Source07
Senior Member
- Oct 5, 2018
- 196
- 353
Heshima kwenu wapenzi wafatiliaji wamichezo na wanamichezo kwa ujumla!
Moja kwa Moja niende kwenye hoja yangu.
Hivi karibuni kama wiki3 zilizopita tulishuhudia kuona uliyokua uwanja wa Taifa ukibadilishwa jina kwa ajili ya kumuenzi Hayati BMW kwa Amri ya Mh. Rais hivyo uwanja huo ukaitwa Benjamin Mkapa Stadium! Sawa haina tatizo kabsa ila sasa nilichokita tukijadili hapa nihiki nilichokisoma kwenye mitandao yakijamii haswa page za Wasafi wakitangaza show za wasanii wao zitakazo fanyika Kahama, katika maelezo yao wanasema uwanja wa Kahama ndio uwanja wa Taifa. Kahama National Stadium, yaani hadhi uliyokua nao uwanja wa Taifa kabla kubadilishwa jina leo hadhi imepewa uwanja wa Kahama. Sawa hakuna neno ila, je Kahama stadium ina kidhi vigezo vyakuitwa Uwanja wa Taifa?
Nakama hili ndio mbona TFF hakuutangaza huu uwanja kua ndio uwanja wetu wataifa kwa sasa, au hata serikali kupitia waizara ya Michezo mbona hawauutangaza uwanja huu kua ni waTaifa? Hawa Wasafi wametoa wapi mandate ya kuita huu uwanja wakahama kua ndio NATIONAL STADIUM!
Ifahamike kua uwanja kuitwa au kuwa ni uwanja wa Taifa ina maana kua mechi zetu zote zitakazo kua zinajumuisha mechi za mataifa mengine haswa zile zilizo kwenye calendar ya FIFA zitachezwa hapo, so wanataka kusema sasa tutakua tunaishuhudia Taifa Stars akicheza Kahama, kucheza huko haina shida ila, je Kahama stadium ina hadhi kweli yakuitwa KAHAMA NATIONAL STADIUM?
Na kingine toka ule uwanja umebadilishwa jina kweli hadhi yake imeshuka Sana kiasi yakwamba husikii Tena ukiitwa uwanja wa Taifa kwanini? Je, kuubadilisha jina ndio kumeathiri mpaka hadhi ya ule uwanja uliyokua nayo hapo mwanzo? Kuna shida gani tukauita Benjamini Mkapa National Stadium? Kuna shida gani, maana sasa hata ukiingia getini unakuta tu jina ni BENJAMIN MKAPA STADIUM au ndio kusema kubadilishwa kwa jina ndio kumeathiri moja kwa moja kuitwa uwanja wa Taifa?
Nimelileta kwenu hili wadau tulijadili kwa mapana sana, au labda nimimi uwelewa wangu mdogo naamini humu wapo manguli watanisahihisha!
Naomba kuwasilisha!
Moja kwa Moja niende kwenye hoja yangu.
Hivi karibuni kama wiki3 zilizopita tulishuhudia kuona uliyokua uwanja wa Taifa ukibadilishwa jina kwa ajili ya kumuenzi Hayati BMW kwa Amri ya Mh. Rais hivyo uwanja huo ukaitwa Benjamin Mkapa Stadium! Sawa haina tatizo kabsa ila sasa nilichokita tukijadili hapa nihiki nilichokisoma kwenye mitandao yakijamii haswa page za Wasafi wakitangaza show za wasanii wao zitakazo fanyika Kahama, katika maelezo yao wanasema uwanja wa Kahama ndio uwanja wa Taifa. Kahama National Stadium, yaani hadhi uliyokua nao uwanja wa Taifa kabla kubadilishwa jina leo hadhi imepewa uwanja wa Kahama. Sawa hakuna neno ila, je Kahama stadium ina kidhi vigezo vyakuitwa Uwanja wa Taifa?
Nakama hili ndio mbona TFF hakuutangaza huu uwanja kua ndio uwanja wetu wataifa kwa sasa, au hata serikali kupitia waizara ya Michezo mbona hawauutangaza uwanja huu kua ni waTaifa? Hawa Wasafi wametoa wapi mandate ya kuita huu uwanja wakahama kua ndio NATIONAL STADIUM!
Ifahamike kua uwanja kuitwa au kuwa ni uwanja wa Taifa ina maana kua mechi zetu zote zitakazo kua zinajumuisha mechi za mataifa mengine haswa zile zilizo kwenye calendar ya FIFA zitachezwa hapo, so wanataka kusema sasa tutakua tunaishuhudia Taifa Stars akicheza Kahama, kucheza huko haina shida ila, je Kahama stadium ina hadhi kweli yakuitwa KAHAMA NATIONAL STADIUM?
Na kingine toka ule uwanja umebadilishwa jina kweli hadhi yake imeshuka Sana kiasi yakwamba husikii Tena ukiitwa uwanja wa Taifa kwanini? Je, kuubadilisha jina ndio kumeathiri mpaka hadhi ya ule uwanja uliyokua nayo hapo mwanzo? Kuna shida gani tukauita Benjamini Mkapa National Stadium? Kuna shida gani, maana sasa hata ukiingia getini unakuta tu jina ni BENJAMIN MKAPA STADIUM au ndio kusema kubadilishwa kwa jina ndio kumeathiri moja kwa moja kuitwa uwanja wa Taifa?
Nimelileta kwenu hili wadau tulijadili kwa mapana sana, au labda nimimi uwelewa wangu mdogo naamini humu wapo manguli watanisahihisha!
Naomba kuwasilisha!