heshima.
Kwahiyo tumia hao watu kutokana na mazingira yako, unaweza kumaliza changamoto yako.
 
Moja kati ya vingi ninavyo mshukuru mungu ni kunijaalia kuzaliwa na huyu mama yangu, aisee nashukuru mnoo, sababu naona wengine wanavyoteseka na wazazi wao, mzazj wa kiume alizikwa kitambo, kupitia stori nae hakuwa miyeyusho.

Kupata wazazi vivuruge ni mtihani watakuvuruga kweli kweli
Nakosa hata la kukushauri ukizingatia pepo zipo kwenye nyayo zao hatuna budi kuwanyenyekea tu, ili mradi tusiwatii katika mambo yasiyompendeza.

Jaribu kutafuta ndugu zako(wakubwa) ambao mnaivaa saana, uwaeleze jambo hili huenda wakawa na mawili matatu sababu walianza kuliona jua kabla yako, huwemda wanawajua wazazi vizuri zaidi yako.
 
Tatizo la wanawake wa Sasa wanataka kututawala kisa Hela hiyo SIYO ndoa.Mwanamke LAZIMA atawaliwe na mwanaume na UKITAKA ndoa idumu miaka mingi muoneshe mume wako ya KWAMBA unamsikiliza anachosema hapo UTAAMINI miujiza ya kuwa msikivu kwa mumewe. Ila unapojidai kuwa HUTAKI kumsikiliza mwanaume kisa vijimshahara vyako hapo inakuwa umebugi. Unateseka kwa sababu hukutaka kuonesha utiifu kwa mumewe. Sasa hivi UNATAMANI awepo mume lakini wazazi wako ndyo wamekuwa kama waume zako Sasa UTAPELEKESHWA SANA. Uache pia kuwa na gubu .Siku zote ukilikimbia zuri Baya huja umemuona mume wako hafai ngoja WAZAZI wakuonyeshe kazi watazidi kukukomoa mpaka UTAKOMOLEKA.
 
Upo mpole sana utapelekeshwa mpaka
Chumbani kwako si ufunge mlango ondoka na funguo,mim kwangu haji mtu hovyo na yeyote aje na adabu kubwa awe yeyote ,kwetu wote wananiogopa wanajua dakika moja au mbili nishavurugwa
 
Pole sana mdada wazazi wako wanakuonea wivu sijui? Maana huo sio upendo wa mzazi kwa mtoto hata kidogo,they want to take full control over you..which is not right.
Amua kitu waza kitu kustopisha all these nonsense.
 
Fanya kuomba likizo kazini. Rudi nyumbani kwa wazazi, waeleze kuwa Kuna kitu kibaya kimetokea kazini. Umesimamishwa au kufukuzwa kazi. Waambie Ni issue nyeti hawapaswi kufuatilia au kujihusisha kwa namna yoyote. Waambie ata akaunti zako umefungiwa. Kwa maana hauna chochote kwa mda huo.
Kama wapo kwa Nia nzuri na wewe utaona kwa kipindi hicho. Na ndo mda wa kujipanga na tabia tofauti na awali. Acha kuzungumzia masuala ya kazini. Ongea kwa kifupi lakini kwa kumaanisha.
Katika maisha, siku hizi watu wa karibu ndo wamekuwa chanzo katika migogoro mingi hasa kwa watumishi. Tena ukiwa ulisomeshwa imekuwa fimbo mbaya kwa wazazi na ndugu. HAWARIDHIKI
Jitaidi kuficha kipato chako. Jishushe, tafuta mme uheshimike.
 
Back
Top Bottom