ozigizaga
JF-Expert Member
- Sep 6, 2013
- 701
- 1,703
way back 2015 au 2016 hivi mida ya saa nne kasoro usiku natoka mwenge narudi home kimara na washikaji kufika hapa mataa ya chuo kuna jamaa na hardbody akaja akaparua gari upande wa kulia na mbele tena akaparua premio... kwasababu kulikuwa na jam akasimama.... nikashuka kumfuata Ile nafika tu pale jamaa akaanza kutema mbovu pale maana alikuwa kikombe tayari, wenzio wamekaa kimya tu. taa zikaruhusu jamaa akatia gear chap ikabidi nindandie chap nyuma na kuwaambia jamaa zangu waendelee na safari Mimi nicheze huyu mkushi. basi chuma imeenda hadi mataa ya tabata Mimi nipo nyuma nikaona kwa huu uendeshaji huku nyuma si salama kwangu ikabidi pale mataa niite boda nimekuuliza una mafuta ya kutosha jamaa akadai ndio ikabidi nipande boda na kumwambia fuata hii gari.... mataa yakaruhusu jamaa akang'oa na sisi tukang'oa na boda... kufika buguruni jamaa akashika njia ya kkoo mpaka mataa ya ilala, pale akashika njia ya keko mpaka taifa, taifa akashika Mandela mpaka tazara na kukunja kushoto uelekeo airport ila pale akasimama kumshusha mshikaji mmoja hivyo kwenye gari wakabaki wawili dereva na mmama na na mimi nilishuka pale kwenye boda kumfuata ila aliendelea kuongea mbovu.. basi pale safari inaanza tena, jamaa alitupeleka mpka chanika huko mbali sana na mpaka tulipokuta kapata ajali nyingine tena ya kugonga Carina na yeye gari yake kupinduka. sasa huku nyuma kumbuka alitugonga wawili kumbe Yule mdada alikuwa ni mjomba wake na kova so taarifa ilikuwa ishapelekwa na Yule dada aliomba mawasiliano yangu kwa jamaa hivyo baada ya kuwa tumemdaka nikamjulisha Yule dada ndani ya dakika 10 ikaja pale cruiser police wakaniambia tu wewe nenda ila asubuhi saa nne uende pale urafiki kituo cha police.... asubuhi nikafika pale nikamkuta mkushi kawa mpole kuliko maelezo kama sio Yule wa Jana plus Yule dada ... ikabidi mafundi waje pale wakadirie gharama na jamaa akatoa... sijajua walimalizana vipi na wa CARINA maana ilikuwa haifai.... kama upo humu nisamehe bure ila hukuwa muungwana ndo maana tulifika Ile hatua...