Wazazi wengi wa Mtwara wana tabia ya kubadilisha majina ya watoto kisa talaka

Wazazi wengi wa Mtwara wana tabia ya kubadilisha majina ya watoto kisa talaka

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Zaidi ya asilimia 70 ya wazazi Wilaya ya Mtwara huenda wakakosa haki za watoto wao kutokana na tabia ya kubadilisha majina ya watoto kwenye vyeti vya kuzaliwa, sababu ikitajwa kuwa ni talaka.

Akizungumza Oktoba 31 katika kampeni ya kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa katika Wilaya ya Mtwara inaoyoendeshwa na Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA), mkazi wa Magomeni mkoani humo, Zuhura Mrisho amesema kuwa talaka zimekuwa chanzo cha wengi kubadilisha majina ya baba kwenye vyeti vya watoto wao.

“Mwanangu simbadilishi jina hata baba yake akiniacha hata asipojali watoto atabaki kuwa baba tu.

“Nimeachana na mume wangu hataki hata kuwaona watoto, lakini nawasisitiza watoto kuwa yule ndiye baba yao pekee. Acheni kuwabadilishia watoto majina ya baba zao,” amesema.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya hiyo, Dunstan Kyobya amesema kuwa wazazi wengi wanakuwa hawana majina sahihi ya watoto wao na kulazimika kubadili mara kwa mara hatua inayowalazimisha kutoa elimu hii.

Amesema kuwa mtoto anatakiwa kuwa na majina sahihi baada ya kuzaliwa ili kuepuka changamoto ya kubadilisha majina.

“Asilimai 70 wanakuja kubadilisha majina ya watoto wao mtoto wakati anaanza darasa la kwanza, akiwa na jina lingine sekondari jina lingine eti limekosewa na chuo lingine.

“Ndio maana tunatoa elimu na kuanzisha kampeni. Tutapita shule kwa shule ili kutoa elimu kwa wananchi wote kwa wingi wa watoto hawa elimu itasambaa zaidi,” amesema Kyobya.

Naye Mratibu wa Vizazi na Vifo Mkoa wa Mtwara, William Felix amesema kuwa wapo wanaokuja kutaka kubadilishha majina hadi ya wazazi wao kwenye vyeti vya kuzaliwa.

“Wengi wanabadilsiha majina yao kwa maana ya herufi wapo wanaotaka kubadilisha ya mama na baba, lakini sheria hairuhusu hata kama wamegombana. Wengi wanakuja na hiyo kesi lakini wakitoa taarifa zao tunawabaini.

“Wengi hawana vyeti ni changamoto wapo wanaotaka kubadili mwaka lakini hatubadili mwaka na siyo utaratibu.

“Wapo wengine wana vyeti lakini wanasema hawana, ukiingiza kwenye mfumo unawakuta yaani majina ya wazazi. Hivyo wyake," amesisitiza Felix.

Chanzo: Mwananchi
 
Wanajielewa sana tena sana. Kwa Mtwara, mtoto ni mali ya ujombani, ndiyo maana hata mahari anapokea mjomba. Hiyo ndizo mila zao, huwezi kuzibadilisha kwa Rita. Definitely it sounds awkward, but that's it! Ni mila zao na wanaziheshimu.
Mkuu Serikali ya Tanzania haifati sheria za kimila, ndiyo mana ukisoma hiyo taarifa ya juu walioenda kubadili majina au umri wameshindwa na sheria ya nchi haisemi Mtoto mzazi wake ni Mama na mjomba wake.
 
Mmesahau kama jamii za Wamakonde ni miongoni mwa Matrilinieal societies,mtoto ni familia ya ujombani, haiwezekani 70% wamebadili majina kisa ndoa. Hapana hizo ni athari za mifumo ya yao(matriliel)
 
Wanajielewa sana tena sana. Kwa Mtwara, mtoto ni mali ya ujombani, ndiyo maana hata mahari anapokea mjomba. Hiyo ndizo mila zao, huwezi kuzibadilisha kwa Rita. Definitely it sounds awkward, but that's it! Ni mila zao na wanaziheshimu.
Basi kama mila na desturi tukizifuata na Wakurya waruhusiwe kukeketa.Kubadilisha ubini halisi wa watoto kihuni ni umalaya wa tabia. Hata wakiachana uzao haubadiliki. Waache ujinga.
 
Wanajielewa sana tena sana. Kwa Mtwara, mtoto ni mali ya ujombani, ndiyo maana hata mahari anapokea mjomba. Hiyo ndizo mila zao, huwezi kuzibadilisha kwa Rita. Definitely it sounds awkward, but that's it! Ni mila zao na wanaziheshimu.
Weeeeh bhana eeeeh sasa unabadilisha jina hili iweje? na uliyezaa nae mlifunga ndoa,

Kuhusu mtoto ni mali ujombani mie najua kwa wale waliozaliwa na mababa wasioeleweka hata ubini wanatumia wa ujombani,

Coz nina watu wa karibu waliozaliwa kwa masingo maza wanatumia ubini wa kwa mama, hiyo inatumika sana huku kusini.
 
Mkuu Serikali ya Tanzania haifati sheria za kimila, ndiyo mana ukisoma hiyo taarifa ya juu walioenda kubadili majina au umri wameshindwa na sheria ya nchi haisemi Mtoto mzazi wake ni Mama na mjomba wake.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] eti mama na mjomba wake.
 
Weeeeh bhana eeeeh sasa unabadilisha jina hili iweje? na uliyezaa nae mlifunga ndoa,

Kuhusu mtoto ni mali ujombani mie najua kwa wale waliozaliwa na mababa wasioeleweka hata ubini wanatumia wa ujombani,

Coz nina watu wa karibu waliozaliwa kwa masingo maza wanatumia ubini wa kwa mama, hiyo inatumika sana huku kusini.
Kwa mtoto ambaye baba haeleweki au mimba ilikataliwa lazima awe upande wa mama, duniani kote.
 
Kwa mtoto ambaye baba haeleweki au mimba ilikataliwa lazima awe upande wa mama, duniani kote.
Kwa huko mtwara best hata kama baba anaeleweka kama tu haujafunga ndoa mtoto ni wa ujombani
 
Sasa ataendaje Sekondari kwa jina tofauti na alilofanyia Darasa la 7?

Ataendaje chuo na jina tofauti na alilofanyia sekondari?

Kwanini RITA wabadilishe jina la Baba? Je hawaoni RITA ndo tatizo?
 
Hawa waliopewa dhamana wana wafanye uchunguzi tena. Kuwaanika watu wengi mfano jamii nzima unaifedhehesha kwenye public, si vizuri.

Hivi ni kweli 70% inabadilisha majina ya watoto wao kwa sababu za kitalaka?
Mkoa wa Mtwara ninavyoujua mimi, jando na unyago ndo vinabadilisha majina ya watoto. Tena sio 70% ni 99.99%
Mtoto anaenda jandoni na jina fulani, anarudi na jina lingine.
Na kwa sasa wamakonde wanafanya hayo kabla mtoto hajaingia shule ya msingi kuepuka usumbufu huo wa kubadilisha majina.

Hizo sababu zilizotolewa na kina Zuhura na Dunstan na Felix, zinatia ukakasi.
Hata wale watoto ambao wamekataliwa na baba zao, hawawezi kufikia 70% kwa sababu wengi wao wanakataliwa mimba au muda mfupi baada ya kuzaliwa kwa hiyo shuleni wanaenda na majina yaliyokubaliwa na jamii. Kwa sio wengi watakaobadili majina. Eti shule ya msingi jina lingine, sekondari lingine na chuo lingine. Hii taarifa kama inawasimanga ndugu zetu wamakonde. Bhaaaa.!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom