Wazee Bukoba: Kumaliza udhia, makelele ya kutaka Mkoa, Geita sasa iitwe mkoa wa Chato

Wazee Bukoba: Kumaliza udhia, makelele ya kutaka Mkoa, Geita sasa iitwe mkoa wa Chato

Hapo inabidi Geita,Simiyu,Mwanza,Shinyanga, na Chato ifanyiwe reshuffle itokee mikoa 3 tu maana Geita mkoa mpya tena ugawanywe wakati kuna mikoa mikubwa kijiografia kama Tabora au Morogoro haijagawanywa miaka 60 ya uhuru sasa!!

Embu tuwe serious,
Sasa kama wanataka kugawanywa siwaombe mbona wenzao wa Pwani wameomba juzi mkoa ugawanywe, kama serikali ya majimbo haiwezekani basi mikoa mipya italeta maendeleo na ajira kwa wingi kama mikoa iliyogawanywa ilivyosogezewa maendeleo na ajira zikapatikana.
 
Sasa kama wanataka kugawanywa siwaombe mbona wenzao wa Pwani wameomba juzi mkoa ugawanywe, kama serikali ya majimbo haiwezekani basi mikoa mipya italeta maendeleo na ajira kwa wingi kama mikoa iliyogawanywa ilivyosogezewa maendeleo na ajira zikapatikana.
Maendeleo hayaji kwa kuongeza idadi ya mikoa walau ungesema devolution kupitia halmashauri ziongezwe vyanzo vya mapato kutoka serikali kuu ili kuweza kusimamia masuala mengi ya maendeleo wenyewe hapo kidogo ndio tutapiga hatua.

Ila kila siku tunaona halmashauri zinaporwa mamlaka na mapato hku mfuko mkuu wa serikali ukinenepa, matumizi yanapangwa Dodoma unadhani vipaumbele vya wananchi wa kijiji cha salama B huko Mugumu vitapata ahueni yoyote??

Suluhu ni devolution kama inavyosuggestiwa na Sera ya majimbo CHADEMA. Maendeleo yatafika kwa haraka kwa kila jimbo kufocus kwenye vipaumbele na comparative advantage zake.
 
Kiukweli Chato haitakiwi kuwa mkoa hilo wala halihitaji shahada liko wazi. Enzi za ibilisi joka kuu zimepita.
Unavijua vigezo vinavyotumika kupata mkoa mpya? au unapinga tu kwa chuki!!
 
Dodoma kutangazwa jiji bado huwa cpati majibu.
Ok sheria ilikuwa inamruhusu,vikao vya madiwani kuomba jiji vilifanyika nakufuata taratibu zote?
Na angekuwa hai tungekuwa na Katibu kiongozi Bashiru
 
Inayo sifa kutokana na vigezo vinavyotumika kupata mkoa mpya kama hujui vigezo sema tukuambie halafu upime mwenyewe kama Chato inafaa kuwa mkoa.
Haina, acheni kulazimisha mambo yasiyowezekana.
 
Kiukweli Chato haitakiwi kuwa mkoa hilo wala halihitaji shahada liko wazi. Enzi za ibilisi joka kuu zimepita.
Toa sababu na si kupinga tu bila sababu. Kuna vigezo vinavyotumika vya uanzishwaji mkoa mpya na si kuamua tu. Kwa kumjibu wa mwongozo wa TAMISEMI wa mwaka 2014, vigezo vya kuzingatia katika kuanzisha mkoa ni pamoja na kuwa na ukubwa wa eneo lenye kilomita za mraba usiopungua 20,000. Pia kuwa na wilaya nne, idadi ya watu isiyopungua asilimia tatu ya idadi ya kitaifa, tarafa zisizopungua 15, idadi ya kata zisizopungua 45 na idadi ya vijiji visiopungua 150. Mkoa mpya wa Chato utakuwa na tarafa 18, kata 87, vijiji 360 huku ukiwa na ukubwa wa eneo la kilomita za mraba 30,215, lenye watu zaidi ya milioni moja laki tano.
 
Toa sababu na si kupinga tu bila sababu. Kuna vigezo vinavyotumika vya uanzishwaji mkoa mpya na si kuamua tu. Kwa kumjibu wa mwongozo wa TAMISEMI wa mwaka 2014, vigezo vya kuzingatia katika kuanzisha mkoa ni pamoja na kuwa na ukubwa wa eneo lenye kilomita za mraba usiopungua 20,000. Pia kuwa na wilaya nne, idadi ya watu isiyopungua asilimia tatu ya idadi ya kitaifa, tarafa zisizopungua 15, idadi ya kata zisizopungua 45 na idadi ya vijiji visiopungua 150. Mkoa mpya wa Chato utakuwa na tarafa 18, kata 87, vijiji 360 huku ukiwa na ukubwa wa eneo la kilomita za mraba 30,215, lenye watu zaidi ya milioni moja laki tano.
Kama hivyo ndio vigezo, nadhani Morogoro, Tanga, Tabora kila mkoa ungezaa sio chini ya mikoa mitatu.

Swali linarudi pale pale, kama wilaya ya Chato ina vigezo vyote hivyo, kwanini imege tena wilaya za mkoa wa Geita, Kagera na Kigoma ili kuundwa mkoa?

Kwanini Biharamuro/Ngara/Kakonko isiwe mkoa na Chato kuwa wilaya katika mkoa mpya wa Biharamuro/Ngara/Kakonko?

Kwanini tuimege wilaya ya Chato kutoka katika mkoa mdogo wa Geita ili tu kuifanya Chato kuwa mkoa?
 
Halafu tunawalaumu wakoloni kwa kutugawa Waafrika na mipaka wakati sisi wenyewe tu tunapenda kujigawa hovyo bila kuzingatia mila na historia ya eneo na wahusika.
 
Na kwenye documents tunabadilisha taarifa? Kuna watu walizaliwa wilaya ya Babati mkoa wa Arusha wakati huo kabla haujamegwa kuunda mkoa wa Manyara ambao Babati ndio mji mkuu. Hii kugawa gawa mikoa inavuruga taarifa za watu. Kama ni maendeleo yanaweza kuja pasipo kugawa ikabuniwa namna nyingine. Kila wilaya iwe na mji mkuu wake na maendeleo yasogezwe hapo. Kama wilaya ni kubwa igawanywe na siyo kuunda mkoa mpya. Mf South Mara and North Mara au Handeni A na B
 
Huu ndio ukabila alioutaka Magufuli.
Mwalimu alisema kiongozi mkabila karne hii ni mufilisi kichwani.
Wahaya ni wakabila hasaa, ukitaka nenda Bukoba makao makuu ya mkoa ujionee jinsi mkoa unaopakana na nchi landlocked ya Uganda ilivyo Nyuma kimaendwleo.
Bado mjini Kati wanapanda migomba na kufuga mbuzi na kondoo. Hawachangamani, mafukara,majigambo na mengine mengi yafananayo na hayo.
 
Toa sababu na si kupinga tu bila sababu. Kuna vigezo vinavyotumika vya uanzishwaji mkoa mpya na si kuamua tu. Kwa kumjibu wa mwongozo wa TAMISEMI wa mwaka 2014, vigezo vya kuzingatia katika kuanzisha mkoa ni pamoja na kuwa na ukubwa wa eneo lenye kilomita za mraba usiopungua 20,000. Pia kuwa na wilaya nne, idadi ya watu isiyopungua asilimia tatu ya idadi ya kitaifa, tarafa zisizopungua 15, idadi ya kata zisizopungua 45 na idadi ya vijiji visiopungua 150. Mkoa mpya wa Chato utakuwa na tarafa 18, kata 87, vijiji 360 huku ukiwa na ukubwa wa eneo la kilomita za mraba 30,215, lenye watu zaidi ya milioni moja laki tano.
Kwa mara ya kwanza tokea sakata hili la mkoa waChato kuibuka, ndo naona mtu aliye toa comment yenye mashiko.

Asante Sana.
 
Back
Top Bottom