Wazazi wangu wakija kwangu wanafanya maamuzi ya nini kifanyike!

Wazazi wangu wakija kwangu wanafanya maamuzi ya nini kifanyike!

Pole sana mkuu

Wavumilie tu ni wazazi wako

Pia tafuta mwanaume atakaekua ni mshauri wako mzuri na faraja yako hautokaa uhuzunike, atakushauri vizuri na pia atakufariji pale unapopitia huzuni

Nawasilisha
 
Asee, kumbe tupo wengi,
Familia za kiswahili sijui zikoje, Wazazi wanakusomesha, wanakupa kiwanja pale pale nyumbani kwao, Wanaanza kukulazimisha ujenge ilihali huna kipato, Unaamua kuondoka kwenda mbali kupambana maana wao walipokuwa na uwezo hawakukusapoti, Ukiwashirikisha kuwa kuna kibarua unataka ukajaribu babati yako wanakuvunja Moyo, tena wanawaeleza watu baki ambao hata siyo ndugu kuwa "anahangaika tu"

"Anajifanya mjanja, tumemsomesha analeta dharau, hatofika popote!.."

Sasa unajiuliza mimi ni mtoto wa kiume, naamua kwenda kupambana na maisha mbali huko, nyuma unasikia kwa watu wazazi wakikusema vibaya,.....
 
Kwa nafasi uliyo nayo n ngumu kufanya au kupata huo uhuru na control yko binafsi kwa sbb moja ty huna mwanaume ambae watu wakiwa wnkuja kwko wnjua kbx pale Kuna mwanaume.
Kwaio kitu Cha kfnya ulshkosea toka mwanzo inwezekana ulkua na kbur kwa jmaa kw sbb una mzd kipato au hkumpa uongoz mty wako pia mybe ulkua unwapa economic status ya mmeo wzaz wako wakaon n foolish kwko.
Kwaio xx Ili hiyo istokee tena tafta men olewa au hta kma kmrdia yule up to u alafu mpe uongozi km mwanaume hamia kwake hata kma umejenga uanze upya n ngumu mwanamk kusimama pkeake hata angemiliki millions of dollars[emoji120][emoji120]
Uzi ufungwe
 
Sijui kwa nini nimekuonea huruma sana niliposoma andiko hili. Inaonekana wazazi wako ni aina ya wazazi ambao ni controlling sana, they like and enjoy to take charge na ku control maisha ya watoto wao. Inawezekana pia wao wamechangia kwa kiasi fulani ndoa yako kupata matatizo na kuvunjika. Inawezekana pia ndio sababu hata ndugu zako uliozaliwa nao wamejiweka mbali nao kwa sababu wanajua kuwa wazazi wao ni watu wa aina gani, hivyo wamechagua kuwaweka mbali wabaki tu kama wazazi, kuwahudumia hapa na pale na kuwatembelea hapa na pale na kuwapigia simu, na sio kuwaweka karibu kiundani kama unavyofanya wewe.
Inaonekana wewe either umechelewa kugundua hilo, au unalijua ila una huruma sana hivyo unashindwa kufanya lolote, na wao wanajua kabisa hiyo weakness yako na wanatembea nayo hiyo hiyo (ndio tabia ya watu ambao ni controlling).
Ushauri:
Je, unaweza kuhama huo mkoa uliopo sasa ambao pia wazazi wako wapo? Kama ni wajiriwa, unaweza kuomba uhamisho kazini kwako ukahamia mkoa mwingine? Kama ndio, fanya hivyo, anza process za uhamisho uhame mkoa kwa kisingizio chochote kile, na ukikamilisha uwaage uwaambia umepata uhamisho inabidi uhame, itakua ni hatua muhimu sana kwako katika safari ya kuondoa hiyo control. Kama ofisi yenu suala la kuhama mkoa haliwezekani, basi pia angalia uwezekano wa kutafuta kazi ofisi nyingine ambayo itakua nje ya mkoa ulioko sasa na wazazi wako.
Unawajua waha wewe?labda ahamie mbinguni
 
Habari wanajamvi,

Kwa muda sasa kuna jambo limekua linaniumiza na nimekosa pa kuliongelea kwa uhuru ila naamini humu nitapata hekima na busara zangu.

Kama ilivyo ndoto ya kila mzazi anaesomesha mtoto ni ili mtoto ajisimamie na awe msaada kwa wazazi na nduguze baadae. Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwangu nimesomeshwa vizuri na nimepata kazi nzuri ambau=yo imeniwezesha kufanya makubwa kwetu ikiwemo kumaliza ujenzi wa nyumba ya wazazi , kuwakatia bima na kuhakikisha wanapata matumizi yao ya kila mwezi kwa kifupi wanaishi maisha comfortable.

Wakati huo pia na mimi kama binti najiendeleza kimaisha maana tayari nina familia japo mwezangu palitokea mgogoro tukatengena.

Shida ipo hivi: Tangu nimeachana na mwenzangu ( kiukweli hakuna aneingia kwenye ndoa achane japo matatizo mengine hayavumiliki) ni kama wazazi wangu ni kitu walichokua wanakitaka maana wana access na mimi na wana nicontrol kama wanavyotaka jambo ambalo kwangu halijakaa sawa kuwaambia siwezi ila mimi pia kama mtu mwenye mji wangu kuna mambo ambayo naamini nimeyavuka nje ya control ya wazazi.

Kwa mfano bi mkubwa akija kwangu bila kuuliza ataingia kabatini na kuvaa nguo zangu magauni, kanga etc sioni kama limekaa sawa japo sisemi. Akija pia nakua sina uhuru na kwangu atapanga kila kitu tuleje, tuishije etc na sio mara moja nimesharudi toka kazini nikakuta sijawekewa chakula nyumbni kwangu mwenyewe mama akiwepo!!

Ikiwa nimepata la deal kazini na bi mkubwa akajua ataniambia nisipeleke pesa kwenye ujenzi bali niwape wao waweke kwenye biashara au watatue issue fulani( ikumbukwe hapo mimi huwapa pesa kila mwezi atleast 200k ama zaidi wakati mwingine mbali na kununua mahitaji, umeme etc) .Ikumbuke issue nyingine za kifamilia misiba, shuhuli etc nimebeba mie japo pia ninao ndugu wengine ila mimi ndio 70% wengine hizo zilizo baki.

Kiuhalisia mbali na kuwahudumia na mimi lazima maisha yaendelee tayari nina mji wangu, kuna wakati alininunia alipojua nimepata hela sijamuambia nikapeleka site. Bi mkubwa ameenda mbali zaidi akija hapa nyumbani hujenga mazoea na watu kiasi kwamba muda wote unakuta nyumba ina watu wengine hata siwafahamu na sio ndugu kitu ambacho sio sawa kwa usalama na privacy. ( Mfano wauza mboga, mara fundi cherehani mara watu wasaluni yani wote atataka awazoeeee kupitiliza)

Najitahidi sana wakija wazazi friji ipendeze na jikoni pawe vizuri wale wanachopenda ila atakula kisha atasema kabisa sijaridhika ikumbukwe yeye ndo ameamua kipikwe nini!! Hapo nitamuuliza nipike nini tena angalau afurahie.....daaaaah naumia kuna wakati mzee alikuja napika chakula saa ingine hagusi au anakula kidogo kisha anamwambia bi mkubwa sijala hapo ntapigiwa simu nisemweeee. Yani wakati mwingine najifungia ndani nalia tu.

Najua kwa baadhi sitaeleweka ila kuna pattern niiliisoma nikaumia kwamba kwa namna fulani huenda shida katika nyumba yangu ilisababishwa na wao kwasabau kwa bahati mbaya yule mwenzangu hakua vizuri sana kwa hiyo ni kama waliona hawanifaidi vya kutosha kwa hivyo kwa namna fulani hivi nilivyo kwao ni fursa.
Najua wengi mnaweza kunisema ila pia ni kitu nimekaa nacho zaidi ya miaka mili kinanisumbua. Naomba mnisaidie naishije ama nafanyaje?

Naomba mnisamehe kwa nitakao wakwaza au kuwaumiza na kuona sina shukrani kwa wazi ila kwa kwli najitahidi sana ila kuna namna fulani naumizwa pia.
Tafuta kidume wewe alafu hamia kwa kidume. Hawawezi kukusumbua tena
 
Asee, kumbe tupo wengi,
Familia za kiswahili sijui zikoje, Wazazi wanakusomesha, wanakupa kiwanja pale pale nyumbani kwao, Wanaanza kukulazimisha ujenge ilihali huna kipato, Unaamua kuondoka kwenda mbali kupambana maana wao walipokuwa na uwezo hawakukusapoti, Ukiwashirikisha kuwa kuna kibarua unataka ukajaribu babati yako wanakuvunja Moyo, tena wanawaeleza watu baki ambao hata siyo ndugu kuwa "anahangaika tu"

"Anajifanya mjanja, tumemsomesha analeta dharau, hatofika popote!.."

Sasa unajiuliza mimi ni mtoto wa kiume, naamua kwenda kupambana na maisha mbali huko, nyuma unasikia kwa watu wazazi wakikusema vibaya,.....
Tupo wengi mkuu

Mimi nilitaka kuendelea na Chuo nikawashirikisha wazee wangu yaan nilichojibiwa sikutegemea nikaulizwa unataka ukasome wapi na Chuo gan na course gan? nikajibu nikaambiwa kwanini usiende kusoma Chuo fulan course fulan? na huko unataka kwenda kusoma hatupataki nikashikwa bumbuwazi nikajiuliza nasoma Mimi au wanasoma wao? nikauliza kwanin..? nikaambiwa hakuna kwenda wewe endelea kufanya kazi tu hapa hapa huko unakotaka kwenda kusoma usiende kusoma sisi ni wazazi wako tumeshasema hatutaki ukasomee hio course na huko unakotaka kwenda kusoma hatutaki uende kusoma uko

Nikaacha kwenda ingawa niliishaanza process za kuapply, wazazi waangu walinikataza nisiendelee kusoma nifanye kazi tu
 
Mi nilimwambia mama nimefukuzwa kazi

Nikapunguza baadhi ya karaha, sijui Kwa nini baadhi ya wamama hufanya hivi hasa Kwa watoto wa kike

Hizi case nimekutana nazo nyingi, yupo tayari akusemee mbovu Kwa mwenzio kama anaona hana maslahi nae ili tu mfarakane ale pesa zako mwenyewe.[emoji20]
 
Mambo 2 ufanye uwambie wazaz hupendezw na wanayoyafanya au uwolewe ten na mwanaume awe kiongoz wa nyumba izo tabu zote utasahau
 
Wazazi wengi wa sasa ni pasua kichwa,
Nakushauri wavumilie tu cha msingi anza kuwabana wasipate nafasi ya kuja kwako
 
Dada una moyo mzuri unapenda sana wazazi wako.....wazazi wengi wanaamini wakiwa na watoto wa kike ni uwekezaji sababu hamsaahau nyumbani kama wewe. ......ila sasaivi unahitaji kujiongeza usiwaambie kitu najua hata ukiwaambia utajisumbua tuu......ANZA KUIGIZA SEHEMU YA KAZINI IMEYUMBA KIUCHUMI. NA WEWE UNAANZA KUFULIA MSHAHARA MNAPEWA NUSU HATA UFOJI BARUA ZA KAZINI ZA UONGO, IKIWEZEKANA UNAWAOMBA HATA USHAURI UTAFUTE KAZI MAHALA PENGINE .PUNGUZA HELA YA MWEZI UNAYOWATUMIA ,UTAONA RANGI ZAO LAKINI VUMILIA.....daah kiufupi usipotumia akili hutoki hapo
 
Asee, kumbe tupo wengi,
Familia za kiswahili sijui zikoje, Wazazi wanakusomesha, wanakupa kiwanja pale pale nyumbani kwao, Wanaanza kukulazimisha ujenge ilihali huna kipato, Unaamua kuondoka kwenda mbali kupambana maana wao walipokuwa na uwezo hawakukusapoti, Ukiwashirikisha kuwa kuna kibarua unataka ukajaribu babati yako wanakuvunja Moyo, tena wanawaeleza watu baki ambao hata siyo ndugu kuwa "anahangaika tu"

"Anajifanya mjanja, tumemsomesha analeta dharau, hatofika popote!.."

Sasa unajiuliza mimi ni mtoto wa kiume, naamua kwenda kupambana na maisha mbali huko, nyuma unasikia kwa watu wazazi wakikusema vibaya,.....
Najua ni ngumu kuamini lakini wazazi wa dizaini hiyo behind the scene huwa ni washirikina na wanamaagano yao either mtoto fulani au wote wasiwe mbali na himaya yao. Pambana it seems unakitu kikubwa ndani yako ambacho katika ulimwengu wa giza wanakihofia
 
Pole sana.
Mtoto kwa mama hakui, ila nakushauri punguza mazoea, ukaribu uliopitiliza na Mama yako.
Imeandikwa mtu atamuacha baba na Mama yake.... (Acha kufuatana na wazazi wako kila wakati, wakutembelee na waondoke kama wageni wengine..)
Chumba chako funga na jaribu kumueleza Mama yako mipaka yako ukiwa nyumbani kwako!! Maamuzi ya jikoni ni ya kwako pia, mama yako hawezi kukupangia cha kupika, labda kumshirikisha tu ili kuwaandalia wanachokipenda, wasiporidhika hilo sio tatizo lako!!
Pia jaribu kupunguza kumwambia mama yako mambo yako, wewe ni mtu mzima sasa na ishi maisha yako, coz wazazi wako wameishi/wanaishi maisha yao!!

Nimejaribu kuhisi pia huenda mwenzako alikuwa anakwazwa na tabia za wzaazi wako ndio maana akaamua kusepa zake!!

Maadamu unajiweza kiuchumi jitafakari na chukua hatua.

Kila la kheri!
 
Nawashukuru sana wotee ambao mmechukua muda wenu kusoma na kunishauri , nawashukuru mno na hekima na busara zenu zimenipa mwanga kwa namna fulani. Toka jana moyo wangu umekua mzito mno kuna wakati najifungia ndani nalia ili nipate relief maana naogopa hata kusema kwa ndugu zangu.
Kuna wakati ndugu yangu alimtambulisha mchumba wake wakawa wanawasiliana matokeo yale mama siku nyingine akawa anaomba hela kwa huyu mchumba hilo jambo lilituumiza sana ila ndugu yangu alipata ujasiri wa kumwambia kua hapendi hiyo tabia.
Kwa wale mliosema mimi naonekana nina gubu ama jeuri kwa wanaume...naomba kuwaambia sipo hivyo nipo tofauti kabisa. Ni aina ya mwanamke ambae naweza kumpa mwanaume kadi yangu ya benki ili tu asijione mnyonge endapo mambo yake hayajakaa sawa, naweza kununua au kufanya kitu kwa hela yangu ila nikiulizwa nitasema mume ndio amefanya.... ni mtu wa kumfichia aibu mwenzangu( nisingependa kumuongelea sana kwasabau sio jambo la msingi kwa mada yangu hii)
Hayo niliyoeleza ni mambo machache kati ya mengi ambayo napitia .
Kuna wakati ilifika nikadhamiria kuacha kazi kwasababu kazi nzuri niliyoipata nikategemea itakua baraka kwangu na kwa familia yangu imegeuka huzuni. Sijawahi ku disclos nalipwa kiasi gani ila sijui ni kwa namna gani walifahamu kwa hiyo kuna wakati wanapoomba wanataka uwape walichotaja sio ulichonacho wewe. Anyways ni mambo mengi lakini nashukuru nimepata nguvu ya kushare haya machache na nyinyi na mkaweza kunishauri, nimepokea kwa mikono miwili na Mungu awabariki.
Kwa mlionifuata PM pia asanteni kwa kuguswa na jambo langu na kunishauri na shukuru pia kwa mnaoniombea. Mwisho wa yote nawatakia baraka, furaha na amani katika maisha yenu.
Suzieq
 
Suala lako ni wewe tu ndo umeshindwa kujisimamia, kiuhalisia mwanamke yoyote ambae anaishi na mwanaume lakini mwanaume huyo akahisi final say na watoa maamuzi ni wazazi wako lazima tu atasepa yaani piga ua, halafu wewe pia ulishindwa kujifunza kwa ndugu zako na pia mama yako ana tabia mbovu za kiswahili kwenye jamiii nyingine na makabila mengine unaweza kumaliza hata miezi hujaongea na mama mkwe coz kuna ile heshima yake kabisa ila yeye anapiga simu na kuomba hela bila aibu kbsa, Sasa ili utoke hapo na kweny hiyo hali yako una option mbili tu, Kujisimamia effectively japo sijui kama utaweza au umtafute mwanaume mtata ila alie vizuri kichwani then mpe nafasi kama mume na msikilizane nyie wawili tu atakusaidia kuwanyoosha hao wazazi wako
 
Ikiwa nimepata la deal kazini na bi mkubwa akajua ataniambia nisipeleke pesa kwenye ujenzi bali niwape wao waweke kwenye biashara au watatue issue fulani
Kwa issue hii kosa ni lako mwenyewe. Banisha kimya kabisa (kwa vile umeshajua hiyo ndiyo tabia ya mzazi wako).
Jitahidi uendeleze jengo lako hata akipiga kelele au akinuna, wewe la muhimu usimjibu lakini endelea na shughuli zako.

Ukiwa na msimamo hawatakuyumbisha, najua watanuna lakini endelea na msimamo wako. Utakuja jikuta umezeeka na wala hujajiendeleza na cho chote.
 
Pole sana mami unapatikana mkoa gani tuyajenge me niko moshi apa
 
Back
Top Bottom