Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Kuna jamaa mwingine anaendesha Dar express ile ya Nairobi.

Nilikuwa napanda wakati ule kabla ya Corona.

Jamaa anajua kucheza na muda, hata mchelewe vipi kuondoka arusha. Muda wa kufika Shekilango haupishani kwa zaidi ya dk 5.
 
Inategemea na chombo ulicho nacho, barabara ilivyo pia. Kama imenyooka na umeisha ona zaidi ya 2 km.. nyeupe haina kitu, hata kama 10.. unazikusanya, ila kama huoni zaidi ya 1 km.. na road ina kona. Ni vyema uwe mpole
barabarani kuna changamoto sana.... siku natoka Dar to Arusha, nikiwa baada ya kutoka msata nafikiri mbele kulikuwa na gari ya mzigo na nyuma yake kluger then Mimi, sasa nikaona sehemu imenyooka safi na inaruhusu kuovertake nikatoa chuma, naanza kuimalizia kluger nikasikia kishindo upande wa kushoto kumbe jamaa wa kluger nae kaanza kuovertake hata bila kuangalia sijui alikuwa anawaza nini... nikacheza na chuma vizuri nikaenda kusimama mbele baada la kulipita na roli, jamaa nae sijaja akasimama anatetemeka balaa, kukagua gari pale alikuwa ameipiga kidogo mlango wa nyuma... ila nikamsihi tu awe makini .... kama upo humu utakuwa unakumbuka ni mwaka Jana mwezi 8/9 hivi...
 
Bora umempa ukweli.
 
Kwamba safari nzima anatembea less than 50kph?! Duh mlifika saa ngapi?
 
Huwa tunajitahidi kupunguza, maana unaweza sababishiwa na mtu au hata chombo yenyewe. Basi Mungu hutulinda. Mie leo Scania lili fail naliona hilo nyuma yangu... dah! Uamuzi niliochukua ghafla ni kuitoa gari barabarani tu. Nashukuru niliitoa salama na yeye alishukuru sana mbeleni nilimkuta kasimama
 
Sio watu wote ni wazuri kwenye matumizi ya side mirrors na rear view driving mirror. No wonder lane shifting ni moja ya vyanzo vikubwa sana vya ajali, raia wengi wanajua kukodoa mbele tu bila 'consultations' nyingine nyuma na pembeni ikiwemo.

Sent from my SM-J730F using JamiiForums mobile app
 
Kwenye baadhi ya Toyota kama Rumion, naona kuna D-S feature. Ukitaka sporty-like speed, gear lever unaiweka kulia mwa D, kwenye S. Hapa naona ndio tunapata speed kama ya OD.
Ahaa mie naionaga tu hio S sema kwenye gearbox za tiptronic!

Nadhani ni kwa ajili ya simulated manual shifting sababu kuna + na - juu na chini ya herufi S! Unaweza panga gia ya kwanza mpaka ya 5 ila ukitaka auto shifting unarudisha D
 
Jana majira ya saa 2 usiku natoka kijichi (mgeni nani) kuelekea bagamoyo kijiji kimoja kinaitwa bom ambapo kuna mtambo wa dawasco hapo. Nilikua na mitsubish pick up ( double cabin) L200 ya mwaka 95 engine 2400, alafu left hand.

Basi bhaana kufika mtongani hapo nakutana na foleni ya kizushi tu alafu malory na daladala tupu, nikafanya vifujo fujo vya kujichomeka huku na kule hatimae nikapasua foleni maana ilitakiwa saa 7 au 8 niwe nisharudi kijichi.

Sasa nimetembea kufika maeneo ya tabata pale kwenye traffick lights, kutokana na haraka nikajikuta navuka kwenye red light, hapo kulikua na IST mbele ilivuka namm nikaunga, kumbe bhana mbele kuna yange yange. Ile kuvuka tu IST akapigwa mkono namm nikapigwa mkono.

Jamaa wa ist sijui akamalizana nae vipi, sasa akaja kwangu... Kijana naomba leseni, (hapo nikakumbuka hata leseni sikuchukua kutokana na haraka) nikaanza kumpiga sound pale jamaa haelewi kakomalia leseni namimi nina haraka zangu. Basi akatoka kidogo akaenda kupiga mkono gari zingine huko, hapo ndo alipofanya kosa [emoji23].

Pembeni kulikua na bodaboda wamepack nikamwiita mmoja nikamwambia vp huyu traffic hapa ana gari au pikipiki? Akasema huyu hana usafiri. Nikamwambia mi nataka nikimbie hapa vp njia hii haina folen mbele huko? Boda anasema ukikimbia huyu askari huwa anakodi boda anakufukuza.

Nikamwambia haina noma ni naishia hapo ubungo tu, ( sikutaka kumwambia ninapoelekea maana asije nichomesha). Basi nika cheki kwa side mirror naona jamaa yuko bize anaongea na gari ya nyuma huko.

Kimoyomoyo nikasema BINGO, manina nikaifumua chuma pale nikaingia rod yaani nilikua kama niko kwenye mashindano vile nilikua napangua gia huku nafanya overtaking za hatari. Kufika pale fly over ya ubungo nilifuta kisahani hadi 180km/hr.

Chuma inanguruma yaan sikutaka hata kujisumbua na side mirro kumcheki kama jamaa anakuja au vipi, mwishoe nikafika mwenge nikakunja bagamoyo rd nikanyoosha goti.

FUNZO : Maedereva tusikubali kuonewa ki bwegebwege, ukiona chuma iko vzuri ingia road timua. Kama anataka ligi akufate. [emoji23]
 
Nimekuelewa na nimekupenda kwa herufi kubwa.
 
Nadhani ndo huyo.

Kwa sura namfahamu.

Jamaa anajua kubalance muda mpaka unafurahi mwenyewe.
Dar ~ Arusha saa 9 keshafika au saa 10 jioni mixer Babati ngoma anaunga hiyo. Sasa akipewa Dar - Nairobi utampenda hanaga shida anatembea balaa ashawahi nifikisha Arusha saa 9 kamili jioni katoka Dar saa 11 Alfajiri njia ya Bagamoyo.

Gari nzima tulikua watu 16 tu, Dar Express Chombo Scania DH.
 
Magari ya kisasa yana blindspot assist.

Kwamba gari ikiwa pembeni yako, kuna sensor ina-assume hujaliona hilo gari.

Kuna taa ina blink kwenye side mirror kukuonesha kuna gari pembeni.

Huyo wa kluger angekuwa na hiyo feature lazima alarm ingempigia kwanza kabla hajatoa gari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…